Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ambayo nilipaswa kuchangia asubuhi lakini nikaamini kwamba umeniweka akiba.

Mheshimiwa Spika, naomba kumpongeza sana Waziri wa Nishati na Naibu wake, Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa REA Vijijini bwana Maganga kwa kazi kubwa ambayo wameifanya kwenye nchi hii katika kuhakikisha kwamba umeme unapatikana wa uhakika pamoja na matatizo madogo madogo, lakini angalau wananchi wanaendelea kupata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye miradi hii ya REA imesaidia sana kufungua maendeleo kwenye vijiji vyetu kila mahali ambapo umeme umewekwa wa REA kuna viwanda vidogo vidogo vimefunguliwa na wananchi kwa hiyo, vimeongeza ajira kubwa sana katika maeneo yetu, lakini pia na kuchangamsha center na ujenzi mpya kabisa wa nyumba za kisasa vijijini sasa unaonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumewahi kutembelea Kamati yetu PAC kule Iringa pamoja na Manyara na Singida tumekuta kule vijijini wananchi wako happy kabisa kwa sababu ya kuona umeme vijijini umekwenda na ninawapongeza na Waziri kwa kweli Mungu amempa kipaji cha kukariri vijiji vyote vilivyoko hapa Tanzania. Kwa hiyo, nakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa kweli umeme walipofanya evaluation uliongeza tija kwa sababu scope zilizokuwa zimeandaliwa mwanzo zilikuwa chache sana na hii imeifanya CCM kupata kura nyingi baada ya umeme huu wa REA kufika vijijini. Kwa hiyo, kwa sina kipingamizi cha kupitisha bajeti ili wakatekeleze hasa kwenye vijiji vyangu 42 ambavyo vimebaki kule jimbo la Magu, Kalemani anavijua na Maganga anavijuwa kwa sababu wamekwenda kule karibu mara nne kwenye maeneo yetu, vijiji vya Isolo, Shishani, Ingombe, vyote wanavifahamu, vijiji vya Chandulu, Mwabulenga, Kisamba vyote wanavifahamu, kwa hiyo, nahitaji hivi vijiji 40 viweze kufikiwa umeme wa uhakika ili wananchi waweze kuwekeza viwanda vya kuchakata mazao mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili ni suala la KVA wamiliki wa viwanda wanalalamika wanamatatizo, kwamba unapofanya kazi kwenye viwanda, ni mdau wa kiwanda naomba ni declare interest unapochambua pamba miezi miliwi, ukikata umeme unachajiwa KVA miezi mitatu bure unalipa hewa. Kwa hiyo, kama mazao yapo umekusanya kidogo ukachambua kwa muda mfupi unaingia hasara tena za kuilipa TANESCO bure, miezi mitatu hii inakatisha tamaa wawekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano kama mwezi wa kwanza ulilipa bill ya milioni 60 na mwezi wa pili ukalipa bill ya milioni 60 maana yake miezi mitatu utalipa milioni 60 mara tatu milioni 180, ndiyo maana wawekezaji wanashindwa hata kule kwako Kongwa, mwekezaji mkubwa wa kiwanda cha Oil Meal Kahama, alikula kwa miezi michache tu mbegu zikaisha. Kwa hiyo, akashindwa kwa sababu faida yote aliyoipata akalipa KVA, pamoja na hasara zingine kwa hili linaleta shida na sheria hii ilitungwa wakati tunatumia umeme wa mafuta IPTL. Kwa hiyo, sasa tunatumia umeme wa kwetu tuondoe hii sheria ili tuweze kuwasaidia wafanyabiashara wa viwanda waweze kuchakata hatuwezi kuvutia wawekezaji kama tunafanya jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na hili waziri haliitaji wadau kwa sababu tunataka kuongeza wazalishaji na wasindikaji wa mazao yetu ili alizeti Kongwa Singida, Dodoma Mwanza ilimwe watu wakitegemea viwanda vyao vitafanya kazi kwa murefu bila kulipa KVA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilizungumze kidogo hili la vinasaba na niweke vizuri kumbukumbu kwamba SIPA ndiye aliyekuwa mwenye Kampuni ya kuuza vinasaba na kuweka vinasaba kwenye nchi mbalimbali, lakini Msumbiji walimfukuza, Uganda walimfukuza, Kenya walimfukuza, Brazil walimfukuza, akaja hapa kwa namna fulani fulani akaanzisha kampuni ya GFI, GFI ndiyo inayonunua vinasaba kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo, uwamuzi wa Serikali hii sikivu wa kuipa TBS wa kushughulika na hili jambo ni uhamuzi sahihi kabisa. Kama kuna watu labda wametumwa kuja kumpigania mnyonyaji washindwe na walege. Kwa sababu, tunajua kwamba TBS ndiyo tumeipa kazi sasa na yenyewe TBS inanunua hivi vinasaba kwa SIPA. Kwa hiyo, tunaamini kwamba TBS itakavyo endelea itatengeneza teknolojia ya kwakwe kuhakikisha kwamba vinasaba hivi hivi vinapatikana hapa hapa au duniani sehemu nyingine. Lakini fedha zile ambazo TBS italipwa hizi shilingi 14 zitabaki kwa Serikali yetu hata kama kuna shida ya reli, kuna shida ya umeme hizi fedha zitasaidia kuliko kuipa kampuni nyonyaji hatuwezi kurudi huko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge ni mdau wa mafuta pia, siwezi kutetea kampuni nyonyaji, lazima tuitetee nchi na nchi ifanye kazi TBS inauwezo mkubwa wa kuweza kusimamia hili jambo bila matatizo yoyote. Kwa hiyo, niseme tu kwamba nchi imeamua sahihi na tuhakikishe kwamba tunapokuwa wazalendo, lazima tuangalie vitu vyenye tija siyo vitu ambavyo vinaipunguzia Serikali fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi fedha halipi mfanyabiashara, hizi fedha EWURA wanapotengeneza mkokoto wa mafuta, kwamba Mwanza petrol itauzwa 2,400/= kama ilivyo leo maana yake kwamba anayelipa ni mtumiaji wa mwisho. Kwa hiyo, tunaamini kwamba baada ya TBS kukaa vizuri wanaweza kuwa wanataja hata shilingi saba kama ambavyo mwezangu Boniface hapa amesema maana yake shilingi saba inaweza kupelekwa kwenye TARURA, inaweza kupelekwa kwenye maji tukaongeza mifuko hii ya kutekeleza miradi yetu tukaweza kuwasaidia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niunge mkono kwa sababu Wizara hii Waziri mwenyewe na Naibu wake anaiweza, unajua hapa duniani kuna watu ambao wanauwezo wa kubeba mizigo mizito na hatuna sababu ya kuwapunguzi hiyo mizigo kwa sababu Nishati, Waziri wanatosha, Wakurugenzi wake, wa REA TANESCO TPDC nao wanatosha wafanye kazi karibu ili kumsaidia Waziri tusipunguze hapo na hayo maneno, tunaweza tukampa mtu akashindwa sasa sisi tuombe sana kwamba tusigawanye wizara huyu anauwezo wa kuibeba Wizara, ameibeba muda wote. Kwa hiyo, niombe sana mpeni kazi aweze kufanya ahsante sana. (Makofi/ Vigelegele)