Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Nishati na kabla sijaanza kuchangia nipende kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Waziri kwamba nimepata simu kutoka kwa Engineer Maro na Engineer Said wa TANESCO na Engineer Fumbuka nashukuru sana wamefika kwetu wanasema Wilaya ya Muleba watashughulikia vijiji 22 lakini nikasema mzee wa Mbongoshi mbona niliomba 28?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nashukuru kwa 22 na endelea kuomba kwa vile vinane lakini katika vile vijiji vilivyobaki kuna Kijiji kimoja kina utata, Kijiji cha Bugasha, kilichopo kando kando ya jeshi la Kaboya ambacho kinapiganiwa na watumiaji wetu mzee angaliaangalia uwape kipaumbele vijana wale wana kazi kubwa.

Mheshimiwa Spika, nianze kuchangia, ni mdau wa mafuta ni mtoto wa sekta hii na leo nitachangia nishati upande wa mafuta tu. Najua unajua, niliingia kwenye sekta hii mwaka 1984 nikiwa kijana navaa kaki na malapulapu na radio call nikifungua valve la kupima matenki mapenzi ya Mungu nikapanda mpaka nikawa Naibu Waziri Nishati. yaani kutoka kufungua valve mpaka kuwa Naibu Waziri unaweza kuona mambo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mafuta ni jambo muhimu na katika ukusanyaji wa mapato sekta ya mafuta inasaidia Serikali kukusanya mapato kwa kutumia jasho kidogo. Yaani TRA wanakuta pesa zinakuja mezani kwa kutumia sekta ya mafuta, tunatumia lita karibu bilioni 3.14 kwa mwaka, na kwa petrol Serikali inakusanya shilingi 792, diesel shilingi 668 kwa kila lita na mafuta ya taa shilingi 615. Mafanikio ya umeme tumepata mafanikio mazuri makubwa sana katika kusambaza umeme yametokana na sekta ya mafuta.

Mheshimiwa Spika, unakumbuka ukiwa umekaa kiti hicho ukiwa Naibu Spika na mimi nikiwa mjumbe wa kamati nikiwa pale nimeshika microphone tuliweza kutenga pesa zilizoweza kusababisha REA isambaze umeme kiasi hiki. Lakini hata kasi hii tunayoiyona ya RUWASA kusambaza maji kama anavyosema Waziri wa Maji kwamba unapomuona Kobe juu ya mti ujue amepandishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sekta ya maji imepandishwa na sekta ya mafuta kwa sababu ile pesa ring fenced ya mafuta ndio inasababisha kasi hii tunayoiona. Hata sekta nyingine iwe reli, iwe nini wana pesa wanapata kutokana na mafuta. Mheshimiwa imebidi niyaseme hayo ninapokumbuka miaka 37 ya utumishi katika sekta ya mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie bomba la mafuta niwapongeze marais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Jeneral Kaguta Museveni wa Uganda kwa kufanikisha mchakato wa bomba la mafuta kufika hapa.

Mheshimiwa Spika, kwangu katika bomba la mafuta la zaidi la mno ni kwamba kuwa na mkuza wa bomba la mafuta unasaidia kuamasisha utafutaji wa mafuta kitaalam sisi tunayo mafuta katika bonde la kutoka Albert kushuka mpaka Tanganyika na Rukwa Eyasi Wembele kuja mpaka kwetu huku. Lakini zile wanaziita stranded reserve lakini zile wanaziita stranded reserve yani ni reserve ziko uwezi kuzifikia kwa sababu hakuna miundo kuwepo kwa bomba ili kutatusaidia, ndio faida kubwa ninayoiona ninachoomba kazi kubwa iendelee.

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa wakati napongeza hiyo nipende kuiomba Serikali na hii naiomba Serikali kwa ujumla wake sio Waziri Tanzania tumekuwa na mapungufu katika kutafuta mafuta kumbukumbu zangu haziko sawa sikumbuki kama kutoka mwaka 2011 kuna leseni ilitolewa ya kutafuta mafuta.

Mheshimiwa Spika, huwezi kupata mafuta bila kutafuta lazima kutafuta na kutafuta kuna gharama nimesoma taarifa ya Kamati nimesoma hii hotuba ya Mheshimiwa Waziri atujafanya lolote hizi pesa zilizotengwa katika kutafuta Eyasi, Embele sijui Mnazibay si chochote si lolote kucholonga kisima unahitaji bilioni 100 hizi pesa zilizotengwa si lolote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kazi ya TPDC kubwa ilikuwa kuhamashisha promotion, u-promote kusudi wadau waje wachimbe ukitaka uchimbe wewe kama Taifa utamaliza miaka minne miaka 100 sisi tunataka kuishi leo tuchimbe mafuta leo tuweze kuyapata.

