Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo katika wizara hii nyeti, lakini pia niseme kwamba nina imani na wizara hii kwa sababu ina viongozi makini ambao wamekuwa wakiendelea kufanya kazi vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mambo machache ambayo ningependa kuongelea kupitia wizara hiikwa maana ya kukjenga ili tuweze kuona tunaelekea wapi katika kuboresha kilimo nchi hii, nilikuwa napitia taarifa tuliyopewa hotuba ya Waziri kuna mambo baadhi niliweza kuyaona yakanipa shaka kwamba hivi tunakoenda tutafanikiwa kweli au tataendelea kupiga mark time.

Mheshimiwa Spika, niliona suala la takwimu wakakiri wazi kwamba hakuna takwimu zinazoonyesha mahitaji ya mbegu nchini, wakulima wapo tunawafahamu na tunajua kabisa maeneo gani wanalima nini na maeneo gani wanalima kilimo gani, watusaidie kupata hizi takwimu ili wanapokuja kama ni suala la mbolea tujea wanatuletea mbolea kiasi gani ambazo zinahitajika na watanzania. Lakini kama ni suala la mbegu wajue kwamba ni kiasi gani cha mbegu kinachohitajika Tanzania ili tuweze kuwa na uhakika wa hizo mbegu.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujikita kwenye suala la uzalishaji wa mbegu nchini hapa Tanzania tunamekuwa na baadhi ya makampuni private ambayo yamekuwa yakiendelea kuzalisha mbegu, lakini tuna shirika pia la kiserikali ambalo limekuwa likiendelea kuzalisha mbegu. Hatujapata takwimu kujua kwamba ni makampuni mangapi Tanzania mpaka sasa yanazalisha mbegu.

Mheshimiwa Spika, naamini kama wizara itajikita kwenye kuwawezesha wazalishaji wa mbegu, hizi tunazohitaji nchini nchi yetu itaweza kufanya vizuri, ndipo ambapo tunaweza kuona kwamba kilimo kinageuka kuwa ni fursa ya kiuchumi kwa maana kwamba tutaweza kuzalisha mbegu nyingi na tutaweza kuuza nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa taarifa niliyo nayo mpaka sasa Tanzania tuna kampuni moja tu ambayo inauza mbegu nje ya nchi na nimesikia kwamba uwa wanauza Rwanda. Lakini changamoto ambayo wanayo haya makampuni ya mbegu mojawapo imekuwa ni kwamba hawajapata support ya kutosha kutoka Serikalini na wao kama wao wangependa kuona kwamba Serikali inaitambua hii sekta na kuipa kipaumbele hili waweze kufanya vizuri katika uzalishaji wa mbegu nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kiufupi ni kwamba tume- experience kwa nyakati tofauti kumekuwa na uhaba wa mbegu mfano kwetu sisi Songwe tumekuwa tukiona kabisa wazi mbegu wakulima wanachukuwa Zambia wanakuja kupanda Tanzania kwa upande fulani inakuwa ni Illegal business lakini ndio inayowasaidia kama Tanzania tukijipanga vizuri kwenye mbegu naamini tutaweza kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, makampuni haya yanatamani kungekuwa na uwezeshaji kwa namna ya kwamba kuwe angalau na grants hizi ruzuku lakini pia kufanyike uwezekano kwa mabenki ambayo yanatoa mkopo kwa riba nafuu ili yaweze kuijenga vizuri. Kwa mwaka 2014/2015/2016 tunafahamu sote, haya makampuni ya mbegu yalipewa kazi ya kugawa mbegu kwa mawakala kwa njia ya ruzuku na tunachofahamu mpaka sasa makampuni haya mengi hayajalipwa pesa zao.

Mheshimiwa Spika, na kwa maana hii kwa kutokulipa pesa hizi kwa wakati Serikali kwa makampuni haya yanashusha uwezo wamakampuni haya kuweza kujiendesha na mengine yamefilisika yamekufa. Kwa hiyo, nilitamani sana kusikia kauli ya Serikali kuona kuwa watalipa lini fedha zao ili makampuni haya kama yanakosa ruzuku kama wanakosa mikopo basi pesa zao wapewe ili waweze kuzalisha kwa upana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini baada ya kusema hayo pia nimepitia eneo la uzalishaji wa mbolea nikaona kwamba mahitaji ya mbolea Serikalini tumeweza kufanikisha kuyafikia kwa asilimia 94.4, ni kiwango kizuri wizara imejitahidi lakini katika eneo hili kuna baadhi ya mambo niliweza kuona kama ni changamoto.

Kwanza niliambiwa kwamba mbolea ambayo inazalishwa nchini ni tani 32239 nikajaribu kutafuta percent kwa kujua mbolea iliyopo nchi iliyozalishwa ndani ni ngapi nikapata ni asilimia 4.75 kitu ambacho nikaona kama uzalishaji wa ndani ni mdogo hivi mbona ni shida.

Mheshimiwa Spika, na sisi tunakiwanda chetu cha Mijingu…

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Neema.

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)