Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Watendaji Wakuu wa Wizara kwa kuandaa vizuri taarifa ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, napendekeza Serikali kuimarisha utafiti katika maeneo ya uvuvi ili kupata fursa ya kutumia vyema eneo la uvuvi wa bahari na maziwa makuu.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali kuimarisha miundombinu ya uvuvi; tatu, kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji wa viwanda vya minofu ya samaki na kuendelea kutafuta masoko ya bidhaa zinazotokana na samaki; nne, Serikali iendelee kutoa huduma bora kwa wadau wa sekta ya uvuvi ili kuwa na maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii; tano, Serikali iendelee kuwekeza katika maziwa makuu kwa kununua meli za uvuvi kama Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa na sita, Serikali kuweka mazingira mizuri, sera na kanuni ili kuendeleza ufugaji wenye tija.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali kuweka misingi rafiki ya wafugaji ili kuondoa migogoro iliyopo baina ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.