Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano iliyoongozwa na Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi zinazoendelea kufanyika za kusambaza umeme kwa nchi nzima. Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati umeandaliwa vizuri. Pia nampongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa utendaji mzuri.

Mheshimiwa Spika, nashauri mambo yafuatayo. Naishauri Serikali kuendelea kusimamia na kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara. Pia nashauri Serikali iedelee kusambaza umeme katika Vijiji na Vitongoji ambavyo bado havijafikiwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, napendekeza Serikali iendelee kukamilisha ujenzi wa Bwawa la Umeme wa Mwalimu Nyerere ili kupata umeme wa uhakika. Pia napendekeza Serikali kuendelea kufanya utafiti wa mafuta, gesi na vyanzo vingine vya kuzalisha nishati ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa Nishati.

Mheshimiwa Spika, nashauri pia Serikali iendelee kuanzisha vituo vya usimamizi katika ngazi ya Tarafa ili kusaidia kutatua changamoto za kiufundi zitakazojitokeza. Vile vile iendelee kusambaza umeme. Kuna changamoto ya uhaba wa upatikanaji wa Transfoma hivyo kuchelewesha usambazaji wa umeme. Hivyo, Serikali isimamie uzalishaji wa Transfoma za kutosha.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali iendelee kusimamia usambazaji wa nishati ya gesi kwa matumizi ya majumbani.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.