Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema zake ikiwemo uzima na afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba ambayo pia ameisoma kwa umahiri mkubwa sana. Serikali ya Awamu ya Tano ni Serikali ya Viwanda, napenda kuishauri Serikali kama tunataka kufikia lengo hili kwa ufanisi ifuatavyo:
Maeneo yote ya EPZA na SEZ ambayo hayajalipiwa fidia yakiwemo ya Kurasini, Bagamoyo na Mtwara wahakikishe kuwa fidia hiyo inalipwa kwa wakati na kusafishwa ili wawekezaji wasipate usumbufu juu ya upatikanaji wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu wezeshi, umeme wa uhakika, barabara na reli ni muhimu sana ili kuhakikisha tunazalisha bidhaa ambazo zitaweza kushindana na bidhaa nyingine kutoka nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kupata majibu kutoka kwa Waziri kuhusu suala la kiwanda cha Mbolea Msangamkuu Mtwara, ningependa kufahamu ni lini kiwanda hicho kitapatiwa uhakika wa kupewa gesi ili kiwanda hicho kianze kujengwa ninafikiri kushika shilingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunataka kweli kuwa nchi ya Viwanda, Serikali yangu ni lazima tuweke sheria za maksudi kwa ajili ya kulinda viwanda vyetu. Nchi yetu ina uwezo wa kuzalisha alizeti na mafuta ya alizeti na kulisha Afrika Mashariki, lakini tunashindwa kwa sababu ya mafuta ya kutoka nje ambayo hatuna hata uhakika wa usalama wa afya zetu. Naomba Serikali iondoe usumbufu kwa wawekezaji, tuangalie sheria zetu za kodi, utaratibu wa kupata ardhi kwa wawekezaji na kuthubutu kutoa maamuzi kwa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, viwanda vya korosho ni muhimu sana kwa maendeleo ya wakulima wa korosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.