Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nashukuru sana kupata fursa ya kuchangia kwenye Wizara hii ambayo inamajukumu makubwa sana hususani katika kipindi hiki.

Nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuwapata watu makini wanadiplomasia makini kuongoza Wizara hii. Namfahamu sana Mheshimiwa Mama yetu mpendwa Balozi Mulamula, kazi aliyofanya kujenga diaspora pale Washington na Marekani kwa ujumla na ninaamini sasa tutaona tofauti kubwa kwenye suala hili la diaspora kwa sababu ni mtu anayelifahamu, anafahamu uwezo wa diaspora kuchangia kwenye maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ninaamini kwamba suala linalozungumzwa la dual passport (passport pacha) litashughulikiwa, lakini pia tukijua kwamba hawa watu hawawezi kuja kuwekeza kwenye nchi ambayo siyo raia, hata kuweka akiba tu wakitaka kufungua account kwenye mabenki yetu inakuwa shida. Kwa sababu wanaambiwa onesheni passport ya Tanzania, kwa hiyo, inakuwa kwamba akiba nyingi ambazo tunaweza tukazileta remittances kutoka nje huko, kutoka kwa diaspora, ambako kwa nchi nyingine zinachangia sehemu kubwa ya pato la Taifa, mpaka asilimia tano kwa watu wa Ethiopia inachangiwa na watu wa diaspora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa kwetu hata ukisema unahesabu haifikii hata 0.1 percent of GDP. Kwa hiyo, ina maana tunapoteza uwezo, lakini pia tunapoteza nguvu kazi ambayo ina uzoefu tofauti na wana-skill tofauti, ambayo wakija hapa wakiwa na uhuru wa kuja na kuondoka wataiacha hapa nchini. Kwa hiyo, nataka kusema kwamba mimi ninamuamini sana kwamba sasa kwenye Wizara hii tumepata watu Mheshimiwa Mbarouk na Mama Mulamula naamini hawa watatufanyia kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwenye suala zima la diplomasia ya kiuchumi ambalo limezungumzwa na wengi. Mimi ningesema hivi, hauwezi kuwa na Balozi ambazo hazina wafanyakazi wa kutosha, tunataka Balozi ziwe na wanamasoko, zamani ilikuwa ni trade attachees, wanakaa kwenye Balozi kazi yao ni kuzunguka na kuangalia ni nani anawekeza, nani mwenye interest, nani anauza nini kwenye masoko yale na kuunganisha watu wetu na wale watu kule pamoja na wawekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi nataka niombe kwamba tusiseme tu kwamba tunapeleka mabalozi wazuri tupeleke pia wafanyakazi wa kutosha kwenye Balozi hizi na tusifungue tu Balozi nchi kama China jamani unakuwa na Balozi moja kwa nini usifungue consul nyingi miji mingi kule Thailand, miji hata mitano tukawa na consulars. Tukiwa na hizo ofisi ndogo ndogo za Balozi, zitakuwa na watu ambao sasa sio tu wanadiplomasia, sasa hivi tutawapeleka watu ambao watasaidia kwenye mambo ya masoko, kwa sababu masoko yako Guangzhou yako na sehemu nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwamba nimeona mmefungua Ofisi ndogo kule Mumbai, tufanye zaidi China jamani ni Taifa la kimkakati, lakini yako mataifa mengine kama Marekani, Uingereza pengine Ujerumani na wapi pia ni ya kimkakati basi tufanye mbinu ya kuongeza presence yetu kwenye hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kingine ambacho ningeomba kuzungumzia ni issue ya ushirikishwaji wa wafanyabiashara kwenye safari za viongozi wetu. