Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kusimama salama hapa, na kuchangia Wizara ya Habari.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Katiba ya TFF kifungu 2.7 inaeleza TFF itashirikiana na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar kwa yale mambo ya kimataifa na ndio kipengele pekee ambacho kipo katika Katiba ya TFF, yenye page 64 lakini cha kushangaza kifungu hiki hakifanyi kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hakifanyi kazi kwa sababu kunako mwaka 2017 Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar lilijiunga na uanachama wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika CAF. Kwa muda mfupi Shirikisho la Miguu Zanzibar likaondolewa uanachama huo, lakini chakusikitisha na chakushangaza Chama cha Mpira wa Miguu - TFF hakikushiriki lolote juu ya kadhia hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili FIFA inatoa mgao kwa wanachama wake kila mwaka usiopungua dola milioni mbili, lakini miradi hiyo yote ipo Tanzania Bara tu kwa mfano Kigamboni Dar es Salaam na Tanga; Zanzibar hakuna mradi wowote.

Mheshimiwa Naibu Spika,…

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimwa Ravia kuna taarifa, Mheshimiwa jitambulishe.

T A A R I F A

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa naitwa Mheshimiwa Sima Hassan Sadiki, Mbunge wa Jimbo la Nungwi.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpa taarifa ndugu mchangiaji kwamba wakati wa uongozi wa Mheshimiwa Tenga alipokuwa Rais wa TFF Zanzibar iliwahi kunufaika na huo mradi ambao anazungumzia kwa kujengewa uwanja wa Gombani, Pemba kule kuwekewa nyasi bandia, lakini toka kipindi hicho si chini ya miaka minane hakuna mradi mwingine wowote wa kimaendeleo uliwahi kufanyika kwamba kwa kutumia fedha hizo. Ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana, Mheshimiwa Ravia unaipokea taarifa hiyo kutoka kwa Mheshimiwa Sadiki.

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea taarifa hiyo na niunge mkono hoja na huo uhalisia ulivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile Zanzibar haiwezi tena kuwa mwanachama wa CAF wala FIFA, kwa hiyo naomba niishauri Serikali mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, zikutane Wizara mbili za michezo kati ya Zanzibar na Tanzania Bara hili kulijadili mustakhabali mzima wa kadhia hii kwa wakati huu; pili, yafanyike marekebisho ya Katiba ya TFF na ndani ya Katiba ya TFF isomeke Zanzibar kitu ambacho kipo mstari mmoja; Makamu mmoja wa Rais TFF atoke Zanzibar; kuwe na Wajumbe wa Kamati Tendaji wa TFF ambao wanatoka Zanzibar; kuwe na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF watoke Zanzibar na isiwe kama sasa hivi Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar na Makamu ni mwalikwa tu wa Mkutano Mkuu, aende pale akasinzie tu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia turejeshe ligi ya Muungano ili tupate wawakilishi sahihi wa Tanzania na tupate kutengeneza timu ya Taifa ya Tanzania Bara yenye ushindani.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kama haya hayatekelezeki naomba Bunge lako Tukufu liridhie na liwaruhusu Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar wawaarifu FIFA kipengele cha 2.7 cha Katiba ya TFF hakitekelezeki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)