Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, lakini ili kutimiza itifaki nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan. Kwa kweli Tanzania inang’ara, amefanya ziara katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki tunamshukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu viwanja na majengo mengi yamezungumzwa; mimi nitazungumza kidogo ili ku-avoid kurudia.

Mheshimiwa Spika, umefika Nairobi kwenye ule Ubalozi tuna kiwanja kile, muda mrefu sana. Sasa hivi majengo haya ambayo Waheshimiwa wengine wamezungumza, sio lazima tujenge kwa kutumia mtaji wa Serikali, tunaweza tukajenga kwa kutumia public private partnership, unaweza ukaingia mashirikiano na taasisi mbalimbali. Nachukulia mfano, labda CRDB Bank wanataka kufungua branch pale, kwa hiyo, CRDB Bank mnakubaliana public private partnershipn sisi uwekezaji wetu unakuwa ni ile ardhi. Kwa hiyo, ningeomba eneo hilo la majengo na viwanja tuweke kipaumbele sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tujitahidi kuendelea kuwapa viwanja Mabalozi hapa Dodoma sasa hivi ndio makao makuu, tutafurahi makao makuu tuanze kuona bendera za Mabalozi zinapepea. Ubalozi wa nchi hii uko hapa Dodoma, Ubalozi wa nchi hii na tukiwapa viwanja Balozi hizi, kimsingi huwa tunabadilishana, ile good gesture ambayo sisi tumewaonesha na wao hivyo hivyo wanatupa viwanja kule katika makao makuu ya nchi zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nipongeze sana Mheshimiwa Waziri hapa mtusaidie na Naibu tuna imani kubwa sana na ninyi. Hata zile Balozi ambazo hazina ofisi hapa Tanzania, ziko Balozi ambazo zina-serve Tanzania, lakini wameweka ofisi zao katika nchi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki na hapa mimi nakuja na swali. Tunatambua kwamba tunazo Balozi takribani 30 hazina ofisi Tanzania; tujiulize kwa nini? Balozi hizi ambazo wanakuja kufanya kazi na sisi wana-present credential hawana ofisi tuwashawishi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unakuta hizi Balozi nyingi zimekaa katika nchi fulani na zingine nchi fulani, sisi tujiulize tatizo ni nini hawaweki ofisi hapa? Tuwape incentive kama ni masuala ya VAT huwa wanadai tuwarudishie kwa wakati, mawasiliano, tuimarishe. Ubalozi mmoja ukiwepo hapa Tanzania wanatumia mafuta, wataajiri vijana wetu hadi wa kule Njombe, huko Ludewa wataajiriwa, kutakuwa kuna local best staff, wahudumu gardener, wale watu wa security, uchumi unaongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna baadhi ya nchi yaani wao uchumi wao unaongezeka kwa kuamua tu kuweka taasisi za Kimataifa, dola zinapita mishahara kwenye account, you see. Hizi Balozi 30 naomba tu-pay attention, hatujachelewa na Balozi zingine mpya ambazo zinaendelea kuweka mashirikiano na Tanzania, tuombe wanavyokuja kuomba kuanza Ubalozi na sisi tuombe waweke ofisi. Mzunguko wa fedha ukiwa na Ubalozi mmoja tu, matumizi ya Balozi moja kwa hizi nchi za nje zikiwa hapa kwetu, unakuta sio chini ya dola 60,000 kwa mwezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bado hapo mishahara inapita kwenye Mabenki kwa hiyo, uchumi huu utaongezeka. Kwa hiyo, niombe sana Madame Waziri tuna imani utusaidie Naibu Waziri, Katibu Mkuu wote hawa ni wataalam ma-guru wa foreign. Balozi hizi zije na watoke Tanzania kwenda nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa huduma, ku-serve au waende nchi za SADC kutokea Tanzania. Wanapoenda wanatumia ATC ni mfano tu, kwa hiyo, uchumi utabadilika

kwa kiasi kikubwa sana. Kwa hiyo, naendelea kuunga mkono hii hoja na hizi changamoto ndio naziweka mezani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la watumishi limezungumzwa; kuna baadhi ya Vituo hatuna Maafisa wa Uhamiaji na kuna kada zingine nyingi kwa kweli ambazo ni muhimu sana. Kada hizi za afisa wa uhamiaji pale unahitaji utoe Visa, tourist visa, unahitaji utoe business visa, unahitaji utoe multiple entry visa, sasa kada hizi wakati umefika tuone namna gani wataalam hawa wanaenda.

