Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema ambaye ameniweka hai na kuweza kuchangia bajeti hii ya viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kujielekeza kwenye bajeti hii kwa kuangalia baadhi ya vitu mimi sina shaka na mipango, mipango ya Chama chetu cha Mapinduzi lakini mipango pia ya Serikali sina shaka. Tumekuwa na mipango mizuri mingi sana tangu Serikali ilivyoanza kuundwa na mpaka hivi leo, ukiangalia bajeti za kila mwaka utathibitisha hilo. Kwa miaka mitano hii inayokuja mipango yetu imekuwa mikubwa na mizuri sana na kama tunavyojielekeza kwenye bajeti ya uchumi endelevu, lakini uchumi shindani pia hili ni jambo zuri kabisa na ni jambo jema lakini tunahitaji kujielekeza nguvu zetu katika utekelezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri tuna shida sehemu katika suala hasa la bajeti kuangalia vipaumbele. Tumekuwa hatujikiti sana katika vipaumbele vya bajeti zetu, tunaongea mambo mazuri, lakini katika utekelezaji nafikiri kumekuwa na changamoto, tuangalie mfano mdogo tu katika bajeti zetu, ukiangalia bajeti ya viwanda kwa mfano bajeti hii ndio mkombozi katika uchumi wa nchi hii kwa sababu kwa kutumia bajeti hii tungeweza kwa namna moja au nyingine kufikia malengo yale ya uchumi endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu gani kama tungeingia kwenye vipaumbele, lakini ukiangalia unakuta miradi ambayo tunajaribu kutaka kuitekeleza ambayo kwa hali halisi ndio miradi ya mkakati unakuta kitu tofauti kwa mfano Mradi wa Liganga na Mchuchuma ambao ni mradi mkakati kwa mwaka 2020/2021 ulitengewa takribani shilingi milioni 120 tu, mwaka 2021/2022 umetengewa shilingi milioni 25. Kwa kweli hatuko serious kabisa kama kweli tunataka kufanya yaani kwamba kama miradi hii ni mradi mkakati tofauti tunachoongea na kile tunachokifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia Mradi wa Mchuchuma tumetengewa takribani shilingi milioni 120 peke yake mwaka 2020/2021 lakini mradi huo huo pia tumetengewa takribani shilingi milioni 25 katika msimu wa mwaka 2021/2022 kwa kweli hatupo serious, hatupo serious kabisa, lakini mradi wa Ziwa Natron wenyewe ulitengewa shilingi milioni 50 peke yake, hali kadhalika kwenye mwaka 2021/2022 ulitengewa shilingi milioni 24 kwa kweli haioneshi kabisa kama sisi tupo serious katika huu uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu tukitaka tuendelee kwa umakini kabisa uchumi wa viwanda lazima tufanya seriousness, ionekane kabisa kwa sababu ukiangalia kiasi kilichotengwa kwa maendeleo kwa takribani kwa miaka hii miwili haizidi bilioni 30 sasa sijui kama kweli tunataka kutekeleza maendeleo ya viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kuzungumza ni nini; kama tutajielekeza kweli kwenye uchumi wa viwanda kikweli kweli tunaweza tukaendelea vizuri sana na tukawa tumepata tija kubwa na mafanikio makubwa sana katika maendeleo na hatuwezi kujidanganya hatuwezi kuendelea pasipo kuendeleza viwanda, kwa sababu viwanda ndio vyenyewe vinakula material, material nyingi sana ambazo sisi tunatengeneza hapa ina maana kwamba kwenye kilimo kwa mfano, lakini kwenye maeneo mengine ya uchumi kwa mfano ya madini na hali kadhalika kwenye maeneo mengine ya uchumi kwa mfano yanayotokana na bahari yaani kwenye uchumi wa blue hivi vyote vinatumika na viwanda ndugu zangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo bila viwanda hivi vitu vyote tunavyovizungumza haviwezi kufanikiwa na hatutaweza kuviendeleza, kama nilivyojaribu kuangalia kwa mfano tuchukulie mfano tuone muonekano halisi wa kadri jinsi haya mambo yanavyokwenda yanavyoweza yakatupatia tija. Tuna issue ya EPZ ambaye na yenyewe hatuoni kama tuna u- seriousness.

Mheshimiwa Mwenyekiti, EPZ kwa mfano pale Benjamin William Mkapa Serikali iliwekeza pale shilingi bilioni 36.4 kwa ajili ya kufidia na kuweka miundombinu, lakini ukiangalia pale kilichotokezea tulipata tija kubwa sana kutoka kwenye hiyo shilingi bilioni 36 tuliyowekeza tija tulizozipata pale tulipata uwekezaji wa mtaji yule mwekezaji aliweka mtaji wa shilingi bilioni 134; unaweza ukaona ni fedha nyingi kuliko tulizowekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa shilingi bilioni 36 tuliyowekeza tumepata shilingi bilioni 134 kama uwekezaji wa mtaji, lakini kampuni pia ilifanya mauzo ya shilingi bilioni 385.93 na kampuni hizo pia zilifanya matumizi ya fedha ambazo takribani shilingi bilioni 2019.184 lakini pia Serikali ilipata faida kupitia kodi ya shilingi bilioni 22.67 on top of that tulipata ajira ya watu 3,156.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnaweza mkaona kwa jinsi gani tija kubwa ya shilingi bilioni 36 tu imezalisha haya yote haya tumepata Watanzania, kama tungewekeza vya kutosha Benjamin William Mkapa bila shaka mngeweza mkaona tija gani mngepata hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ukiangalia SEZ eneo na Bagamoyo Serikali iliwekeza shilingi bilioni 26 peke yake lakini katika kuwekeza shilingi bilioni 26 Serikali ilikuja ikapata tija kubwa sana kulikuwa na tija kwa mfano shilingi bilioni 4.8 ya uwekezaji; mwekezaji aliweka hizo fedha, lakini mwekezaji pia alifanya mauzo ya nje ya shilingi bilioni 56.2 lakini kama haitoshi kampuni pia ilipata kwa kulipa kodi shilingi bilioni 1.305. Kwa hiyo unaweza ukaangalia kwa kiasi kidogo tu cha shilingi bilioni 26 tulizowekeza Bagamoyo tumepata fedha nyingi hizi, lakini cha kushangaza hapo hapo Serikali inadai kujaribu kurudisha baadhi ya maeneo ambayo tungeendelea kuyawekeza ya SEZ kwa kweli hatupo serious na kama tupo serious kwa kweli tunatakiwa tuwekeza kikamilifu kwenye viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, lakini naomba seriousness kwenye viwanda ifanyike, ahsante. (Makofi)