Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Shanif Mansoor Jamal

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. SHANIF M. JAMAL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kwanza ya kipekee ya upendeleo niweze kuchangia hoja ambayo ipo mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, naomba nichukuwe nafasi hii pia ku-declare interest mimi ni mdau kwenye biashara ya mafuta na mdau mkubwa kwa Wizara ya Nishati. Naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri sana ambayo ameitoa leo hapa pia naomba nichukuwe nafasi hii kuunga mkono hotuba yake mia kwa mia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mie nitachangia maeneo machache la kwanza ningeomba kuchangia kwenye sehemu ya REA III. Mpango wa kuusambaza umeme vijijini, kwenye Jimbo la Kwimba umeanza miaka mingi 2013 REA round III, ilianza kuna vijiji tulikuwa tumekubaliana tulipewa orodha kwamba vitapata umeme kwenye miaka miwili ya 2019 na 2020.

Mheshimiwa Spika, mpango wa REA III kwenye Jimbo la Kwimba unasuasua sana kuna maeneo mkandarasi anasuasua sana wameweka nguzo lakini waya bado hajasambaza umeme kwa kweli unaenda kwa suasua sana kwa wananchi, pia kuwaunganisha wananchi pia imekuwa ni changamoto kwa sababu ukienda kwenye REA unaambiwa elfu 27 wananchi wakienda kwenye Ofisi ya TANESCO waambiwa 177,000 kwa kweli ni mkanganyiko mkubwa sana.

Mheshimiwa Spika, ningeomba Mheshimiwa Waziri aliweke wazi kwamba Jimbo la Kwimba ni jimbo ambali lina vijiji 59 ina mitaa 14 lakini ni sehemu ambayo kama kijiji kwa hiyo inatakiwa iwe ni bei ya 27,000 lakini kuna maeneo wananchi wanatozwa 177,000 wanashindwa kulipa na pia kuunganisha wananachi wengi sana wameshalipia lakini kuunganisha umeme pia ni shida sana.

