Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote niwashukuru Mawaziri na niwapongeze sana kwa collabo nzuri ya kupiga kazi, hakika inatupendeza sana. Tunaona kabisa kwamba mafanikio makubwa yanakwenda kupatikana kwa kuunganika kwenu na kufanya kazi pamoja kwa bidi. Ni mfano mzuri tuwaige Mawaziri hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kwenye Wizara hii ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa kwenye GDP ya Taifa letu. Mkoa wa Tanga nasi tumebarikiwa kuwa na Hifadhi ya Saadan kwa kilomita zaidi ya 1,062. Hii Hifadhi ya Saadan ni hifadhi ya kipekee kabisa Afrika Mashariki kwa kuingiliana na Bahari ya Hindi. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa uoto huu wa asili, lakini lazima tukiri kuna changamoto ambazo zinatukabili ku-enjoy zawadi hii ya Mwenyezi Mungu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Wilayani Pangani kuna vijiji ambavyo vinataabika mno kwa kutokuweza kuwa-control wanyama waliopo ndani ya Hifadhi ya Saadan. Kwa mfano, Kijiji cha Buyuni kiko ndani ya Hifadhi ya Saadan, pia Kijiji cha Mikocheni, Sange, Mkalamo, Bulizaga hivi vyote vinaathirika mno kwa tembo wengi sana ndani ya hifadhi ile. Vijiji hivi vimekuwa vinasua sua katika kilimo kwa sababu ya kuwepo kwa tembo wengi sana, lakini hata miundombinu ya barabara ambazo barabara zetu ni za gravel zinapata shida mno kwa sababu ya uwepo wa tembo wengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Afisa Mhifadhi Mkuu anakiri wazi kwamba tembo hawa ni wengi wananishinda nguvu. Nahofia kumwambia kaka yangu wa Songea tuongozane wote, lakini natamani kabisa Mawaziri hawa watoke pamoja tuone namna gani tunakwenda Pangani tushirikiane na watendaji wa Pangani kuweza ku-control hali ile. Tembo wanaingia kwenye mashamba kuanzia saa 12.00 jioni na wanatoka saa 1.00 asubuhi na ni hatari kwa watoto wetu wakati ambapo wanakwenda mashuleni. Tunaomba sana sana tuunganike kwa pamoja tukatatue changamoto zilizopo Wilayani Pangani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia pia kule Handeni, vijiji viwili na wananchi wawili walishawahi kuuawa kwa ajili ya tembo. Tuone namna nzuri ya kupambana kwa pamoja kwenda kuziondoa changamoto hizi, ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali kupitia Wizara hii ya Maliasili na Utalii iliwahi kutoa zuio kwa kusafirisha viumbe hai kwenda nchi za nje. Miongoni mwa viumbe hai vilivyozuiliwa ni pamoja na vipepeo wanaozalishwa na watu binafsi katika Wilaya ya Muheza, Mkoani Tanga. Kwa kuwa basi, katika hotuba ya Mheshimiwa Rais, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, alitoa wito kwa Watanzania tufuge wanyama mbalimbali na viumbe hai kwa ajili ya kujiongeza kiuchumi. Je, Wizara hawaoni kuendelea kuliweka zuio linaendelea kuwadumaza wananchi waliokuwa wakifuga vipepeo hao kiuchumi? Ionekane haja sasa kwenda kuliondoa zuio hili ili wananchi waweze ku-enjoy kufanya biashara ile ya kusafirisha viumbe hai kuvipeleka nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuongeza basi mapato ya Wizara hii ya Maliasili na Utalii, nasi tujaribu kujikita kuzifanya hizi routes zetu za ndege zinapopita nazo zi-move zifanye maneuvering around a Mlima Kilinjaro. Naziona juhudi za Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kuutangaza Mlima Kilimanjaro kwamba upo Nchini Tanzania, lakini wenzetu hiyo ndiyo technic wanayoituma. Niliwahi kumpa mtu zawadi ya kahawa ya Kilimanjaro, nikamwambia kawaha hii inatoka Tanzania ananikalia inatoka ananiambia inatoka Kenya. Nikamwambia tu-google hapa, tulivyo google ndio akakubali kwamba kama Kilimanjaro ipo Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, aliniambia, nilipoingia Nairobi, nilipitishwa maeneo yale nikauona Mlima wa Kilimanjaro kwa mbali kwa hiyo sisi tunashindwaje ku-coordinate na ATCL kuhakikisha kwamba ndege zetu nazo zinafanya maneuvering around area ya Mlima Kilimanjaro ili tuweze kuwavuta watalii zaidi nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tuone haja basi ya kutengeneza festivals ambazo kila mwaka zitakuwa zinafanyika au kwa season maalum na zitangazwe all over the world kuhakikisha watalii zaidi wanakuja nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)