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwamba alivyoenda Kenya juzi hapo alianza kutuonesha mfano mzuri kwamba anachukua watu waliochujwa, wafanyabiashara waliochunjwa kutoka TPSF pamoja na may be CTI pamoja na Mawaziri. Lakini ukweli ni kwamba, wakienda wenyewe hawa wafanyabiashara wanakuwa wanajua na watakuwa wamelenga na wanaunganishwa na watu ambao wataleta uwekezaji haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kila mtu atataka mbia, wewe ukiwa hapa ndani ukitaka kuanzisha biashara kubwa ni lazima uwe na wabia kutoka sehemu hizo na mimi ninaamini hili linakuwa na tija na ninaomba kwamba liendelezwe sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ni kwamba tumeona pia kwamba mmejaribu na ninawapongeza sana Wizara, kusema ukweli nawapongeza Wizara kwa sababu wamejaribu kuunganisha wajasiriamali kwenye maonesho ya viwanda nimeona kuhusu China na NMB wameweza ku-sponsor, wameweza kutoa ufadhili kwenye jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nafikiri hili ni jambo la kuomba sana kwamba liendelezwe, lakini na mabenki mengine au na wafadhili wengine hata wabia wenyewe watu wa maendeleo tuwaombe waweze kuchukua vijana wetu kwenda kuona, kwa sababu kuona ndiyo kuelewa na ndiyo kuamini. Kule China viwanda vidogo vidogo vimejaa na bei zake ni bei chee kabisa, unaweza kununua kiwanda kidogo cha shilingi hata laki tano ukaja nacho hapa ukachakata vitu, ukatengeneza fedha, ukawa tajiri, tena tuna umeme. Kwa hiyo naamini kwamba, tukiwapeleka wale vijana kule wakiona hata wale wanaofanya kama mashamba wataunda vitu ambavyo ni demonstration tukiwapeleka wale wachache, lakini watakuja kuwaonesha wenzao kwamba ni possible kufanya vitu vikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kingine ni ujenzi wa maofisi ya Balozi ambapo ni vizuri tujenge, nimeona kwamba wanamkakati wa kujenga hizo ofisi, nilikuwa nasema kwanini tusitumie mortgage financing kule? Bei ya mkopo kule Marekani au Uingireza nchi nyingi bei ya mkopo riba ni asilimia mbili na hususan ya mortgage. Tunaweza tukachukua mortgage zile na kwa sababu hatuna mtaji wa kutosha wakati huu kwa sababu tunawekeza kwenye miradi ya kimkakati basi tunaomba mkopo kwenye benki ya kule, tunachukua mortgage ile fedha tunaipeleka Balozi kwa pango ikatumika kama ni fedha ya kulipa mortgage na baada ya miaka siyo zaidi ya 10, 20 mnakuwa mmeshalipa mortgage, nyumba ni yenu na hamjatoa fedha yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna wakati mimi nafurahi kwamba NSSF walitaka kufanya vile, lakini ilikuwa pia siyo nadharia nzuri, kule mortgage ni kitu straight forward. Kwa hiyo, tunaweza tukafanya, tukakopa kwenye benki kule balozi ikajengwa wakakaa lakini wanajipa ile mortgage kwa fedha ya pango. Hata wafanyakizi wa balozi wanaweza wakafanya vile. Naomba sana hilo lizingitiwe kwa sababu naamini litaweza kuleta tija. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, ninataka niseme kwamba, nimefurahishwa sana na nilivyosoma kwamba kwenye taarifa ya utekelezaji ya mwaka uliopita, wameweza kufanya vitu vingi, miradi mingi ambayo wemeweza kuhamasisha kutoka kule na nikasema kwamba kweli Wizara hii imechangia vizuri na ninawapongeza kwa sababu huu ulikuwa ni mwaka mgumu sana ni mwaka wa ku-survive, lakini bado tunaweza kupata miradi, tunaweza kupata ufadhili wa kutosha kutoka kwenye nchi mbalimbali na tunaweza kupata wawekezaji.

Mimi nawapongezeni na ninaamini kwamba kweli tukitia nguvu kwenye Wizara hii basi uchumi wa kati wa kipato cha juu unaweza ukafikika kwa kipindi ambacho tunataraji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)