Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi na mimi niopate kuchangia katika Wizara ya Mambo ya Nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitaanza kuzungumzia suala la ajira; wako wafanyakazi wengi ambao wanatoka nje ya nchi na wanakuja kuajiriwa katika nchi yetu ya Tanzania, lakini pamoja na kwamba wanaajiriwa, wanaajiriwa kwa kigezo cha kwamba ni wataalam, lakini pamoja na kuajriwa wamekuwa wakilipwa fedha nyingi sana ambazo fedha hizo wakati mwingine wamelipwa fedha dola za Kimarekani.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo lakini bado katika nchi yetu tumekuwa na wataalamu ambao wakati mwingine wanazidi vigezo vya hao wageni ambao wamekuja kupata ajira katika nchi yetu, lakini wafanyakazi hao wengi wamekuja kwa namna ya kupitia makampuni mbalimbali ambayo yamekuwa yakipata tender katika nchi yetu, hususan katika masuala ya barabara, uchimbaji wa madini, katika masuala ya minara, na kadhalika. Wamekuwa wakipata tender hizo kupitia hao wataalam ambao wamekuwa wakija kupitia hizo kampuni ambazo zimekuwa zikija kupata tender katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo yote kumekuwa na changamoto kubwa na kumekuwa na utofauti mkubwa wa Watanzania wanapokwenda kuomba ajira ama kupata fursa nje ya nchi. Watanzania wengi wanapokuwa wakienda kupata fursa nje ya nchi za kupata ajira wamekuwa wakiambulia kupata mambo yasiyoridhisha kama vile kufanya usafi, kulinda, kufanya kazi za ndani, changamoto nyingi pia wamekuwa wakikumbana nazo ikiwa ni pamoja na kuteswa na kudhalilishwa wakati mwingine utu wao kwa sababu tu ni Watanzania.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hiyo changamoto, naomba niiombe Serikali, ni wakati muafaka sasa Serikali kupitia balozi zetu kwenye nchi mbalimbali duniani kuhakikisha wanafanya njia mbalimbali kuhakikisha Watanzania wetu wanapata fursa stahiki wanapokuwa wamekwenda kuomba kazi huko nje ya nchi. Kinyume na hapo balozi zetu zisipofanya hivyo zitakuwa hazijatutendea haki kwa sababu sisi sote tunashuhudia namna ambavyo Watanzania wamekuwa wakati mwingine wakipitia mazingira magumu sana wanapokuwa huko nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, tuombe Serikali sasa itumie fursa hii kupitia mabalozi wetu walioko nje ya nchi kuhakikisha wanazitafuta fursa maana yake pia ni sehemu ya wajibu wao, watafute fursa za ajira kwa ajili ya Watanzania wetu kwa sababu tumeona wakati mwingine hao wageni wanapokuja kupata ajira katika nchi zetu wamekuwa wakipewa ushirikiano wa kutosha na Serikali zao huko nje, jambo ambalo limesababisha wamefanya kazi kwa ufasaha na wamefanya kazi kwa kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kisawasawa. Ni wakati sasa na sisi tuombe balozi zetu zitusaidie huko nje kuhakikisha zinatafuta fursa stahiki kwa Watanzania ili waweze kupata ajira za kutosha huko nje na mwisho wa siku pia warudi kufanya maendeleo katika nchi yao.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo yote naomba nizungumzie suala la uwajibikaji wa mabalozi wanapokuwa huko nje. Ni wazi kabisa kwamba uwajibikaji wa mabalozi haujawa wazi. Uwajibikaji wa mabalozi wetu huko nje haujawa zai kabisa na tuseme wazi ili kuhakikisha kuwa mabalozi wetu wanakwenda kusimamia na kukuza diplomasia ya uchumi tunatakiwa tuweke mikakati, lakini pia tunatakiwa tufanye mabadiliko ya mfumo wa uwajibikaji wao, lakini mwisho wa siku mabalozi hawa waweze kuwajibika kwa hili Bunge. Wakiwajibika kwa hili Bunge ninaamini watafanya kazi kiufasaha na uwajibikaji wao utakuwa wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia tunahitaji hawa mabalozi wawe wanawasilisha mpango wao wa kazi kila mwaka. Wawasilishe mpango wao wa kazi kila mwaka katika Bunge hili kupitia Kamati ya Mambo ya Nje, wakifanya hivyo inaweza kusaidia wao kuwajibika ipasavyo wanapokuwa huko nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ninaamini kwamba ikiwa taarifa zao za uwajibikaji zitaletwa katika hili Bunge, pia Bunge tupewe nafasi ya kutoa mapendekezo kwa nafasi zao za teuzi. Tunapoona wamepwaya katika suala zima la uwajibikaji Bunge tuna uwezo wa kutoa mapendekezo ni nini wafanye. Ninaamini tukifanya hivyo tunaweza tukasaidia uwajibikaji wa mabalozi wetu wanapokuwa huko nje.

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Kuna Taarifa Mheshimiwa Stella Fiyao.

T A A R I F A

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba kumpa Taarifa Mheshimiwa Stella kwamba kwa mujibu wa utaratibu wa miongozo, taratibu, kanuni, sheria na miongozo mbalimbali zipo taratibu za kila makundi kuwa na sehemu ya uwajibikaji wake. Serikali itawajibika kwa utaratibu wake kwa maana ya watumishi wanajua jinsi ya kuwajibika, lakini vilevile tunayo Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Kamati hii imekuwa ikipata taarifa mbalimbali za uwajibikaji wa mabalozi, ikipata taarifa mbalimbali za masuala yote ambayo yanahusu Wizara ya Mambo ya Nje. Kwa hiyo, haipo na wala haitakuja kutokea Bunge kuja kuanza kuwahoji mabalozi kuhusu uwajibikaji wao. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Stella Fiyao unapewa hiyo Taarifa.

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwanza huo nilikuwa natoa ushauri wangu. Kwa ushauri una uwezo wa kupokelewa ama kutokupokelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaamini tukifanya hivyo hii itaondoa uzembe katika utendaji, pia itasababisha mabalozi kuwajibika ipasavyo katika majukumu yao wanapokuwa nje ya nchi na itaondoa dhana iliyojengeka muda mrefu kwamba cheo cha ubalozi ni cheo cha starehe.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)