Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza Waziri pamoja na timu yake yote kwa kazi kubwa wanayoifanya. Pia niendelee kuwapongeza kwa kuwaagiza Wakandarasi wawe wanawasiliana na Waheshimiwa Wabunge. Nawapongeza sana.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Lushoto lina Kata 15 na baadhi ya Kata, umeme umepita maeneo ya barabarani tu. Kwa hiyo, kumekuwa na malalamiko mengi sana kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Lushoto. Hata hivyo, namshukuru Waziri kwa kutoa maagizo yake ya kuhakikisha vijiji vyote vya Jimbo la Lushoto vipatiwe umeme. Wasiwasi ni Wakandarasi: Je, watafanya hivyo kweli? Kama hivyo ndivyo, naomba niorodheshe vijiji vyangu vyote ambavyo havina umeme kabisa, pamoja na vitongoji vilivyorukwa.

Mheshimiwa Spika, hivi ndiyo vijiji ambavyo havina umeme kabisa. Gare, Yamba, Kongei, Masange, Boheloi, Kwemashai, Ngulu, Miegeo, Handei, Milungui, Kireti, Kwemakame, Mazumbai, Ntambwe, Kigumbe, Bombokamgobolo, Kilole, Mbelei, Mavului, Mazashai, Kigulunde, Mdando, Kweulasi, Bwaya, Kwetango, Bombo na Ngulwi Chumbageni.

Mheshimiwa Spika, hivi ndiyo vijiji ambavyo havina umeme kabisa. Pamoja na hayo, kuna Vitongoji zaidi ya 27 navyo vimerukwa. Kwa hiyo, naomba Serikali ivipatie Vitongoji hivyo vilivyorukwa na umeme ili kuepuka malalamiko ya wananchi waliokosa umeme na wakati huo huo wanauona umeme unawaka kwa jirani.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, wananchi wa Lushoto wana uwezo mkubwa wa kuweka umeme, lakini wanakwamishwa na watu wa TANESCO, kwa kuwaambia umeme bado ni shilingi 177,000. Hili suala linawakatisha tamaa wananchi wa Lushoto. Kama hivyo, basi naiomba Serikari itoe waraka wa kutoa bei elekezi kwa wananchi ili kuepuka usumbufu kwa wananchi wanaoupata kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.