Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Waziri na timu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu waliofanikiwa duniani ni wenye jeuri ya kuthubutu. Nakuomba Mheshimiwa Waziri tusiache kuthubutu kuibua maeneo mengine mapya ya utalii kwa sababu waliofanikiwa duniani ni wenye jeuri ya kuthubutu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kwenye eneo la sheria tunasema kama huna vielelezo, haujafanya utafiti, usiongee. Mwaka 1996/1997 nilikuwa Mombasa, Kenya, sehemu moja inaitwa Mtwapa katika hoteli moja ya Serena. Nilikutana na mtalii mmoja akaniambia maneno yafuatayo: amekuwa akiitembelea Kenya na Mombasa for the last 15 years, hana kitu kipya cha kuona, anafikiria aende ama South Africa au kwingineko. Ujumbe anaouleta ni nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, aina hii ya watalii tunatakiwa ndani ya nchi yetu tusiwapoteze kwa kuibua maeneo mengine mapya. Kama this time around alikuwa Kaskazini, next time aende Magharibi, the other time around aende Mashariki, hivyo. Kwa hiyo, huyo tuna uwezo wa kumhifadhi ndani ya nchi yetu, lakini kwa kuboresha maeneo mengine. Nilikuwa naliomba hilo sana na hiyo ndiyo tabia. Naomba niwapitisheni, mtalii ni nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana, tutajikita kutengeneza hoteli nzuri, mbuga nzuri, lakini tusipomtambua mtalii na tabia yake, hizo hoteli Wazungu wanasema zitakuwa ni white elephant. Kwanza mkumbuke mtalii ndio bosi wetu. Kama bosi wetu, ana tabia zifuatazo; tusipotii kiu yake hana nafasi ya kuja kwetu. Kwa hiyo, nilichokuwa nawaomba Waheshimiwa, lazima tujikite kwenye kujua mahitaji ya mtalii. Ni mtalii gani tunayemlenga?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu ukiorodhesha, nikiacha watalii wa ndani ambao ni Watanzania wenyewe, lakini hata hao watalii kuna kundi la watalii huko kwenye kada, wengine wanasema watalii vishuka. Kuna mtalii ambaye tunaweza tukabanananaye mtaani, tunakula wote muhogo wa kuchoma, anatembea pekua na vitu vingine kama hivyo, hatukatai, naye tunamhitaji. Ila kuna mtalii mmoja anakuja kwenye nchi yako, mtalii huyu akiridhika na kazi zetu na huduma zetu; leo tunauliza habari ya kwenda kutangaza CNN na kwingineko, yeye mmoja ana uwezo wa kubeba dhamana hiyo akiridhika na huduma yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tunaambiwa kwenye Hotel Industry, kwenye utalii kwa ujumla wake ni Hospitality Industry. Kwa hiyo, tusipokuwa watu wa kutii kiu ya watalii, itabaki kuwa ni gumzo.

Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana. Sasa ili tukawapate watalii wa daraja hilo, je, tumejikita katika mahitaji yake ya kimsingi? Leo kwa mfano, tuna hoteli kweli za viwango vile? Tuna hoteli ambazo zinaweza leo ukisema mtalii mmoja makini wa kutoka Marekani amekuja hapa tunaweza tukam- accommodate? Hayo ni mambo tuendelee kuyaangalia. Mtu anayehitaji labda huduma, bima, anahitaji flying doctors, hayo yote kweli tunayo? Ni vitu vya kimsingi sana kuviangalia. Maana mwingine anasema, nakwenda Tanzania, nime-fall sick, nimeugua sasa hivi, huduma nazipata wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nashukuru Marais wote ambao wameendelea kuboresha huduma zetu hapa nchini hata kama ni kwa maana ya first aid ataipata nchini kabla hata hajaruka kwenda kwenye nchi yake, ni jambo la msingi sana. Naomba tena tuendelee kuelewa leo tuna trained personnel kweli kweli jamani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda baadhi ya nchi za watu, ile tu umefika kwenye nchi yao, even tax driver wamekaa kistratejia. Tax driver tu ukiwanaye kwenye gari anaiuza nchi yake. Umwache huyo, ukikuta kama ni air hostess wanauza nchi zao. Ukimkuta kama labda ni waiter au waitress, umekaa hotelin,i dakika mbili za kukaa pale yuko well trained, anajua kwamba nifanye nini katika kuiuza nchi yangu. Huko tuendelee kwenda kwenye namna hiyo ya kufanya shughuli zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba pia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Ooh! Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Naunga mkono hoja.