Mheshimiwa Spika, inasikitisha hatujatafuta mafuta kwa zaidi ya miaka 10 hukuna kilichofanyika, hata hii mafanikio ya Embele nimesoma kwenye taarifa Embele hakuna kitu kimefanyika. Tuamue kama Taifa na ninajua utata ulipo nani atachimba atapata nini ni kanuni ya dunia uwezi kuibadilisha ama uende PSA au uwe na pesa umtafute mkandarasi au utumie concession kama unadhani utaliwa wewe tafuta pesa zako utumie contract uchimbe yakikosa inakula kwako.

Mheshimiwa Spika, kisima kimoja bilioni 100 vichimbe 10 vikose tirioni 1 utawaaambia nini watu hapa kwa hiyo ama utumie PSA kama anavyosema mzee mmoja ukitaka kula na wewe uliwe kidogo PSA mgawane mwende mbele. Au uende kwenye concession kusudi mwende ule mlabaa haina ujanja lakini bottom tunataka mafuta leo tuchimbe na huwezi kupata bila kuchimba. Nimeangalia Uganda kutoka mwaka 2002 mpaka sasa wamechimba visima 100 hivi vya Eliyasi, Embele vitatu tena vifupi hatutafika popote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bomba la kwenda Uganda litapeleka gesi ya kupikia au natural gas Uganda. Na kuna agenda ya kupeleka gesi Kenya, ni muhafidhina katika hilo, na niliwahi kuwa katika kiti cha maamuzi nikiwa Gasco; nilikuwa nakataa gesi kwenda Kenya. Tutapeleka gesi Kenya atatengeneza mbolea tatuuzia mbolea. Yanakuwa yale yale ya parachichi, yanakuwa yaleyale ya mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuchimbe gesi Mtwara, kina kifupi; tuchimbe Lindi; tuchimbe nyumbani Mkuranga, kuna gesi, tutengeneze kiwanda cha mbolea. Kiwanda cha mbolea kina makandokando; haiwezekani tukatafuta makandokando kuyaondoa kwa miaka yote. Tukubaliane leo kiwanda cha mbolea kianze kwa sababu tunahitaji mbolea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie usalama wa mafuta, na amelizungumza mwenzangu, Mheshimiwa Mansoor, na wewe ulilizungumza wakati tunahitimisha ile bajeti ya Mazingira. Tatizo liko wapi?

Mheshimiwa Spika, tunayo sekta ya bodaboda, na wale wanahitaji mafuta kwa sababu mafuta ni upatikanaji wake, waipoyapata watayatafuta vyovyote. Namna ya kufanya – na kweli EWURA mjiangalie – zamani tulikuwa na vituo vya aina tatu; fuel service station, fuel station na cab site. Wale wakongwe wenye faida ya umri kama mimi, ulikuwa ukienda kununua mafuta utayaona yanapanda kwenye chupa wanasonga hivi halafu yanakwisha.

Mheshimiwa Spika, tuanzishe vituo hivyo vidogo ambavyo vinaweza kuwa vijijini, vijana wanatunza lita 100, 200, 300 salama. Yataangalia ubora wa mafuta, usalama wa mafuta na uwezo wa kupatikana kwa karibu walipo watu. Hatuwezi kuepuka biashara ya bodaboda, tunazihita pikipiki leo kuliko siku nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, EWURA – na mnaweza kuja, nitawaelekeza bure – lazima muende kwenye cab site muweze kupunguza gharama ndiyo tutaweza kusambaza vituo mpaka vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie uagizaji wa mafuta. Nimesoma taarifa; yako maendeleo yameonekana. Lakini katika mafuta ninachotafuta ni nafasi ya mafuta kuchangamsha uchumi wa nchi hii. Sisi location advantage ya Tanzania ambayo nasema location advantage siyo faida, faida ni kutumia hiyo location advantage.

Mheshimiwa Spika, sisi tuko kwenye nafasi nzuri ya kuweza kuwauzia wenzetu. Pamoja na taarifa ya Waziri kwamba tumepunguza premium kwenda wastani wa 36 lakini tujipime na Kenya; Tanzania tunaposema premium ya 22, 25, 58, Kenya wanasema 4, 5, 6. Kwa nini premium Kenya zinakuwa nafuu premium Tanzania zinakuja juu?

Mheshimiwa Spika, lakini jiulize; kwa nini unapowaita watu walete bid kuja ku-supply mafuta wanakuja wawili kila siku? Ukimuita ni yuleyule, Magesa na Mwijage, kila siku haohao; kwa nini hawaji kumi? Lazima tujipime tuangalie katika mfumo mzima, kuna nini hapa? Ndiyo maana tunapata mafuta yenye gharama kubwa kiasi kwamba hatuwezi kupata competitive advantage. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)