Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kunipatia nafasi hii awali ya yote nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai mpaka leo nipo hapa Bungeni. Lakini sambamba na hilo nianze kwa kuwapongeza viongozi wa wizara hii Kaka yangu Mheshimiwa Profesa Mkenda na kaka yangu Mheshimiwa Bashe pale mnafanyakazi vizuri Mungu awabariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikianza na mchango wangu kwenye hii wizara nikiwa kama mkulima wa zao la tumbaku namwakilishi wananchi waliowengi wanaolima zao la tumbaku naiona kabisa Serikali haina nia ya dhati kabisa ya kuhakikisha hili zao linaendelea kuwa ni kitega uchumi cha wananchi wetu, lakini pia ni mbadala wa kuweza kuhakikisha hawa watu badala ya mazao mengine yanayowafanya waweze kudidimia liweze kupanda mbele.

Mheshimiwa Spika, zao hili limekuwa na changamoto sana pamoja na kuwa Serikali ilituahidi mambo mazuri sana kuanzia mwaka juzi na mwaka jana, lakini bado naona kama ahadi zake hazitekelezeki na zaidi ya yote tunawadanganya wakulima wetu. Ni miongoni mwa wakulima watumbaku, nimefaidika sana na tumbaku, lakini kwa miaka mitano iliyopita bado hili zao limekuwa lina misukosuko mingi na bado mbadala wake hatujapata.

Mheshimiwa Spika, mfano leo hii tuliahidiwa wakulima tumbaku kwamba tutakuwa na uhakika wa soko la tumbaku yetu. Ninachokuambia kwenye jimbo langu wanunuzi watumbaku badala ya kununua bei elekezi iliyopangwa na Serikali ambayo ilikuwa ni dola 1.61, leo hii wakulima wameuza tumbaku yao chini ya bei elekezi dola 1.2. Wakati gharama za uzalishaji wazao hili kwa kilo moja ni dola 1.4, leo hii, gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa halafu unakwenda kununua tumbaku ya huyu mkulima kwa bei ndogo, tunania ya dhati kuhakikisha kweli huyu mkulima anasonga mbele au tunamrudisha nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali kama tunania ya dhati kabisa kuhakikisha ili zao na wakulima wetu wanasonga mbele hebu tuweze kuhakikisha haya masoko ya tumbaku yanakuwa yanafuata bei elekezi, lakini pia yawe na uhakika wa kununua hizi tumbaku. Tunaona kuna makampuni mengi yatumbaku halafu tunaita ya wazawa hayana uwezo wa kununua tumbaku matokeo yake wananchi wetu wanakuwa na madeni siku baada ya siku hawalipwi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niiombe sana Wizara na Kaka yangu Bashe pale nakumbuka tumeongea sana hili suala la hawa wakulima wa tumbaku, kuna kampuni kama ya GRAND, kuna kampuni ya MAGEFA hizi kampuni zina waletea mzigo sana wananchi wetu. Tunaona kabisa, kwanza kuna riba ya asilimia nane ya mkopo, anayesababisha hii riba iongezeke ni hawa hawa wanunuzi wanashindwa kupeleka pesa kwenye vyama vya msingi matokeo yake anayekuwa responsible kwa ajili ya kulipia hiyo riba ya asilimia nane ni mwananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini sasa Serikali msione kuna haja ya huyu anayesababisha hii riba iongezeke ndiyo awajibishwe. Nataka Kaka yangu Mheshimiwa Bashe na Kaka yangu Mheshimiwa Prof. Mkenda pale mkija ku-windup mtuambie hawa wanaouza kwanza tumbaku yetu chini ya bei elekezi mnawachukulia hatua gani? Lakini pia hawa wanaosababisha riba ya asilimia nane iongezeke ili hali Serikali imekaa kimya tunataka mtupe majibu la sivyo nitashika shilingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini, nakumbuka mwaka jana tukiwa kwenye kampeni Mheshimiwa Bashe tulikuwa naye kule na Mama Samia Suluhu wananchi wa Urambo, Kaliua, Ulyankulu wa Tabora kwa ujumla walipewa matumaini kwamba mwaka huu tumbaku yao itauzwa kwa bei nzuri na hata yale makinikia yale ma-reject yatauzwa kwa shilingi 500, nataka niwaulize hivi mlishawahi kufanya research kwamba hivi haya makinikia haya ma-reject mnaenda kuyanunua kwa shilingi 500 mnakwenda kuyafanyia kazi gani? Hatujawahi kuambiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia tunaona mwaka jana kuna mnunuzi kutoka Kenya na Sudan walikuwa wayanunue haya ma-reject kwa bei ya shilingi 100 je, mliweza kujifunza kwamba huko wanakoyapeleka wanayafanyia shughuli gani? Kuliko kuwaacha wakulima wetu huku mnanunua kwa shilingi 500 kumbe yanaweza kuwa yanabei kubwa huko nje ya nchi kuliko kuwakandamiza wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niombe tena suala jingine, suala jingine niombe sasa kulikuwa kuna mnunuzi mkubwa TLTC ambaye alikuwa anauhakika wa kununua tumbaku yetu…

(Hapa kengele ililia na kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)