Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa fursa hii muhimu, nianze kwa kuipongeza Wizara.

Mheshimiwa Spika, wakati umenitaja nichangie nilikuwa naangalia viongozi wakuu wa hii Wizara. Nimetazama Waziri naona ni Profesa, nimetazama pia nafahamu kaka yangu Bashe yeye ana Masters lakini namuona pia Katibu Mkuu yeye naye bila shaka ana Masters lakini pia kuna Prof. Siza.

Mheshimiwa Spika, normally people they do not care about how much you know until you know about how much you care. Naomba nirudie normally people they do not care about how much you know until you know about how much you care. Telling people, you are a professor/Ph.D holder/ Masters’ holder is nonsense if you don’t deliver services to the society. Kuwaeleza watu kwamba mimi ni profesa, daktari, nina masters kama hutoi huduma kwa jamii ni kazi bure. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, changamoto sio weledi, sina mashaka na weledi wa viongozi wa wizara hii ni mahiri kabisa kwa maana ya knowledge. Changamoto kubwa niliwahi kusema hapa na hii ni kwa Watanzania tulio wengi ni mambo matatu; la kwanza ni mtazamo (mindset), la pili ni commitment na ya tatu ni uzalendo basi, sio fedha. Tunazungumza financing, kwenye kilimo hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niseme neno moja, nchi za Ulaya karne ya 16 zilianza mapinduzi ya kilimo (agrarian revolution) ndiyo wakaenda kwenye viwanda, walivyotoka kwenye mapinduzi ya kilimo wakaenda kwenye mapinduzi ya viwanda karne ya 18. Na walifanikiwa tu baada ku- engage private sector, kazi ya Serikali tusi-engage pia na kwenye masuala… kazi moja tu nishauri Wizara tuandae mashamba mazuri yaliyopimwa vizuri, tutafute private sector tuwaambie tunawakabidhi haya; ukienda Zambia wanafanya hivyo na nchi zote zilizofanikiwa kwenye kilimo wanafanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, leo hii hata tukisema hapa bajeti ya Wizara ya Kilimo iongezwe kutoka asilimia 0.8 hiyo fedha unatoa wapi, haipo; turuhusu sekta binafsi. Kazi ya Wizara iwe ni namna ya usimamizi…

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Pokea taarifa Mheshimiwa Godwin.

T A A R I F A

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nimpe taarifa mzungumzaji kwanza anachochangia ni sahihi sana na kimsingi sio kwamba tutafute private investors kwenye ishu ya kilimo, wapo vijana ambao wanafanya vizuri ambao hata Wizara ni mashahidi na watu wa SUA ni mashahidi. Vijana kama Malembo Farm ambao wanafanya consultation, RAYMAK wapo Miyuji tu hapa Dodoma ambapo pia Wabunge wanaweza kwenda pale kuona RAYMAK yupo pale anafanya agribusiness. Kwa hiyo, wapo vijana ambao wameshajitolea kufanya hiki na wanafanya mpaka greenhouse, wanafanya vitu vikubwa sana. Kwa hiyo, tunaweza tukaanza na hao kuwapa hata ruzuku waendelee kufanya shughuli zao, ahsante. (Makofi)

SPIKA: Unaipokea hiyo taarifa Mheshimiwa.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nadhani anaendelea kuniunga mkono.

Mheshimiwa Spika, niendelee kusema tu kwamba lakini pia financing agriculture, tutafute benki ambazo zisikae Dar es Salaam, Dodoma wala zisikae mijini ziende kwenye maeneo ya kilimo. Yaani mkulima anaweza kukopa benki iwe kwenye Kata yake. Leo hii ukimwambia mkulima kuna benki zinazo-finance kilimo hawajui, hawajui kabisa. Kwa hiyo, twende kwenye private sector kama nilivyosema awali tutenge maeneo maalu, lile shamba lipimwe liwe na hati mkulima anaweza kukopesheka. Kwa hiyo, Wizara hizi zishirikiane; Wizara ya Kilimo, Wizara ya Ardhi na Wizara ya Viwanda wafanye kazi kama timu moja. Naamini tunakwenda kufanya mapinduzi makubwa ya kilimo ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nijikite kwenye eneo hili la zao la mpunga; tumekuwa tukizungumzia mahindi. Duniani kote chakula kinacholiwa na watu walio wengi ni mchele kwa maana ya mpunga, sio mahindi, mahindi wakati mwingine Marekani wanakula Wanyama lakini mpunga/mchele wanakula wanadamu duniani kote, ukienda Japan wapi. Sasa zao la mpunga leo hii ukiuliza soko la mpunga na hii niiseme nisije nikasahau wakati Mheshimiwa Waziri unakwenda kuhitimisha bajeti yako nisaidie umejipangaje hasa kwenye soko la zao la mpunga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jimbo langu nalima zao la mpunga kwa maana ya Mkoa wa Morogoro ukiondoa wenzetu wa Mbarali na Kyela, Jimbo la Mlimba tunashika nafasi ya tatu kwa kilimo cha zao la mpunga lakini wananchi wangu mpaka leo. Mwenyewe nimefungia gunia 70 ndani sina mteja. Sasa na mimi mkulima pia, nataka ni-declare interest hapa. Kwa hiyo, nimefunga mpunga wangu upo ndani sina mteja wa kuuza, Mbunge sina je wananchi wangu ikoje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, itoshe kusema tusijikite kwenye mahindi ambayo wakati mwingine yana alternative, mpunga hauna alternative. Kwa hiyo, tutafute masoko kwenye zao, hata maghala huwezi kuona ghala la mpunga; lipo ghala la zao la mpunga, hamna hata maghala tu. Kwa hiyo, zao hili ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, nirudi tu moja kwa moja nijikite kwa wananchi wangu wa Jimbo la Mlimba ambao wamenituma nifanye kazi hii. Pale Kata ya Mngeka kuna shamba la Serikali la hekta 5,000. Shamba hili hekta 3,000 tayari zina miundombinu ya umwagiliaji lakini huu ni mwaka wa nne shamba lile Serikali imelitelekeza; leo tunasema irrigation scheme iko pale hatuitumii.

