Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

hon Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi niseme nikushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukizungumza suala la michezo ndani ya nchi yetu inawezekana tukazungumza kwa mapana na marefu sana kwa muda mrefu lakini bila kuelewa changamoto tulizokuwa nazo au kupata tija juu ya michezo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nataka nianze kwenye masuala ya mchezo wa mpira. Hatuwezi kuzungumza kwamba tunakwenda kucheza mpira bila kujiandaa, lakini mara nyingi nimekuwa nasilikiza hotuba za viongozi wetu wanatueleza kwamba Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu, lakini haya yote yanakuja kwa sababu hatuna maandalizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la viwanja hatuwezi kulibeza, inawezekana tukawa na academy nyingi za kutosha, lakini kama hatuna msingi wa kutengeneza viwanja vya kutosha, hizi academy zitakwenda kuchaza wapi mipira.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunavyo viwanja vya Chama cha Mapinduzi, viwanja hivi mimi nadhani nimeshiriki wakati niko Hai nilijenga kiwanja pale kikubwa cha mpira na nadhani kiwanja sasa hivi kiwanja kile kinatumika, lakini nilivyofika Iringa niliboresha kiwanja cha Iringa pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanja hivi vinahitaji kugharamiwa, lakini ukiangalia mapato yanayopatikana kwenye viwanja vile CCM nadhani inapata kwenye asilimia 20 ya mapato. Lakini tunapoingia sasa kuvikarabati viwanja vile mzigo unabaki kwa Chama cha Mapinduzi. Sasa angalizo langu tuna fedha sisi ambazo zinatoka FIFA kwa ajili ya kuboresha masuala yote ya mpira katika chama chetu cha mpira, lakini tujiangaliea na tuangalie kwamba je fedha hizi zinatumikaje kwenye suala la mpira? Lakini leo tuna vilabu timu nyingi zinakwenda kwenye awamu ya kwanza zikishapanda daraja, awamu ya pili timu zile zinatelemka daraja. Lakini timu hizi zinatelemka daraja kwa sababu tayari hatujafikia malengo ya kuzilea hizi timu kwa mfano mimi ninayo kule timu ya Ndanda, toka inacheza ligi kuu inatoka Mtwara timu ya Ndanda wanasafiri kuja Dar es Salaam lazima ungo utembee, lakini kuna wafadhili ambao wanaifadhili TFF, lakini ukiangalia kwenye kasma za fedha ambazo wanapewa kila klabu kwenda kuendeleza suala zima la mpira hawawezi ku-move kwenye suala zima la mpira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, angalizo langu leo Azam wametoa fedha nyingi sana, fedha hizi Mheshimiwa Waziri usipokuwa nazo karibu, hizi fedha zitaishia mikono ya watu, kama kuna fedha za FIFA zinakuja kwetu kwa ajili ya kuboresha mpira na fedha ni nyingi sana inayokuja Tanzania, lakini vilevile tumeshindwa kabisa hata kui-maintain timu yetu ya Taifa tutaweza haya mabilioni ya Shilingi yanayokuja, haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kweli nikuombe kwenye suala hili la mpira kwetu Tanzania kwanza tuangalie kwenye viongozi wa TFF, hawa wanaweza wakatuvusha? Lakini la pili kuangalia mfumo wenyewe wa mpira tunaocheza Tanzania, tunazungumza kuhusu wachezaji wa kigeni, hatuwezi kuwakwepa wachezaji wa kigeni, wachezaji wa kigeni lazima waje na lazima wacheze kwa sababu hatuja waandaa wachezaji wetu humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mchezaji wa Kitanzania akishaingia amecheza Simba, amecheza Yanga na jina lake tayari limeshakuwa kuwa kubwa siku kesho anakwenda kucheza mpira leo anatafutwa yuko baa, kwa namna moja au nyingine wachezaji wetu hili lazima tulizungumze bado hawajajitambua kama mpira ni ajira. Wachezaji wa wenzetu wa kigeni wanakuja kucheza mpira Tanzania kwa sababu wanaelewa mpira ni ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema Wizara ijielekeze sasa kwenye kuangalia mazingira yote ya mpira, ukiangalia pale Brazil kuna wachezaji wa zamani, lakini wale wachezaji wote wa zamani wanapomaliza muda wao wa kustaafu wanakuwa kuna chombo mahsusi ambacho kinawaweka kwa ajili ya kuwa makocha. Lakini leo ukiangalia Tanzania timu zote kubwa ukienda Namungo, Simba, Yanga na timu zingine zote kuna makocha ambao si wa zawa ni makocha wa nje, lakini timu za Brazil mnazoziona wanacheza mpira tunaziita samba wale kule kuna wazawa wenyewe ambao kuna chuo pale kinafundisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sisi niombe tujielekeze na sisi sasa kufundisha makocha tunaposema sasa tunataka tusome lazima tuwe na walimu, hatuwezi kuzungumza kwamba tunataka tusome wakati hatuna darasa, walimu tunasema tunakwenda kusoma kusomea mpira, ni kitu ambacho hakiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wengi wamezungumza kuhusu academy, academy hizi zina gharama kubwa sana katika bajeti hii ya Wizara niliyoiangalia sijaona sehemu ambayo Wizara inakwenda kujikita kwenda kuendesha haya madarasa ya chini ya watoto wetu ili waweze kupanda. Leo ukiangalia inawezekana tukamzungumzia Messi amekulia kwenye academy ya Barcelona na amekaa pale na wachezaji kadhaa, amelelewa, amefundishwa mpira toka akiwa na miaka mitano leo hii anaonekana mchezaji mkubwa duniani ambaye analipwa fedha nyingi duniani. Tunashindwa nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, hayo ni mambo ambayo Mheshimiwa Waziri anatakiwa afanye sasa maamuzi kwamba sasa tunaingia, tutengeneze academy na vijana wetu waweze kucheza mpira. Mimi nina imani sana kubwa mtoto ukimfundisha akiwa mdogo ni mwepesi sana kushika kile kile unachomfundisha, lakini sasa sisi bado hatujajajiwekeza huko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wamezungumza kuhusu BASATA; kama kuna chombo ambacho kinawezekana baadaye kikaenda kuua mziki wa kitanzania ni BASATA. Hili inawezekana Wabunge tukazungumza hapa na hatuzungumzi kwa mapana na marefu sana, lakini chombo hiki hakipo kwa ajili ya kuwa-accomadate wanamuziki, lakini chombo hiki kipo kimaslahi zaidi na matendo yao wanayoyafanya, yako ambao wanayafanya hata wanamuziki wenyewe, wasanii wenyewe wamekata tamaa na chombo hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kuwa na chombo yaani leo tunampishi anasema anampikia Mtenga ugali, lakini Mtenga anatoka anakotoka akienda kwenye sahani anasema ugali huu mimi siwezi kula, ni vitu ambavyo haziwezekani. (Makofi)