Katika hilo hilo eneo la visa, kuna visa inaitwa referred visa sasa hivi visa zinatolewa kwenye mtandao. Lakini hiyo referred visa mara nchi hiyo inapoomba kupata visa watu wake, lazima taarifa ziende makao makuu ya nchi na wafanyie upekuzi. Wakati mwingine suala hili mchakato wake unachukua muda mrefu, tuko kwenye uchumi shindani, tuangalie list yetu ya Referred Visa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unakuta sisi tumewekea nchi kadhaa referred visa, lakini ile nchi ambayo sisi tumeiwekea referred visa yamkini yenyewe haijaweka referred visa kwa Tanzania. Kwa hiyo, naomba tu-review list ya nchi ambazo tunazitambua kama nchi za referred visa. Leo hii mtalii anakuja anasema, nataka kuja Tanzania tunasema nchi yako iko kwenye referred visa, subiri wiki tatu, ataangalia Mlima Kilimanjaro kutokea nchi jirani, ataenda nchi jirani atasema beach ya Zanzibar inafanana na beach fulani ya nchi jirani, ata-opt kwa sababu ile nchi jirani inampa Visa on arrival, lakini sisi tunamuambia you know Sir referred visa you have to wait two weeks. Anakuambia vacation yangu imeisha, my holidays are gone I can’t wait, ataenda nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, twende na reforms, Waziri mtusaidie tunaomba sana. Wenzetu nchi jirani wameshabadilika hamna ma-referred visa inategemeana. Huko nyuma wakati tunapigania uhuru na nini changamoto zilikuwepo, sasa hivi kuna mitandao watu wa usalama wanajua kujua kama huyu ni criminal ama vipi?

Mheshimiwa Spika, eneo lingine kwa haraka haraka diplomasia ya uchumi, Balozi zetu nawapongeza sana Mabalozi wote, wanafanya kazi kubwa nzuri sana, diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa tuendelee kuimarisha tunahitaji masoko ya mbao za kutoka Njombe, Mufindi. Mimi nashukuru sasa hivi mbao za Mufindi, Njombe tumejitahidi zinakwenda mpaka Somalia. Lakini ili jambo hili lifanikiwe mazao kama mahindi, viazi, korosho, pamba lazima tupeleke taarifa za kutosha katika Balozi zetu kiasi kwamba mwekezaji anapokwenda pale Ubalozini anapouliza kwamba una tani ngapi za pamba, una tani ngapi za korosho isiwe tena, ngoja kwanza niwasiliane na Wizara waniletee, inachukua muda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini taarifa hizi zikiwa kwenye website za Balozi zetu e-government yaani ni haraka sana wawekezaji watakuja, tutapata masoko na watatangaza fursa mbalimbali kwa hiyo nawapongeza sana Mabalozi wamekuwa wakifanya kazi kubwa na nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine, ambalo ni muhimu, tufungue Balozi mpya, tusiogope kufungua Balozi mpya. Hivi karibuni tumefungua Balozi Mpya takriban saba/nane ni pongezi nyingi lakini dunia ni kubwa we need to connect. tuendelee kufungua Balozi. Unaweza ukachagua nchi ukafungua Ubalozi pale unaamua kupelekea chai, unasema nchi fulani ni soko langu la uhakika la chai. Sasa hivi tunauza chai takriban dola 7 kwenye mnada wa Mombasa, lakini chai inaweza kutujengea Bandari ya Tanga.(Makofi)

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Sophia Mwakagenda nimekusikia.

T A A R I F A

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ninaomba nimpe Taarifa mzungumzaji anayezungumza sasa kwamba anachokisema ni sahihi, Guangzhou ni mji ambao ni mji wa kibiashara lakini pale hatuna Balozi mdogo ambaye angeweze kusaidia wafanyabiashara wetu wakienda wakasaidiwa kwa haraka. Ninamuunga mkono na ninampa taarifa hiyo. (Makofi)

SPIKA: Taarifa hiyo unaipokea Mheshimiwa Hazara.

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Spika, Taarifa hiyo naipokea na nimekumbuka kuweka msisitizo chini ya Balozi kuna Honorary Consul, you see kwa hiyo tunaweza tukaweka Consular Mkuu, pia tunaweza tukaweka enhee Honorary Consul, kwa hiyo haya yote yanawezekana utakuta nchi hatuna uwakilishi, hatuna Honorary Consul, hatuna Consular Mkuu, Consular General, we need to connect, huu ni wakati Mheshimiwa Waziri tusaidie, tusaidie, tuna Balozi chache sana tukilinganisha na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi za SADC. Wenzetu wanafunguka, wanafunguka wakati umefika vijana wetu hawa wakasome nje, wapate fursa mbalimbali za masomo, utaalam wa aina mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sijasikia kengele nadhani, naendelea, ahsante.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ni diaspora; diaspora Watanzania waliopo nje wanarudisha fedha nyingi sana nyumbani. Wanasaidia kuongeza uchumi, duniani kote diaspora wamekuwa ni tool muhimu sana. Kwa hiyo, diaspora wetu ambao wako nje ni pongeze sana Mabalozi wamekuwa wakiwasajili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)