Mheshimiwa Spika, ningeshauri pia kwamba TANESCO kila mradi ukisoma kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri amewapa TANESCO watafanya, lakini TANESCO naona kama uwezo wao utakuwa umekuwa ni mdogo sana kwa sababu kila mradi TANESCO unatekeleza. Ningeshauri pia maeneo mengine tuweke wakandarasi waweze kusaidiana na TANESCO tukiwapa TANESCO kazi zote hizi za kuunganisha wananchi nyumbani kwao itakuwa ni shida sana ningeshauri pia wakandarasi wengine waweze kuunganisha wananchi wapate umeme kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, TANESCO nafikiri out-stress hawana watumishi wa kutosha wapo lakini hawatoshi kwa sababu kazi ni kubwa tunataka tufike vijiji vyote vipate umeme awamu hii sasa maana yake lazima tufanye kazi ya ziada.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la REA ningeomba hilo walifanyie kazi lakini pia maeneo mengi wanaweka nguzo za miti lakini kwetu kwenye Jimbo la Kwimba kuna maeneo wakati mvua ikinyesha maji yanapita nguzo zinaanguka wanarudia kazi ya marudio imekuwa nyingi sana. Ningeshauri kwamba kuna maeneo wanaona ni korofi waweke nguzo za zege kwa nini wanarudia kwa hiyo watu wanapenda kufanya kazi ya marudio maana yake labda inalipa posho kwa hiyo watu wacha turudie lakini wananchi pia wanapata shida. Umeme unakatika mara kwa mara kwa sababu ya nguzo zimeanguka mimi ningeshauri maeneo korofi mengine waweke nguzo za zege angalau kazi isiwe ya kurudia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu nyingine ningependa kuisemea ni sehemu ya EWURA nimeshasema kwamba ni mdau kwenye sheria ya EWURA ningeomba kama ungeweza kukubali ungeagiza Serikali walete sheria EWURA ifunguliwe upya hapa Bungeni tuanze kuiangalia upya kwa sababu sheria EWURA tuliunga miaka 20 iliyopita. Sasa hivi sheria EWURA imekuwa ni sheria kandamizi kwa vituo vya mafuta, imekuwa kandamizi kwenye kuendeleza sekta ya mafuta kwa sababu faini zao zimekuwa ni kubwa sana kwenye vituo ambavyo kwa kweli vituo vinashindwa kulipa vinakula mtaji. Tunataka vituo viende mpaka vijijini lakini masharti na kanuni za EWURA hazitafanya mtu apeleke kituo kwenye Kijiji kwa sababu gharama zao ni kubwa sana kwanza kupata kibali ni gharama mazingira ukienda vibali ni vingi sana ningeomba suala hili la EWURA tuliangalie kwa upya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza EWURA wamekamata maji, nishati, mafuta nao wamezidiwa, ningeshauri hii sheria iangaliwe upya labda tuwe na taasisi inasimamia maji peke yake, kuna taasisi inasimamia nishati peke yake, kuna taasisi inasimamia mafuta peke yake. Kwa hiyo, sasa hivi ukiangalia Bodi wa EWURA pia inateuliwa na Waziri wa Maji lakini huku Waziri wa Nishati nae anatakiwa afanye kazi na wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, inakuwa ni ngumu sana ningeshauri EWURA tungeweza kuifumua upya tena sheria yake tukawa na taasisi tofauti tofauti. Mfano nilikwambia juzi EWURA wametangaza kwamba gari ya abiria ikiingia kwenye kituo utatozwa faini milioni 7 kwenye kituo, sasa mwenye kituo una makosa gani kama basi imeingia na abiria anataka mafuta unatozwa wewe milioni 7. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, milioni saba ni pesa nyingi sana kwenye kituo, labda uuze lita laki moja ndio upate milioni 7 hiyo, maana yake hizi faini wanazitoa wapi sijui ningeomba tuliangalie hili kwa undani sana kwamba hizi faini zimekuwa ni kubwa sana mfano ukikutwa na kosa na EWURA unatozwa faini ya milioni tano kosa la pili milioni 10 kosa la tatu milioni 20 kosa ya nne unafungiwa sasa hizo pesa ni nyingi sana ningeomba suala hili la EWURA tuliangalie upya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, uliagize waambie wakuletee faini wanazozitoza EWURA utashanga kituo huwezi kuendesha hii sekta ya mafuta kutoa huduma vijijini inataka iwe tuboreshe huduma ya mafuta ipatikane mpaka vijijini haitafika huko kwa sababu masharti haya hatutafikisha huko tuisaidie Serikali tuangalie utaratibu mpya wa kupata vibali vya kujenga pia vibali vya kujenga vijijini pia vina masharti kibao unawaambia milioni 2 ulipie mazingira pia umpe usafiri wa kufika kwenye eneo husika kwelli vibali ni vingi sana hatupata maendeleo kwenye sekta hii, ningeshauri hilo kwamba EWURA tuliangalie upya ili tuweze kufanikisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya tatu ningependa kuchangia ni sehemu ya vina saba nawashukuru sana Serikali wamefanya maamuzi mazuri kwamba TBS wasimamie vina saba waweke TBS, lakini sheria ya TBS ni kusimamia ubora wa mafuta kwenye sheria yao hawana sheria ya kusema pia vina saba ni sehemu ya kazi yao. Kwa hiyo, muhimu sana tuangalie hiyo sheria ya TBS kama inawaruhusu kufanya hiyo kazi.

Mheshimiwa Spika, pia suala lingine pia tumelisema sana kwamba GFI alikuwa ni mkandarasi wa nje alipata gharama kubwa lakini lazima tujuwe GFI alikuwa ni mwekezaji ni kampuni ya kitanzania, GFI ni Tanzania Limited ni kampuni ambayo inalipa kodi ndani ya nchi yetu. Lazima tulijue hili kwa sababu hawa ni wawekezaji sisi tunataka Mheshimiwa Rais amesema anataka wawekezaji waje ndani ya nchi basi tuwe na utaratibu wa kuwatoa kwenye mikataba kwa sababu tunataka wawekezaji waje watulipe kodi GFI atalipa kodi kila mwezi analipa VAT analipa kodi ya mapato, TBS hizo atalipa.

Mheshimiwa Spika, tumeamua tunaenda huko lakini ninachosema tuwe na process ya kuachana na mtu kwa utaratibu hilo ndio nimeona niliseme mimi kuhusu vina saba napongeza Serikali kwa maamuzi kwamba TBS wafanye lakini pia utaratibu mwingine ni kwamba TBS sasa hivi wananunua vina saba, kwa walewale wazungu wako na ubia na GFI. Kwa hiyo, lazima wajibadilishe pia. Watafute tenda watangaze wanunue kwa utaratibu wa Serikali sasa hivi inanunuliwa bila kufuata utaratibu kwa hivi ni muhimu ningeshauri Serikali wafanye utaratibu TBS wanunue kwa utaratibu wa PPRA wafuate sheria zote za nchi ili tupate unafuu, unafuu wa vina saba tunapoelekea kwamba tu-save pesa kwenye gharama za vina saba ili tupate pesa kwenye TARURA basi tufike pale kwenye lengo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nakushuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia ahsante sana. (Makofi)