Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante nianze kwa kumpongeza sana Waziri wa Kilimo na naibu wake pamoja na timu ya wataalam kwa kazi nzuri wanayoifanya Wizara yetu ya kilimo. Nitachangia kwenye sehemu mbili ya kwanza ni umuhimu wa kuongeza bajeti ya kilimo nataka niiombe Serikali kitu hapa na cha pili ni fursa zilizopo Mkoani Kilimanjaro kwenye sekta ya umwagiliaji hasahasa kwenye jimbo langu la Moshi Vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wote tunakubaliana kabisa kimsingi kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu na muhimili mkuu kwenye kukuza uchumi wa Tanzania. Kilimo inachangia vitu vingi sana asilimia 65 ya watanzania wako kwenye kilimo inachangia asilimia 27.5 kwenye pato la Taifa asilimia 24.7 kwenye fedha za kigeni asilimia 60 kwenye malighafi za viwanda na asilimia 100 kwenye chakula cha nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na umuhimu huo wa kilimo hawa watu wanapewa hela ndogo sana, Serikali inatenga pesa ndogo sana kwenye hii Wizara na tunamlaumu waziri na timu yake lakini kusema ukweli shida haiku kwa hawa watu. Kwa sababu hata wewe Mheshimiwa Spika jana uliongea nikafurahi sana, ni mtoto wa mkulima unaguswa na kuna kitu kizuri hakiko sawa sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pesa ambayo Wizara ya Kilimo imetengewa kwenye bajeti ambayo waziri ameaomba ni asilimia 0.08 haijafika hata one percent, mnataka waziri afanye nini na timu yake jamani, sisi kama Serikali, hela hii ni kidogo na haitoshi tukilinganisha bajeti za nchi zingine za nchi za Afrika Mashariki ambazo Kenya Uganda na Rwanda hawa wanawekeza vizuri sana kwenye kilimo ukilinganisha na sisi watanzania ambao tunalima kwa uhakika zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika niishauri Serikali ni muhimu kabisa tuongeze bajeti ya kilimo tukisema tumewapa pesa tuwape hili wafanye kazi, bila hivyo tutakuwa tunalalamika na hatuwatendei haki wakulima wetu. Niseme kwamba kuna declaration ya Malabo ambayo Serikali yetu iliingia mwaka 2014 tarehe 26 mpaka tarehe 27 Juni. Viongozi wa nchi wakakubaliana kwamba tutatenga angalau asilimia 10 ya bajeti iende kwenye kilimo kwenye haya mataifa maraisi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naona hatujafika hata one percent jamani tunakwenda wapi niombe tu angalau tungekubaliana na hiyo ten percent kilimo leo tungukuwa tunawapa kitu kama tirioni 3.6 ambayo wangeweza wakafanya kiti kidogo, wakaboresha utafiti wakaboresha ugani, na vitu vinginevyo ambavyo wameweka kwenya mpango wao. Kwa hiyo, ombi langu kwa Serikali na Waziri Mkuu wetu yupo hapa baba yetu Waziri Mkuu tunaomba kabisa Wizara ya Kilimo iangaliwe kwa jicho la huruma kwa sababu tunavyokwenda sio sawa kabisa nakubaliana na Mheshimiwa Joseph Kandege bajeti ya kilimo ni ndogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hilo niende kwenye jimbo langu sasa Mkoa wa Kilimanjaro una fursa nyingi sana za kilimo cha umwagiliaji eti tumebarikiwa kuwa na ule mlima unatiririsha maji mengi sana kutoka mlimani na yanaishia bahari ya Hindi. Bahati mbaya sana maji haya hayajatumika vizuri, nina naishauri wizara itumie hii fursa ya yale maji badala ya kuishia baharini na kuuwa watu kwenye mafuriko tuwekeze tujenge skimu za kutosha tuboreshe ile mifereji ili kilimo kule Kilimanjaro tutoe mchango kama tulivyokuwa tunafanya zamani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna maeneo ya ukanda wa tambarare kule jimboni kwangu, eneo la Mabogini tunaweza tukajenga skimu mpya, kuna kama hekta 1,350. Kata ya Arusha Chini tunaweza tukajenga skimu mpya kwenye vijiji viwili, kuna hekta kama 2,000. Kuna eneo la Old Moshi Mashariki kwenye Kijiji cha Mandaka Mnono kuna hekta 1,250. Tukiwekeza katika maeneo haya, nina uhakika tutachangia kikamilifu katika zile hekta ambazo Serikali inategemea kuboresha kwenye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naomba kuunga mkono hoja. Naomba sana tuifikirie Wizara ya Kilimo kwenye funding. Ahsante sana. (Makofi)