Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi hii, awali ya yote nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Dada yetu Balozi Liberata Mulamula, Naibu Waziri, Balozi Mbarouk Nassor pamoja na wajina wangu, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine na timu nzima ya Wizara kwa kazi nzuri ambayo kwa muda mfupi toka wameaminiwa wameifanya na tumeiona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pongezi hizi lazima zitanguliwe na pongezi na shukrani kubwa kwa Mheshimiwa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo wameonesha uwezo mkubwa sana na nia ya kushungulikia masuala ya kidiplomasia na kukuza diplomasia ya nchi yetu. Hata uteuzi wa mabalozi uliofanyika hivi karibuni ni ishara tosha kwa sababu uteuzi huu umefurahisha watu wengi kutokana na jinsi ambavyo umefanyika kwa umakini na kwa wigo mpana wa kuwagusa watu wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu kwa miaka mingi imekuwa na sauti kubwa sana kwenye mambo ya kimataifa hasa upande huu wa Kusini mwa Afrika kutokana na mambo mawili; kwanza, historia yetu na pili msimamo wetu ambao tumekuwa nao katika mambo yanayohusiana na haki na mambo mengine ya kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ni waasisi wa SADC ambayo ilianzia kwenye Umoja wa Nchi Tano za Mstari wa Mbele, sisi ni waasisi wa African Union ulioanzia kwenye OAU pamoja na East Africa na hata katika masuala ya Pan Africanism umajumui Afrika nchi yetu ilikuwa mstari wa mbele na tumeaminika na kuheshimika kwa hilo. Tunaiomba Wizara iendelee kuratibu ushiriki wetu katika jumuiya hizi ili sauti yetu iendelee kuwa pale pale na sasa hivi tuna nguvu kubwa zaidi kwa sababu tuko katika uchumi wa kati, kundi ambalo najumuisha karibu asilimia 75 ya population ya dunia tunapokuwa pale na sauti yetu tunakuwa na nguvu zaidi kuliko hata ambayo tulikuwa nayo mwanzoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi na uteuzi mzuri wa mabalozi ambao unafanyika ingawa bado hawajapelekwa kwenye nchi mbalimbali, lakini tuendelee tu kusisitiza vigezo na masharti kwamba mabalozi wetu wanakokwenda huko ni muhimu wakazingatia kwamba either huko waliko watuletee wawekezaji au watuletee masoko au fursa za elimu au ajira zote za chini na za kibigwa pia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu si kila balozi ataleta wawekezaji kwa sababu pengine nchi halioko haina wawekezaji wengi ambao tunawahitaji, lakini kutakuwa na masoko, kutakuwa kuna ajira au kutakuwa na fursa za elimu nina amini kabisa nchi yetu haiwezi ikafungua ubalozi mahali ambapo hakuna fursa, tunachohitaji ni kwamba mabalozi wetu watutangulie katika kuhakikisha kwamba fursa hizo tunazipata. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tusiwe watu tunasisitiza tu kwamba tutowe permit haraka haraka kwa watu wafanye kazi kwetu, lakini je, sisi kwenda kufanya kazi kwenye maeneo mengine. Uniruhusu nitaje tu kwamba mimi binafsi nafurahishwa sana na utendaji wa balozi wetu alioko China, tunaona jinsi ambavyo anashughulika na matokeo tunayaona, naamini kabisa mfumo huo ukienda namna hiyo tutaendelea kufaidi Zaidi katika diplomasia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu ni mfupi ninzungumze moja tu la mwisho juu ya Chuo chetu cha Diplomasia. Tunafahamu kwamba chuo kile kilikuwa hakidahili sana wanafunzi kutoka nje kilikuwa ni zaidi ya kukuza uwezo wa ndani, lakini hivi karibuni kimekuwa kikidahili wanafunzi wengi hata vijana wanaotoka Jimbo langu la Mwanga wengi wanasoma pale na wengine wameshasoma pale tayari. Kwa hiyo, ipo haya ya kukiongezea nguvu ya miundombinu pamoja na walimu na rasilimali zingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo Lingine ambalo linasumbua kidogo kwenye chuo kile ni kwamba vijana wanapokwenda field kuna tatizo kubwa sana ya kupata nafasi sehemu ambazo ni relevant.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu taratibu za ki-protocol ambazo zinafanya vijana hawa wasipokelewe kwenye balozi kufanya field, lakini mimi ningeshauri Wizara au Serikali i-negotiate na hizi balozi ili vijana wetu waweze kwenda kufanya field katika hizi balozi ili waweze kupata hasa uzoefu wa kile ambacho wanakisomea, si lazima tuanze na balozi zote tunaweza tukaanza na balozi chache kama za East Africa Community au za SADC ili vijana wetu wanaposoma waweze kutoka vizuri zaidi kwa kufanya mazoe katika mambo ambayo wanayasomea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naunga mkono sana hoja ya Wizara hii na nasisitiza kama walivyosema wenzangu kwamba Serikali itoe fedha kama ambavyo zimeombwa na zitakavyopitishwa kwenye bajeti ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yake, ahsante sana na naunga mkono hoja (Makofi)