Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie pia kwa maandishi mambo machache.

Mheshimiwa Spika, kwanza, hali ya mialo kwa upande wa Ziwa Nyasa si nzuri. Hakuna miundombinu ya barabara kiasi kwamba watu hulazimika kubeba mizigo mikubwa kichwani. Nashauri nanyi msaidie kusemea mnapokuwa na Wizara husika kama sehemu ya kuendeleza sekta hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali ifikishe umeme kwenye mialo. Pia kuwe na mpango maalum wa kutambua na kulinda maeneo ya mazalio ya samaki, yajengwe madogo kila mualo. Pia kuwe na utaratibu wa kutambua ujuzi wa wavuvi (RPL) ili kuwatia moyo kama ilivyo kwenye ujenzi, useremala na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya fukwe zina mmomonyoko mkubwa wa ardhi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mifugo; angalau kila kata kuwe na Afisa Mifugo mtaalam mmoja ili kuwashauri wafugaji pamoja na kutoa huduma za kitabibu hali ya sasa ni kuwa kila mfugaji atumie uzoefu wake.

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha matumizi ya Ranchi za Serikali wananchi wakatiwe vipande vya hekta 50 hadi 150, wakodishwe kwa bei ndogo lakini Serikali iendelee kumiliki asset yake ya ardhi kwani ni vigumu kupata tena maeneo makubwa kama hayo.