Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sekta ya kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa letu basi Serikali ilipe kipaumbele suala hili la bajeti ili kukidhi mahitaji ya Maafisa Ugani, mbegu, mbolea bora na pembejeo kwa ajili ya kuchochea hali ya wakulima na hivyo kuchochea uzalishaji bora wa mazao ya chakula na biashara.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali izamilie kuwasaidia wakulima wetu kuuza mazao kwa bei yenye tija na kupata masoko ya uhakika hasa kwa mazao ya kahawa, pamba na kadhalika ili kuwezesha mkulima kunufaika ipasavyo na kilimo.

Mheshimiwa Spika, kutokana na ukosefu wa mbolea umewafanya wakulima wetu hasa waliopo karibu na mipaka mfano Wilaya ya Tarime wakulima wamekuwa wakinunua mbolea Kenya ili kukidhi mahitaji ya kilimo hii pia ni kwa kuwa mbolea yetu haiwafikii kwa wakati lakini pia ikiwepo huuzwa kwa bei ya juu zaidi.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ifanye haraka upatikanaji wa mbolea katika mipaka hiyo ili pia kuzuia magendo ya mbolea, kwa sababu wakulima wanafuatwa mpaka mashambani na TRA kuwakamatia mbolea hizo.