Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi hii uliyonipa na mimi ya kuchangia Wizara hii ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; kwanza kabisa naomba niipongeze Serikali kwa kazi nzuri wanayofanya katika Wizara hii kwa ajili ya kusaidia vijana wetu, lakini na Taifa kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijikite kwenye sanaa, najua wenzangu wamechangia michezo naomba niongelee Sanaa na Sanaa inavitu vingi kuna mziki, kuna movie na vingine. Naomba nijikite kwenye upande wa movie peke yake. Sanaa ni kazi, sanaa inasaidia vijana wetu wanapata ajira, sanaa inasaidia kuitangaza nchi yetu nchi mbalimbali, lakini sanaa hii itasaidia utalii na vitu vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takwimu zilizopo watoa huduma ambao ni wasanii wetu na walaji kidogo kunakuwa na kupishana au kidogo kunakuwa na walaji wanaona kwamba hawapati ile wanaohitaji kutoka kwa watoa huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kumekuwa na wimbi kubwa sana la watu hapa hapa Tanzania kuangalia movie za Kinaijeria, kuagalia movie kutoka kwenye channel tofauti tofauti netflix na zingine. Sasa huwa najiuliza kwa nini hatupendi vya kwetu? Kuna tatizo gani kwa nini tusiangalie movie za kwetu na tuangalie movie za watu wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikagundua tatizo lipo kwa upande wa Serikali pia, Serikali imejikita sana kwenye habari na michezo nadhani sanaa haiipi uzito mkubwa na ukiangalia ndiyo inayoajiri vijana wetu kwa asilimia kubwa, wanahangaika kutoka chini lakini mpaka watafika juu. Kwa hiyo, nilikuwa naomba nimepitia ripoti ya Waziri kwa kweli wamejitahidi sana pamoja na timu yake nzima kuainisha kwenye upande wa sanaa kwa mwaka wa fedha ujao watafanya nini, ameainisha ataanzisha tuzo za kitaifa, mikopo mbalimbali kwa wasanii, ameainisha mengi mazuri ambayo atawafanyia Sanaa ili iweze kukuwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata Kamati pia wamekiri kwamba kuna ukuwajuwaji wa asilimia kubwa kwenye sanaa kwenye nchi yetu toka mwaka 2015 wamesema ilikuwa asilimia 6.2, lakini sasa imekuwa mpaka asilimia 11, kwa hiyo tumeona kuna tija ya Serikali kuwekeza zaidi kwenye sanaa ili wavijana wetu waweze kujiajiri, lakini pia waweze kutengeneza vitu ambavyo vitakidhi matakwa ya malaji ambayo ni customer kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la sanaa yetu, tatizo la movie zetu za Tanzania zinakosa ubunifu, lakini zinakosa uhalisia kwa sababu ni kwanini watu wengi wanapenda kuangalia movie za nchi nyingine kama India, China, lazima tujiulize sababu ni nini, wale wana ubunifu na wana uhalisia; kwa hiyo na sisi tujikite kusaidia vijana wetu waje na ubunifu, lakini waje na uhalisia kwa sababu ni ukweli usiopingika sanaa ni another digital economic, mtu anaweza aka-act movie Tanzania ikaangaliwa Marekani na wakalipia netflix, tunalipia movie za kinaijeria kwanini vijana wetu wasiweze ku-act na nchi nyingine wakalipia wakapata kuangalia movie zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuna tatizo lazima tuangalie jinsi ya kulitatua, lakini lazima tuangalie jinsi ya kuli- facilitate. Mheshimiwa Waziri anaposema kwamba mashindano ya kitaifa, ya kimataifa, mikopo kabla ya kumpa mtu mkopo, kabla ya kumpa huyu mtu kufanya tuzo mbalimbali tuangalie ground, ground ya tatizo ni nini, kwa sababu uwezi ku-solve problem kama ujajua tatizo la problem nini tukitajiwa tatizo la problem tunaweza tuka solve problem. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema movie zetu hazina uhalisia na watu wengi hawapendi kuangalia kwa sababu ya vitu wanavyo act baadhi ya movie hizo hazivutii hata kutazama, lakini tukiongeza haya ya ubunifu na uhalisia kwa vijana wetu kwa kusaidiana na Serikali watafika mbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kuna mataifa kama Korea, kuna mataifa kama Turkish wamefanya investment kwenye sanaa kwa sababu walitambua kwamba sanaa inaajiri vijana wengi sana wakawekeza kwenye taaluma mbalimbali, wakawekeza kwenye ubunifu mbalimbali na kwenye vitu mbalimbali ambavyo vitakuza hivi vipaji vya watu, lakini watoa huduma watoe huduma ambayo inakidhi matakwa ya mlaji ambayo ndiyo customer.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa na ushauri mdogo tu kwa Serikali ambao nahisi kwamba itakuwa ni solution labda kwa soko letu la movie au wasanii wetu wa movie au wasanii wetu wa movie kwa ujumla. Unapotaka ku-solve problem kuna long term solution na kuna short term solution, mimi naona Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo waje na long term solution hata kama itatuchukua miaka mitano, hata kama kumi, lakini mwisho wa siku tuje na kitu ambacho mtu akiangalia wanasema kweli hii ni Tanzania imebadilika ya sanaa, long term plan ndiyo inatakiwa na wala siyo short term plan.