Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, kuhusu Agricultural Trust Input Fund (AGTIF), hiki chombo lazima kifanyiwe maboresho, badala ya kusaidia wakulla kinachangia kuua morale wa kilimo Tanzania. Mfano mkulima amekopa shilingi milioni 40 na amewekewa cummulative interest ya shilingi milioni mbili na total ni shilingi milioni 42 kwa miaka mitano, hapa taasisi inafahamu kilimo cha Tanzania ni cha mvua na masoko hayapo. Lakini mkulima baada ya kulima akipata mazao soko hakuna, yanauzwa au anauza underprice wakati huo AGTIF madai yao yapo pale pale.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kwa kuwa analima kwa kutegemea mvua, kilimo kinategemea msimu na hali ya hewa. Sasa inatokea hakuna mvua ya kutosha, ratiba ya malipo ya AGTIF ipo pale pale, mkulima baada kuona kilimo hakimlipi atakopa pesa popote kulipia mkopo wote wa AGTIF kwa muda uliopangwa wa miaka mitano mitano, lakini atakutana na riba kubwa ya zaidi ya asilimia 50 ya principal.

Mheshimiwa Spika, hili jambo halikubaliki Serikali kuuza mali za wananchi waliokwisha kulipa principal yote pamoja na interest ya Serikali bado AGTIF wanataka kuuza sababu ya penalt interest ya kuchelewa kurejesha.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Serikali inapokopesha mkulima iwe na backstop follow up kujua situation anayo face mkulima na iondoe kabisa riba kwa mkulima aliyelipa mkopo wote ndani ya muda wa mkataba.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.