Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwanza naomba nichukue nafasi hii nikushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi hii na mimi kuwa mchangiaji katika Wizara hii ya Habari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi ninalotaka kuliongelea kwenye Wizara ya Habari kwanza ni kuwapongeza namna utendaji wao wa kazi za kila siku hasa kupitia vyombo vyetu vya Serikali ikiwemo TBC. Vyombo vya habari vya Serikali vinafanyakazi kubwa sana, lakini pamoja na kazi kubwa inayofanywa bado ipo haja kwa Wizara ya Habari kuona wanafanya kila jitihada kuangalia waandishi wa habari kwa vile wao ndiyo waelimishaji wa jamii ndiyo ambao wanapasha umma katika habari mbalimbali za nchi yao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia waandishi wa habari hawa wana kazi ya kuelimisha umma, wana kazi ya kuburudisha, wana kazi ya kuonesha namna gani wanamichezo na sanaa wanafanya katika nchi yao. (Makofi)

Mimi ningeongelea jambo moja kwa waandishi wa habari, bado waandishi wa habari wanapaswa kuenziwa, wanapaswa kulindwa katika masuala mbalimbali yakiwemo maslahi yao, lakini pia yakiwemo masuala la overtime kama tunavyofahamu waandishi wa habari wanafanyakazi sana hasa wa vyombo ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, waandishi wa habari hawa ni mashahidi sisi wote kwamba wanafanyakazi bila upendeleo lakini wanajituma usiku na mchana sijui Wizara ina mpango gani kuona inaandaa fidia maalum pale waandishi wa habari wanapopata ajali wakiwa kazini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo haya naomba kuunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)