Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu na Watanzania wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuijalia nchi yetu baraka katika ustawi wa kijamii, kichumi, kisiasa, kidiplomasia mbele ya mataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuapishwa kushika hatamu ya kuliongeza Taifa letu, Mwenyezi Mungu amlinde na kubariki kutuongoza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mbulu Mjini naungana na Watanzania wote kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano katika uongozi wa Mheshimiwa Hayati John Pombe Magufuli, Rais wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano, viongozi wake waandamizi, watendaji na wadau mbalimbali kwa jinsi walivyosimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2021 hususan sekta ya viwanda kama mhimili mojawapo uliotufikisha uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha kwa namna ya pekee naomba kumwombea Mheshimiwa Hayati John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Seikali ya Awamu ya Tano, Mheshimiwa Khatib Said, Mbunge wa Jimbo la Konde, Wahshimiwa Wabunge wenzetu na Watanzania wote waliotangulia mbele ya haki, Mwenyezi Mungu awapokee katika ufalme wake wa mbinguni, Amina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nitoe mchango wangu kupitia mapendekezo ya bajeti ya Wizara hii, kwanza tunaiomba Serikali ifanye tathimini ya viwanda 100 kila Hamashauri zilizoanzishwa na Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Wizara ya TAMISEMI, kwani uwepo wa viwanda 100 ulikuwa chachu ya ajira kwa kila Halmashauri, japo kuna haja kubwa ya kuwa na Maafisa Biashara watakaosimamia, kushauri na kuratibu uendeshaji wa viwanda hivi ili kulinda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ifanye mapitio ya mchakato wa uanzishwaji viwanda na biashara kwa kuondoa vikwazo, urasimu na vigezo ambavyo siyo rafiki katika uanzishwaji wa viwanda hapa nchini kwa kuwa suala la uwekezeji lina ushindani mkubwa sana duniani kote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali ijitahidi kupeleka fedha zote zinazoombwa kwenye bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara ili kuleta ufanisi mkubwa katika sekta hii kushikilia uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iwe mstari wa mbele kusimamia suala la ubora wa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kwa ajili ya kulinda afya ya watumiaji na kukidhi ushindani, bei, ubora na soko la ndani na nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isimamie suala la kuhamasisha matumizi sahihi ya blueprint kama dira katika kuhamasisha wawekezaji hali itakayochochea uanzishwaji wa viwanda kulinda uwepo wa Tanzania kudumu katika kundi la nchi za uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja hoja asilimia mia moja, naomba kuwasilisha.