Mheshimiwa Spika, namshukuru Wizara ya Fedha imeanza kuchukua hatua, kulikuwa kuna deni la NMB kuna mwekezaji uchwara alienda pale sijui akafanya nini akaondoka akaacha deni kama bilioni 10, jana Mheshimiwa Waziri wa Fedha amenipa matumaini amesema sasa wamechukua jitihada wanakwenda kulipa lile deni lakini changamoto hizi hekta 5,000 zinakwenda kufanya nini.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mlimba miaka ya 1985 wakati Hayati Baba wa Taifa amepata msaada wa nchi ya Korea ili nchi yetu ijikimu katika chakula, alipata msaada huo Wakorea wakaja wakajenga mitambo kila kitu hadi umeme tunafua pale wenyewe megawatt karibu 350 tunatoa pale ile mitambo iko pale kama park elephant.

Mheshimiwa Spika, sasa nikanasema namshukuru Waziri wa Fedha, akishalipa hilo deni la NMB, hizo bilioni 10 msimu ujao kama Serikali haijatuletea mwekezaji pale nitawaambia wananchi wangu tukalime, hatuwezi tukaacha maeneo yanakaa tu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitachukua hatua tu, nitaenda kuhamasisha wananchi wa Mlimba, tukalime hizo hekta 5,000 nadhani tutasimamiwa na Halmashauri yetu ya Mlimba.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Musukuma.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba kumpa taarifa mzungumzaji, niko Kamati ya Nishati na Madini sijawahi kusikia kama Mlimba tuna megawatt 350, kilowatt au megawatt ili kumbukumbu zikae sawa.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, sipokei taarifa kwa sababu haihusiani na hoja ninayojenga hapa, naomba niendelee.

Mheshimiwa Spika, nataka kusema nini? Nazungumzia suala la zima la namna gani tunaweza kufanya kilimo chetu kiwe na tija, kwa mfano, tunaeleza kwa Habari ya asilimia 65 ya wakulima, na kule ukienda kijijini wako wazee tu sisi vijana wote tuko mijini kwanini kilimo hakituvutii kwa sababu Serikali haijaweka mazingira Rafiki kwa vijana kupenda kilimo. (Makofi)

MHE. ENG. AISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Na kwa bahati mbaya tunasema ajira, ajira!

SPIKA: Naona kuna taarifa nyingine tena endelea Mheshimiwa nimekuona.

T A A R I F A

MHE. ENG. AISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa mzungumzaji kwamba anachosema ni kitu sahihi kuna daktari mmoja nchini Afrika ambaye ameishauri Wizara husika ya kilimo katika nchi yake kwamba kilimo kinapaswa kufanywa kuwa sexy ili vijana wakivutie. Huwezi kuweka kitabu cha kilimo kina picha cha bibi mzee amechokaa kijijini always haiwezi kum-attract kijana kujiunga kwenye kilimo. Let make the agricultural sector sexy to attract youth. (Makofi)

MHE. GODWNI E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa.

SPIKA: Unapokea taarifa hiyo Mheshimiwa Godwin?

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, naomba niseme jambo moja niliwahi kupata fursa ya kwenda training ya quality ya infrastructure system kule Japan Tokyo. Nilipofika kule walikuwa wakisema wa Japan wale, wanaagiza chakula cha mwaka mzima kutoka nje ya nchi, ikiwemo nchi nyingi za Afrika, wanaitaja Zambia, wameitaja pia na Zimbabwe, why not Tanzania? Why not Tanzania hoja ndio kama hizi kwamba bado tuna changamoto kubwa hatujaweka mkazo mkubwa kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, itoshe tu kusema kwamba tukiweza kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo itatusaidia ku-export na faida kwenye uchumi uki-export sana halafu leo hii cha ajabu zaidi tuna ardhi ya kutosha, tuna yenye rutuba, lakini bado tunaagiza mazao yanayotokana na kilimo nje ya nchi kwa mfano suala la sukari, leo hii sukari unaagiza nchi ya nje kuliko Tanzania kweli?

Mheshimiwa Spika, mimi nataka kusema tu kwamba hasara tunayoipata Watanzania kwa kuagiza sukari na ngano, wachumi watanisaidia kwenye uchumi kuna terminology tunasema capital flight ambapo ni kitendo cha kukusanya fedha za ndani ya nchi kwenda kubadilisha na dola kununua bidhaa nje ya nchi. Definitely, tutapata inflation ambayo inasababishwa na capital flight lakini tukizalisha kwa wingi mazao ya kilimo tutakuwa na balance of payment na nchi yetu ita-invest na kuwekeza kwenye maendeleo mengine ya uchumi.

Mheshimiwa Spika, wakati wa kupitisha bajeti ya Mheshimiwa Waziri naomba mambo mawili; jambo la kwanza anieleze ni lini skimu yangu ya umwangiliaji Udagaji inakwenda kuendelea, maana mpaka sasa imetelekezwa na shilingi milioni 30 imepelekwa pale.

Mheshimiwa Spika, jambo la la pili Mheshimiwa Waziri au kaka yangu Mheshimiwa Bashe Naibu Waziri, baada ya Bunge hili kwisha niwaombe twende wote Jimbo la Mlimba mkaone utajiri wa Jimbo lile kwenye kilimo. Ahsante sana. (Makofi)