Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi na kwanza kabisa nimpongeze professor Waziri wa Kilimo, Naibu Waziri na timu yake na nawapongeza sana kwa sababu kwenye hotuba hii walau Kiteto imetajwa mara mbili tu, ukurasa wa 30 na ukurasa wa 127, lakini nawapongeza tena zaidi kwa sababu walau ninyi mmefuatilia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, na tunaka kila wizara tufuatilie Ilani hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukisoma Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ukurasa wa 42 tulijiwekea malengo ya kutengeneza tani laki 710 za alizeti, lakini kwenye hotuba hii nyinyi mmeweka tani milioni moja excellent tunataka tuwe na mwelekeo huu wa Ilani yetu. Lakini vilevile ukurasa wa 42 tulisema tutajenga maghala 14 kwenye mikoa hii ipo hapa excellent. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile tumesema kwenye ukurasa wa 43 tutawapatia vijana 400 kutoka mikoa tisa vifaa ipo kwenye hotuba yenu hapa safi sana. Lakini sasa nataka muongeze hivi vijana 400 mikoa tisa, kila mkoa tunataka mgawanye mlete mathematics ni vijana 44, na mkifika kwenye mikoa ile tunataka mtuambie mkoa ina wilaya ngapi na vijana wangapi watoke humo mimi nimeshapiga mahesabu nisipopata vijana sita kutoka Kiteto, Manyara mtakuja kutueleza mmefuata nini sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la umwagiliaji Kiteto ambayo nilikwisha kusema ni bread basket, kilimo cha mvua ni asilimia 99.9 kati ya hekta 1385 ambazo tumetenga kwa ajili ya umwagiliaji ni 0.00 percent ndio inatumika haiwezekani. Ni lazima tuwe wakweli kabisa tunaposema kilimo, kilimo inachangia pato la Taifa asilimia 29, 28 au 26 data zenu zote zinasema hivyo na inawaajiri watanzania asilimia 65 halafu tunapokuja kwenye bajeti tunawatengea bilioni 300, haifiki hata bilioni 300 honestly watafanya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Maputo declaration na Malaba declaration inasema nchi zime-commit kuongeza asilimia 10 kwenye agriculture, hii haifiki hata percent moja, hata hii program tunayosema tunafuatilia hii program ya kuendeleza kilimo ya pili ili-commit bilioni 13 kwa ajili ya kilimo we are not even one percent kwa hiyo, lazima tuwe serious tunapozungumzia agriculture. Imeajiriwa watanzania 65 pato la Taifa kubwa namna hiyo halafu tunawekeza sijui kwenye masekta gani huko tuwe serious kwa kweli tunapozungumzia agriculture. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na Ilani yetu imesema vilevile Chama Cha Mapinduzi tunataka kutoa wakulima kwenye jembe la mkono na kwenda kwenye matrekta, yamekuja matrekta hapa ya Urususi hapa wakulima wangu Kiteto wamechukua karibu matrekta 100, halafu mnawapeleka kwa Wizara ya Viwanda is a confusion yanatakiwa matrekta haya yawepo kwenye Wizara ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ili kwa sababu nyinyi mpo karibu na wakulima hawa halafu mnawaambia kwamba yale matrekta yale yalikuwa ya bei nafuu ni uongo mtupu, trekta bilioni 45, trekta milioni 55, sasa kuna unafuu gani hapo halafu mabovu kwanza, hebu tuwapatie wakulima matrekta haya wapate kuzalisha. Namshukuru sana waziri kwenye hotuba yako umewashukuru wakulima kwa sababu ni kweli, kilimo nchi hii ingekuwa wakulima wale hawalimi wala tusingekuwa na chakula. (Makofi)

SPIKA: Ahsante, Mheshimiwa Edward.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika baada ya hayo nashukuru naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)