Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza sana Waziri wa Nishati na Naibu wake pamoja na jopo la wataalamu wa Wizara kwa kazi kubwa wanazofanya kwenye kuipeleka nchi yetu kwenye Tanzania ya Wiwanda kwa mchango wao mkubwa kwenye sekta ya umeme.

Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali, bado wananchi wengi wa Jimbo la Moshi Vijijini hawajapatiwa nishati ya umeme kupitia mradi wa umeme vijijini (REA).

Mheshimiwa Spika, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 inaelekeza kwamba kufikia 2025, vijiji vyote Tanzania vitakuwa vimeunganishiwa umeme. Upatikanaji wa umeme vijijini utachochea kuboreka kwa maisha, ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kama zile za kuchomelea vyuma, gereji, maduka, salon za kunyoa na kutengeneza nywele na mabanda ya kuonyesha mpira.

Mheshimiwa Spika, ni kutokana na ahadi hii, ninaiomba Wizara ya Nishati isaidie kutatua changamoto za nishati ya umeme katika Jimbo langu la Moshi Vijijini. Kukosekana kwa umeme katika baadhi ya vijiji na vitongoji jimboni kwangu kunawafanya wananchi kuingia gharama kubwa ya kununua mafuta ya taa kila siku ili waweze kupata mwanga nyakati za usiku.

Mheshimiwa Spika, maeneo yenye changamoto ya umeme Jimbo la Moshi Vijijini ni katika Kata ya Kindi, Kijiji cha Chekereni Weruweru, Vitongoji vya Miembeni, na Kisiwani havina umeme kabisa. Mbunge ametokea Kata ya Kibosho Kirima. Katika Kijiji cha Boro kwenye Vitongoji vya Boro Kati na Boro Juu (anakotokea Mbunge), voltage za umeme ni ndogo sana na hupelekea kushindwa kuendesha vifaa vya ndani kama friji na vyombo mbalimbali vya ndani. Mashine za Welding (kwenye vitongoji hivi) na pump ya kuvuta Maji Masoka Sekondari hushindwa kufanya kazi kutokana na umeme mdogo. Shule hii ina wanafunzi zaidi ya 800.

Mheshimiwa Spika, wajasiriamali wameshindwa kuweka mashine za kusaga unga, mashine za kutengeneza matofali na miradi mingine midogo inayohitaji umeme wa uhakika. Wanafunzi wa bweni wa Sekondari ya Masoka hushindwa kupata huduma ya umeme ili wajisomee usiku kutokana na umeme mdogo. Umeme huwaka kuanzia saa
5.1 usiku. Naomba Wizara isaidie kutatua changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Okaoni, Vijiji vya Sisamaro, Omarini na Mkomilo vinahitaji kuunganishwa japo baadhi ya maeneo nguzo zimepita ila bado kuunganishwa. Kata ya Kibosho Mashariki inahitaji huduma. Katika Kijiji cha Sungum Vitongoji vya Kyareni na Nkoitiko havijaunganishwa. Katika Kijiji cha Singa, Kitongoji cha Singa Juu hakijaunganishwa. Katika Kijiji cha Mweka, Kitongoji cha Mweka Juu na Omi havijaunganishwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Kibosho Kati, baadhi ya maeneo ya Kijiji cha Uri hakijaunganishwa. Kwa ujumla, katika vijiji vya Otaruni na Uri, kuna changamoto ya ukosefu wa umeme kwenye baadhi ya Vitongoji. Pia kuna tatizo la umeme kidogo (low voltage) kwenye vijiji hivyo. Tunaiomba Serikali iweke Transfoma za kutosha ili kukabiliana na tatizo hili.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Uru Mashariki, Kijiji cha Materuni, Kitongoji cha Wondo hakijaunganishwa. Walichimba mashimo kwenye baadhi ya maeneo na kuleta nguzo tokea mwezi wa Tisa mwaka 2020 na hawajarudi tena. Katika Kata ya Mbokomu, Kitongoji cha Mmbede Kyaroni, Tema na Masanga na baadhi ya maeneo ya Korini Kati havijaunganishwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Mabogini sehemu ambazo hazijapata umeme hadi sasa ni kama ifuatavyo:-

(1) Vitongoji vya Sanya “Line A” na Mjohoroni vilivyopo katika Kijiji cha Mabogini.

(2) Kitongoji cha Uru, katika Kijiji cha Muungano;

(3) Katika Kijiji cha Maendeleo, Vitongoji vya Mshikamano na Uarushani;

(4) Mgungani katika Kijiji cha Mtakuja;

(5) Katika Kijiji cha Mserekia, hakuna umeme katika Vitongoji vya Mbeya kubwa, Mbeya ndogo, Remit, Mkwajuni na Mafuriko. Vilevile Kijiji cha Mji mpya, Kitongoji cha Utamaduni hakijaunganishwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Mabogini wapo wananchi waliofanya wiring lakini surveyor hawaji kukagua ili waruhusiwe kulipia; pili, wapo wananchi ambao wamesharudisha form na hawajaitwa kwenda kulipa ili wawashiwe umeme. Tunaiomba Wizara ifuatilie jambo hili.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Old Moshi Magharibi Kitongoji cha Saningo katika Kijiji cha Mandaka mnono hakina umeme kabisa. Kata ya Kimochi Kitongoji cha cha Kiwalaa kilichopo Kijiji cha Sango, Kitongoji cha Iryaroho kilichopo katika Kijiji cha Mowo na Kitongoji cha Maryaseli katika Kijiji cha Lyakombila havina umeme.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali ikamilishe ujenzi wa miundombinu ya umeme katika maeneo niliyotaja hapo juu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha umeme wa kutosha unapatikana katika maeneo yote ya Jimbo la Moshi Vijijini. Hili litafanikiwa ikiwa Wakandarasi watalipwa kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, vilevile, naishauri Serikali iwe na programu ya kuwaelimisha wajasiriamali wa vijijini kuhusu fursa zilizopo vijijini, na ni kwa namna gani wanakijiji wanaweza kutumia nishati hii kujiajiri na kuongeza thamani ya bidhaa zao?

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo yangu hapo juu, naunga mkono hoja.