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ukifanya long term plan utaanza kufanya kuanzia ground tatizo ni nini? Solution itakuwa ni nini? Na mimi kwa kufanya uchambuzi mdogo tu japokuwa na yapo mengi zaidi, lakini uchambuzi niliouona cha kwanza tufanye investment, Serikali lazima wawe willing kufanya investment, investment unaweza uka- invest leo return yake ikawa baada ya miaka 10, baada ya miaka mitano, but ikisha-turn around inakuja kuwa the best inakuja ku-solve tatizo lote kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tu-invest katika ku-empower watoto kuanzia wakiwa wadogo. Mataifa mengine wanakuwa kuwafundisha watoto kuongelea na miaka mitatu, anamfundisha mtoto kukimbia anamiaka mitatu huyu mtoto akifika hakija kuwa the best performer hakuna miujiza imetumika ni training aliyoipata kutoka chini, hawa ma- actor na ma-actress wakubwa wanaoingiza milioni za pesa kwenye nchi za wenzetu hawajatokea tu ukubwani kama mimi niende ku-act kesho wamepikwa kuanzia chini wakafundishwa, wakasaidiwa na Serikali yao kwa namna moja au nyingine kesho hakiwa anafanya vizuri ni matokeo ya investment ambayo imefanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna shule za msingi, tuanzie kwenye shule za msingi tusiongelee kwamba tuna kuna chuo watoto wataenda kusoma, huyu mtoto wa maskini hatatokaje kule vijijini aende kwenye kile chuo, tukianza kufandisha masomo ya sanaa, lakini pia tukasaidia kuboresha hata kama yapo, wakaja mwisho wanamaliza la saba wanajua kuna kipaji cha huyu mtoto, wale watu wa sarakasi wanachukua, wa ku-act wanachukua, wa sehemu tofauti wanachukua, kunakuwa na designated sekondari moja kwenye kila kanda zitakuwa nne kwa mfano unasema Singida tunasema shule fulani tunaiweka inakuwa masomo ya kawaida, lakini na masomo ya sanaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mtoto akimaliza darasa la saba ataenda form one mpaka form six kwenye shule ambayo inatoa masomo ya kawaida, lakini inatoa na masomo ya sanaa pia. Kwa hiyo, akitoka hapo hata akichuliwa kwenda ku-act atakuwa the best kwa watakaishia pale, lakini watakaoendelea na chuo wataenda Bodi ya Mikopo na itawapa mikopo. Hizi programu za fine art and perfoming designing watakuwa the best, wanaenda kupewa mikopo watamaliza tukitoka hapo sasa tutazaa kizazi kipya cha bongo movie kwa sababu waliomaliza ndio watakwenda kuleta mapinduzi ya ubunifu, wataleta mapinduzi ya uhalisia, kwa sababu kaanzia kuanzia chini kujifunza na hata atakuja kuleta uhalisia na watu watapenda vya kwao kama ilivyo sasa tofauti watu wanapenda vya nje kuliko vya kwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hayo kwa sababu Serikali isipoingilia kati kusaidia hili suala kwa long term solution tutaimba wimbo ule ule kila siku na tutaendelea kufaidika mataifa mengine tunaona Azam analipa pesa nyingi sisi tunaangalia movie zimekuwa translated Kiswahili, kwa nini tusiangalie za kwetu? Kwa nini ile pesa iende kule badala ya sisi tuipate hapa? Ni reform tu inayotakiwa kwenye suala la sanaa ambalo litasaidia vijana wetu waje na ubunifu mpya, waje na mbinu mpya tofauti na sasa hivi ukiangalia movie mtu anaweka sumu, anakoroga na anaonja; kweli utavutika kuangalia hiyo movie? Hapana, na movie hazina hisia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo soko hili ni kubwa lakini linaleta mamilionea na mabilionea wengi na tunawajua sitaki kuwataja, tuna tatizo gani tusitengeneze mabilionea hapa Tanzania au mamilionea ma-acter na maactress ambao watafanya kazi Tanzania zitauzika sehemu tofauti tofauti.

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ulikuwa mchango wangu kwa leo, lakini naiomba Serikali ije na long term solution, tukifanya short term solution atakuja Waziri mwingine ataimba Wimbo wa Taifa huu, atakuja mwingine ataimba huu kwa sababu kwa mfano mzuri tu, hawa waliiomaliza bachelor of fine art and perfoming Mheshimiwa Waziri labda ni takwimu alizonazo ni wangapi wameajiriwa walipomaliza hizi shule? Unakuta hakuna, lakini hata bodi ya mikopo hii field ambayo ni muhimu kwa sasa hivi kwa digital economy je, hao wanafunzi wanapewa mikopo asilimia 100 inavyotakiwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ndio hii tunasema tunasoma degree hazina faida lakini degree ya performing arts ina faida.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga hoja mkono, ahsante (Makofi)