Kwa hiyo tuangalie Mheshimiwa Waziri afike mahali aiangalie hii BASATA, lakini arudi tena kwa upande wa TFF nenda pale ukaangalie viongozi wako wengine wana miaka 20 pale TFF hawa waliokuwa miaka 20 ndio leadership, wale wanapanga viongozi, wanajua mambo yakufanya, wanajua deal ziende wapi. lakini wanajua mpira wao wanataka kuuendesha kwa namna gani, hatuwezi kumove kwa viongozi wale ambao ni watendaji pale TFF hata siku moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tutakuwa tunajidanganya, hivyo leo kama tuna premier league tuna timu zaidi ya 12 au 14, lakini timu hizi kama tungekuwa tuna watu wenye uwezo wa kufikiri tungefika mahali tukasema bwana kila timu kwa mfano kwangu mimi kule tuna timu ya Ndanda pale tuna Dangote; TFF wangekwenda kuzungumza na kampuni ya Dangote, wakafanya makubaliano wakawa mdhamini namba moja, lakini kuna Breweries, sijui Kilimanjaro kuna kampuni gani; vilabu vyote tusifike mahala hapa tukamsifia Mheshimiwa Waziri Mkuu kesho inawezekana Waziri Mkuu inawezekana akasema jamani nguvu zimeniishia za kufanya hii kazi ya mpira nani anamsaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tutengeneza sasa impact ya kujua kwamba tunawatafuta wawekezaji na hili ni suala la kulibeba Serikali sio suala la vilabu hivyi, kwa sababu vilabu vinakotokea mpaka vinapanda madaraja haya wanakwenda hawa kwa kuchangishana fedha zao. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa muda wako umekwisha ahsante sana.

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)