Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi niweze kuchangia katika Wizara hii ya Nishati. Nipende kumpongeza Waziri na Naibu wake Waziri kwa kazi nzuri. Nimpongeze Waziri kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa, lakini vile vile nipongeze kwa kazi nzuri wanazozifanya hususan katika umeme wa REA vijijini. Pamoja na kazi nzuri wanazozifanya bado tuna changamoto nyingi hususan katika Mkoa wetu wa Tabora. Umeme umekuwa ni wa shida, umeme una katikatika katika wilaya zote zinazopatikana Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mradi mkubwa unaotarajiwa kutengeneza sub-station katika Wilaya ya Urambo pamoja na Sikonge. Urambo kwenda Kaliua mpaka Kigoma na Sikonge kwenda Katavi. Lakini umekuwa mradi ambao ulikuwa na malengo yake yalianza toka mwaka 2016 mpaka hivi sasa ni miaka mitano bado hatujaweza kufikia malengo. Na tatizo kubwa linalokuja hapa mkandarasi ameshapatikana lakini shida ni due diligence ambayo inayochelewesha sana kufikia ukamilishaji wa kupata transformer kuweza kupeleka kwenye huu mradi ulipangwa Urambo na Sikonge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mradi huu toka umeanza kitu ambacho kimeweza kufanyika ni kujenga majengo ya kupokelea umeme na pamoja kuweza ku-identify njia za kupitishia umeme. Lakini changamoto za kupeleka transformer bado ni shida kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, vilevile Mheshimiwa Waziri mwezi wa tatu alikuwa Wilaya ya Igunga pamoja na Uyui kuzindua umeme wa REA ambapo Wilaya ya Igunga waliweza kumueleza wanahitaji kutengenezewa vituo vya kupozea umeme pamoja na Uyui alizindua umeme katika Kijiji cha Ivumba na akaahidi utawaka kuanzia Aprili. Lakini mpaka leo wanakijiji wale wa Izumba wanasubiri sana umeme huo uweze kuwashwa lakini bado haujawashwa zaidi tu ya usumbufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile nilikuwa naiomba wizara iweze kuharakisha huu mpango na mchakato wa kuweza kuhakikisha transformer zinafika kwa wakati katika kujenga vituo vya kupozea umeme katika Wilaya ya Urambo. Tunachangamoto nyingi sana katika Mkoa wetu wa Tabora hususan ni hizi wilaya ambazo nimezitaja umeme unakatika, hatuwezi tukasema Tanzania ya viwanda kama bado hatujawa na umeme unaoweza kujitosheleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kusema watu wajiajiri kama bado tunawakwamisha katika kuhakikisha wanajitafutia kipato na kukuza uchumi wao. Inafikiwa wakati kuna kina mama ambao wengi wamejikiti kwenye kufanya biashara za saluni, vijana na wenyewe saluni za kiume lakini mtu ana mteja umeme unakatika; hakuna utaratibu kwamba leo tutakuwa tumewashiwa kwa siku tatu au nne lakini leo umekaa tu unamuweke mteja rollers umeme umekatika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa Mkoa wa Tabora wananchi wengi wamejikita katika uwekezaji wa mashine za kukoboa na kusaga. Mashine hizo zinatakiwa zitumie umeme, sasa kama umeme hauna nguvu ndio mtu ameweka tu mpunga kwenye mashine yake umeme katika haujulikani utawaka lini tunategemea huyu mtu mapato yake aweze kupata kwa wakati gani. Wakati huo huo TRA bado inamuhitaji kupeleka mapato ambayo yametokana na biashara anayofanya; biashara yenyewe inategemea umeme, umeme unakatika bila ya mpangilio tuweze kuangalia katika huu Mkoa wa Tabora ambao kidogo kila kitu naona kama kinakuwa kipo nyuma nyuma.

Mheshimiwa Spika, tunaomba wizara mturahisishie upatikanaji wa umeme wenye tija, wenye nguvu, ili wanawake hawa wa Mkoa wa Tabora wanaojikita katika shughuli zao za saluni wafanye kazi zao vizuri na shughuli zote zinazotumia umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hivyo naomba niunge mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)