Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Wizara hii nyeti ambayo imegusa maisha ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya katika Wizara lakini vilevile kuwapa pole kwa haya ambayo yanaendelea kutokea. Yote haya naamini kabisa yanatokana na ufinyu wa bajeti ambapo kwa namna moja au nyingine kama wangeweza kupata fedha nyingi haya yasingetokea.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi kubwa ambayo Wizara inafanya, naomba niseme bado kuna kazi kubwa ambayo Wizara inaifanya katika kuinua kilimo kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, mimi nijikite kwenye eneo moja tu; naamini kabisa kilimo chenye tija na cha uhakika kwa Mtanzania ni kilimo cha umwagiliaji. Hadi hivi sasa tunavyozungumza kupitia Tume ya Umwagiliaji, tunaambiwa kwamba kuna lengo la kulima hekta milioni moja na laki mbili na hadi hivi sasa tumefikia asilimia 58 ambayo ni hekta 695. Ombi langu na ushauri wangu kwa Serikali, naomba tujikite kwenye maeneo ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, nianze na moja tu, tunapoteza maji mengi ambayo yanakwenda baharini na Serikali imekaa hatuingii huko. Mfano, nataka nizungumzie kwenye Bonde la Kongwa unapoingia Kibaigwa, maji yanatiririka mwaka mzima, yanakokwenda hapajulikani lakini pale tungeweza kuchimba mabwawa watu wakafanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile Mto wa Dumila, mpaka tunaharibu barabara, zinakatika. Mimi niishauri Serikali katika maeneo kama yale ya Dumila, Ruvu, hebu tungechimba mabwawa watu waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji ambacho kitaweza kuleta tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi Watanzania wanalima maeneo makubwa, dhamira kubwa ni kukusanya kidogokidogo kwenye kila hekta ili kuweza kupata tija. Nilipata nafasi ya kwenda China mara mbili, mtu analipa hekta tano, tatu analima mpunga mbili analima kilimo cha horticulture, ndani ya mwaka anapata tija kubwa kuliko Mtanzania ambaye analima hekta mia katika Tanzania yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi naamini kabisa kilimo cha umwagiliaji ndicho ambacho kitamkomboa Mtanzania. Mkoa wa Morogoro umeambiwa ni FAMOGATA – Fanya Mkoa wa Morogoro kuwa Ghala la Taifa la Chakula. Ndani ya Mkoa wa Morogoro tuna eneo ambalo linatosha kwa kulimwa kwa kilimo cha umwagiliaji hekta 230,000 lakini mpaka hivi sasa tumetumia hekta 28,000 tu. Kama kweli we are serious na kilimo hebu tu-inject hela katika kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Jimbo langu la Morogoro Kusini tuna mradi wa Kongwa Tulo ambao una uwezo wa kulima hekta 3,000. Hadi hivi sasa zimetumika hekta 200 tu. Kuna mradi wa Mbangarawe, kuna hekta 230 tumetumia hekta 200 tu bado 30. Kuna mradi wa Lubasazi, una uwezo wa kulima hekta 120, hadi hivi sasa kuna shilingi milioni 800 imewekwa pale lakini bado mradi haujaendelea, maana yake tumeweka fedha ambazo hazitumiki. Kuna mradi wa Kirokwa ambao una hekta 105, mpaka dakika hii tunatumia hekta 40.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ukijaribu kuangalia, tuna-ijnect fedha kwenye miradi lakini haifanyi kazi. Tumeomba katika mradi wa Kongwa Tulo ili tuweze kuendelea mwaka karibu wa pili huu sasa, nilikuwa Mbunge miaka mitano iliyokwisha, miaka mitano nimekwenda likizo, hakuna kilichowekwa. Sasa hivi tumeomba tena shilingi bilioni 1.4; Mbarangwe shilingi bilioni 1.5; Lubasazi shilingi bilioni 1.5; Kiroka shilingi bilioni 3, ukijumlisha ni shilingi bilioni 7. Fedha hizi tukipeleka pale nina uhakika tutanyanyua kilimo cha Watanzania na wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile nizungumzie suala la masoko. Kwa kweli watu wengi wamezungumzia suala la masoko; ni kero kwa wakulima wetu. Hivi ninavyozungumza kuna wakulima wangu kule mazao yako ndani na wanakaribia kuuza nyumba zao kama hatutaweza kuwasaidia kuwapatia masoko.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)