Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nishukuru kiti chako kwa ufupi. Pili, naomba niseme kwamba ninashikiri au niko kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama. Nimekuwa nikijaribu kuwasikiliza Waheshimiwa Wabunge hapa kwa muda mrefu toka tumeanza Bunge kuna jambo linaendelea kujitokeza sana. Sasa naomba hasa wenzetu wa Serikali hili walitafakari tena kwa kina na hatua za dharura zichukuliwe.

Mheshimiwa Spika, mara nyingi tunapata mafunzo au tunachukua hatua tunapoona matokeo yanazidi kukithiri. Siku chache zilizopita tulisikia tatizo dogo kutoka kutoka TRA kwamba mifumo kila siku iko chini lakini baadaye tukasikia tatizo la TANESCO kwamba watu hawawezi kununua LUKU lakini hapa kiongozi amerudia tena kuongelea suala hili inaonekana limerudiarudia. Ombi langu kwa TANESCO, tuko kwenye cyber war, kuna kitu tunaita cyber war na kitu tunaita cyber-crime, umeme ndiyo unaotumika kupeleka athari zote kwenye mifumo yetu. Naomba sana na hili TANESCO mliangalie sana, vinavyotokea havitokei kwa bahati mbaya, ni mambo yanayopangwa na yanapangwa yatokee ili siku moja tu-collapse. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie wenzetu kwamba TANESCO tumewapa kuongoza Serikali kwa sababu leo maji tunalipia kwa internet, umeme tunalipia kwa internet maana yake ni kwamba hata benki zetu zinatumia internet kufanya mambo yake maana yake ndiko kelele ziliko. Hata hivyo, internet leo inawezeshwa kupitia kwenye umeme, ombi langu kwa TANESCO haya mambo hayaji kwa bahati mbaya iko siku sote tuta-faint kwa sababu tunaelekea kwenye cashless economy ni kwamba ni mitandao ndiyo inayotuwezesha kufanya mambo yote maana yake tumewapa kuendesha Serikali kwa kutumia umeme. Tunawaomba sana muwe makini na suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mkiangalia attempt zinazofanywa BoT, iko siku tutawaomba hapa waje watuambie attempt za mara ngapi zinafanywa kwenye benki zetu kwa kutumia internet ambazo zinapitia kwenye umeme. Tunawaomba sana tumewapa shirika hili au taasisi hii muweze kutulindia nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waziri Mkuu alitukumbusha kwenye backup maana yake tuweze kujilinda lazima tuwe na plan B na plan C kwenye kujilinda ili tusifikie siku tukawa hatuwezi au kila kitu kime-paralyze kwa sababu ya internet kumbe siyo internet ni kwa sababu ya umeme. Kwa hiyo, nawaomba sana mlitilie maanani suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili naomba uendelee kutusaidia wataalam wetu walikumbuke kwamba umeme ndiyo unaotumika kupitisha kila kitu. Juzi Marekani nadhani mmeona wataalam, Serikali ya Marekani ililazimika kuwalipa wataalam wa IT ambao huku tunawaita hackers, si kwa sababu walipenda kwa sababu system zao za mafuta ziliingiliwa na hackers, waliwalipa! Pamoja na policy zao kwamba hatuzungumzi na watu ambao hawahusiki na system zetu lakini waliwalipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba shirika letu au Wizara yetu ilisimamie suala hili ili kuhakikisha kwamba hatufiki mahali tukashindwa kufanya mambo yetu kwa sababu tumeshindwa huko. Lazima tuwe na wataalam wetu wa ndani ambao watalinda mifumo yetu ili tusishindwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)