Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia fursa na mimi siku ya leo niwe miongoni mwa wachangiaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya pamoja na changamoto ambazo zinajitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama mchangiaji wa kwanza alivyoanza kuchangia kuhusiana na tatizo la tembo, nami ni miongoni mwa waathirika wakubwa sana katika Wilaya ya Kalambo imekuwa ni historia ambayo hatujui imetoka wapi kwa sababu tunaambiwa zaidi ya miaka 100 tembo walikuwa hawapo katika eneo letu la Kalambo, lakini kwa sasa hivi imekuwa kama ni mifugo ambayo inaongezeka kwa kasi kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri analijua hili na nimekuwa nikiwasiliana naye na wananchi wanatuambia kwamba enzi za mkoloni walikuwepo Maafisa Wanyamapori ambao walikuwa stationed pale. Sasa hivi ninachoomba wahakikishe kwamba wanakuwepo ili kutoa utaalam, lakini pia kuwaswaga tembo hao ili wasiendelee kuharibu mazao ya wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo naomba kwa leo nichangie; wamechangia wachangiaji waliotangulia kuhusiana na circuit ku-promote upande wa Nyanda za Juu Kusini ikiwemo pamoja na Katavi lakini na Kalambo Falls. Kalambo Falls ndio maporomoko ya pili ya Afrika baada ya Victoria Falls; hili nalisema kwa mara nyingine nikiamini sasa hivi Serikali inaenda kuweka nguvu yake kubwa kufanya promotion katika maporomoko ya Kalambo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Scenery nzuri ipo upande wa Tanzania lakini wenzetu wa Zambia wamekuwa wakitangaza as if scenery nzuri ipo upande wa kwao. Sasa nimwombe Mheshimiwa Waziri pamoja na watalaam wake na Katibu Mkuu yupo, akiwa TANAPA tuliomba kwamba sisi Halmashauri ya Kalambo hatuna uwezo wa kutangaza, tuliwaomba wachukue maporomoko ya Kalambo kuyatangaza, lakini nini ambacho kimetokea, TFS ambao wana Hifadhi ya Msitu wa Kalambo wamechukua pamoja na maporomoko ambayo hawana uwezo wa kutangaza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachoomba, TANAPA ndiyo wachukue maporomoko, ule msitu ubaki na TFS lakini isiwe TFS ndiyo wachukue na Maporomoko ya Kalambo kwa sababu hawana uwezo wa kutangaza. It’s high time kwamba tutangaze Kusini Nyanda za Juu ikiwemo pamoja na Maporomoko ya Kalambo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namsihi sana Mheshimiwa Waziri, najua ana changamoto ya kibajeti, lakini kwa namna ambayo tunaweza kuchachusha, utalii ni pamoja na kuhakikisha kwamba maeneo yale ambayo hayajatangazwa, yanatangazwa na yanakuwa kivutio, sio kila wakati iende kaskazini, kaskazini imeshakuwa saturated, it’s high time kwamba sasa hivi tutangaze kuelekea huko ambako kuna mambo mazuri sana kwa ujumla yakitangazwa Taifa letu litanufaika wakati tunaendelea na changamoto za huko kwingine ambako watu hawapendi tena kwa sababu tumekuwa tukizidiwa na wenzetu wa upande wa Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri afike, kila Waziri ambaye amehudumu katika Wizara hii akifika Kalambo anakuja na picha, ndio inakuwa kwenye budget speech yake. Akawaulize Mheshimiwa Maige, Profesa Maghembe, Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla mpaka kuna point wakati anateremka aka-faint pale tunaita Kigwangalla Point na yeye aende, hakika hatojutia kwenda kuona Maporomoko ya Kalambo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango huu, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)