Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu na niwapongeze sana Mawaziri na Naibu wake kwa utekelezaji mzuri wa majukumbu yao. Vilevile nimshukuru na kumpongeza sana Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati kwa wasilisho zuri ambalo limetupa guidance ya kutosha kuweza kuchangia hotuba hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni hivi karibuni tunaona nchi zetu mbili na Marais wetu; Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Uganda wakitia saini ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima mpaka Chongoleani Jijini Tanga. Kwa mujibu wa maelezo ya mradi huu unatajwa kwamba takriban ajira 6,000 – 10,000 zinaweza kutokea na kuna fursa nyingi sana za kibiashara zinaweza kutokea kwa watu ambao mradi huo utapita. Naomba kuishauri sana Wizara i-manage expectations za wananchi wetu katika maeneo ambayo mradi huu unapita. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yangu ni nini? Tusije tukawaahidi wananchi wetu kwamba kutakuwa na fursa nyingi sana za kibiashara mwisho wa siku ikawa kinyume chake. Tunaiomba Serikali na kuishauri ituletee tathmini walioyofanya katika ujenzi wa TANZAM wakati wanajenga bomba ya mafuta kutoka Tanzania mpaka Zambia fursa gani zilipatikana na za aina gani na wananchi waweze kujiandaa. Vilevile tulipojenga bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam watuletee tathmini ya ajira na fursa za kibiashara ambazo wananchi waliweza kufaidika ili watu wetu waweze ku-manage matarajio yao ili mradi ule ukafanyike vizuri bila kusabbisha chaos wakati wa utekelezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile naomba sana kuishauri Serikali i-coordinate na Wizara nyingine ambazo zitarahisisha utekelezaji wa mradi huu. Tunafahamu kwamba wakati wa ujenzi huu kutakuwa na huduma za consultation kati ya wataalam wa mradi na ninyi wataalam wa Serikali, ina maana kwamba kutakuwa na safari nyingi sana kati ya Tanga na Dodoma, kati ya Tanga na Uganda kwa ajili ya consultation za utekelezaji wa mradi huu. Hata hivyo, inashangaza ninyi Wizara ya Nishati mmekaa kimya, Kiwanja cha Ndege cha Tanga hakijajengwa mpaka sasa, mna mpango gani na wataalam wa mradi huu hamuoni kama mtawasababishia difficulties katika utekelezaji wa kazi zao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mnafikiri Hayati wetu alipotoa ahadi ya kutekeleza ujenzi wa kiwanja kile pale Chongoleani wakati anazindua mradi huu maana yake ilikuwa ni nini? Maana yake ni kutaka ku-facilitate utekelezaji wa mradi huu kwa haraka. Kwa hiyo, niiombe Serikali kwa maana ya Wizara ya Nishati ya Madini ika-coordinate vyema na Wizara ya Ujenzi ili Kiwanja cha Ndege cha Tanga kijengwe haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile katika mradi huu tunafahamu kwamba gesi itachimbiwa ardhini kwa maana ya lile bomba lakini tunafahamu kwamba lazima kuwe na facilities kama za zima moto katika maeneo yote ambayo bomba hili litapita. Wizara hii inapaswa ku-coordinate na Wizara ya Maji kuhakikisha maeneo yote yale ambayo mradi huu unakwenda kupita kunakuwa na maji ya kutosha incase kama bomba linakwenda kuvujisha lazima tuwe na tahadhari za kutosha kuhakikisha wananchi wetu wanaendelea kuishi salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunashukuru kwa upande wa Chongoleani kaka yetu Mheshimiwa Aweso maji yamekwenda lakini maji yale hayatoshi. Ni lazima tujenge water high drinks za kutosha katika maeneo yale ili wananchi wetu waweze kuishi salama.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)