Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuchangia kwa maandishi ili kuweza kufafanua baadhi ya mambo kwenye mchango wangu kwa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ETS; kazi yake kubwa ni kuhesabu, viwanda vilifunga mashine hizi kwa maelekezo ya Serikali, lakini tija yake haifanani na gharama halisi pamoja na mengine mengi, lakini mkataba wa Kampuni ya SIPA haukuwa wazi sana hasa kwenye suala la bei ya uchapishaji wa stamp hizo. Mkataba huu ulikuwa wa miaka mitano, muda umekwisha, kuna haja sasa ya Serikali kupitia upya mkataba huo ili kuweza kuangalia upya gharama zake.

Hivi sasa kwa mfano gharama ya kuhesabu chupa moja ya juice ya mls 200 ni shilingi 23, wakati Serikali kodi yake ni shilingi 1.8 tu hivyo utaona mwenye kuhesabu anapata pesa nyingi zaidi kuliko Serikali, na hii ni kuongeza tu gharama kwa wazalishaji na hatimaye bei kwa walaji, sawa na vinjwaji baridi na vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu VAT Refund; kwa nini Serkali hairudishi kwa wawekezaji na wafanyabiashara VAT hasa kwenye viwanda vikubwa, hii pia inachangia sana kukwamisha mitaji na kudorora kwa uzalishaji kwenye viwanda. Serikali inadaiwa sasa walau kiasi cha shilingi bilioni 10 katika VAT, pia kuna suala la industrial sugar, karibu miaka mitano sasa pesa hiyo haijarudi na kusababisha viwanda vingi kuendelea kukosa operating capital, kwa mfano viwanda vya vinywaji baridi, CocaCola na Pepsi, Serikali ibadilishe utaratibu wa kushikilia pesa hi kwa sababu imekuwa mziogo mkubwa sana kwa wenye viwanda.

Kuhusu suala la unyaufu; Serikali kupitia Wizara itoe msimamo ili kuondoa athari zinazoweza kujitokeza wakati wa msimu wa ununuzi wa korosho. Unyaufu umekuwa ni tatizo kubwa na bado mpaka sasa Serikali haijawa na msimamo wa pamoja kuhusu suala hili, mwaka jana wafanyabiashara wa maghala wamepata hasara kwenye uendeshaji wa maghala kwa sababu Serikali imechukua pesa toka kwa wafanyabiashara hao na kuwa hasara kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Liganga na Mchuchuma inafaa kuwekewa nguvu zaidi ili kuweza kuendeleza migodi hiyo, pia lazima kuwa na mfumo ulio wazi kwenye jambo hili, lazima sasa Liganga na Mchuchuma zianze uzalishaji ili kuchangamsha uchumi wa Ukanda wa Kusini Bandari ya Mtwara na reli ya Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu biashara ya korosho; katika Ilani ya CCM 2020 - 2025 kuhusu eneo la viawanda vya korosho, ibara ya 34 sehemu ya (c) iliahidi kuanzisha Cooperative Seed Fund, huu ni mfano wa REA, Mfuko wa Maji na Road Fund, kwenye mpango huu CCM ilidhamiria pamoja na mambo mengine kuanzisha viwanda 33 vya kubangua korosho, pamoja na kufufua viwanda vingine vilivyokufa na kufanya ubanguaji kufikia asilimia 50, tani 550,000 kufikia mwaka 2025, vipi bajeti ya Wizara hii imeweza kujibu hii ilani na mkakati uliopo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri sasa jambo hili liwe katika utekelezaji, kuna hasara kubwa sana inapatikana kwenye korosho, hadi sasa korosho ghafi na mazao yake yanauzwa ni pamoja na ajira, nchi inapata hasara kubwa sana, maganda ya korosho ni uchumi, sawa na mabibo, kochoko ndiko ambako wine na mvinyo zinakotokea, kwa mfano Scotland ambako ndiko unakotengenezwa mvinyo wa Scotish Whiscky, wanaliingizia Taifa lao Euro bilioni 4.5 kwa mwaka jana peke yake. Wizara ione namna ya kushirikiana na Wizara ya Katiba na kuamua kubadilisha Sheria ya Vileo (Liquer and Intoxication Act ya 1978) ili wananchi sasa waweze kuzalisha gongo kitaalamu na kuweza kujipatia pesa za kigeni lakini pia ni sehemu ya uchumi kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.