Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, muda ni mchache sana, lakini napenda kuchangia kwenye Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kwamba Tanzania tumebarikiwa madini ukiacha madini, kuna maliasili na utalii lakini kilimo kwa maana kilimo chenyewe, mifugo na uvuvi. Natambua kabisa Rais wetu Mama Samia amewachangua Waziri na Naibu Waziri strategically, Waziri anatoka kwenye jamii ya wafugaji na Naibu Waziri anatoka kwenye jamii ya uvuvi.

Kwa hiyo, tunatarajia kuona matokeo chanja na dhamira ya dhati ya mama alivyokuwa anahutubia Bunge hapa lime-reflect kwenye bajeti ya mwaka huu ambapo ametenga kweli fedha za maendeleo shilingi bilioni 99 sasa kutenga ni kitu kimoja na utekelezaji ni kitu kingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa bajeti umekuwa ukisausua mathalani mwaka 2016/2017 bajeti ilitengwa lakini zilienda asilimia 3.25 mwaka 2018/2019 bilioni nne lakini hawakwenda chochote kile na 2018/2019 ilienda asilimia 39 tu. Bajeti ya maendeleo ikitelezwa vizuri ina maana Wizara hii itaenda kufanya tafiti za kina kuweza kugundua fursa mbalimbali, kuweza kugundua mbegu mbadala matharani kwa kuwa na ufugaji wa tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yake najua Tanzania tuna ufugaji wa asili na huu wa ranchi ambao huu nao unasuasua, ufugaji wa asili wapo wale ambao wapo awalimi wanafuga tu na wengine tunalima na kufuga kwa maana ya agropastoral kama sisi hapa Wakurya tunafuga na kulima. Sasa mkiweza kugundua kwa kiwango kikubwa ambacho cha mifugo tulichonacho lakini tija ni ndogo sana na ukafanya tafiti ya kina kuweza kugundua tatizo ni nini, tutaenda mbali.

Mheshimiwa Spika, ufugaji na uvuvi ni sekta ambayo ikiwekezwa kwa kina kabisa tutaenda kupata pato kubwa sana Taifa na shilingi bilioni 23 kwa maana mifugo shilingi bilioni 10 na uvuvi shilingi bilioni 13 mmepeleka shilingi bilioni 11 tu. Lakini makusanyo ni shilingi bilioni 51; sasa mnakusanya shilingi shilingi bilioni 51 mnashindwa vipi kuwekeza shilingi bilioni 23 ili tija iongezeke maradufu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kama hata Kamati ilivyoshauri kwamba wadau mbalimbali wanalalamika kuwa sera, sheria na kanuni zimepitwa na wakati, ifanyike review twende na ufugaji wa kisasa. Hata kama Ranchi ya Taifa ambayo ni asilimia tano ya uwekezaji katika mifugo tuliyonayo nayo inasuasua yaani capacity ni ng’ombe 80,000 mpaka 90,000 mpaka sasa ranchi zetu za Taifa kulingana na takwimu zilizopo 12,000 na … ni bora tufanye ugawaji mzuri wa ardhi, tutafute na tuvutie wawekezaji, tutoke kuwekeza kwa government iende kwenye sekta binafsi. Wawekezaji waje wengi ili sasa hata tuweze kupata na masoko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwenye mazao ya mifugo, nyama tuna viwanda 25 lakini capacity yake ni kuweza kuchakata kilo 627,000. Lakini sasa hivi wanafanya under capacity, kilo 81,000 tu. Tatizo ni nini; labda teknolojia imepitwa na wakati, labda kuna factors nyingi, lakini tukiwekeza tukafanya tafiti tutagundua na tuweze kuwekeza kwa kina. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini hata tunapopeleka nje, yaani tuna-export tani 2,000 na tuna-import tani 2,000. Lakini tunazozi-export zinakuwa na bei ndogo kuliko zile ambazo tuna-import sisi, what is this? Tuangalie ubora wa nyama zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata ukija kwenye zao la ngozi utaona ngozi zetu za kondoo, ng’ombe, mbuzi, hazipati market huko nje na sababu ni nyingi. Tumesema hata upigaji chapa, maeneo ya machinjio, makaro yenyewe na kila kitu, ni wakati hata wa kuwekeza kuhakikisha kwamba walau katika kila Wilaya au Majimbo yanakuwa na machinjio ya kisasa kama ambavyo mmewekeza kule Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye maziwa sasa ndiyo unaweza ukalia, yaani hapa ninyi mna-document kwamba tunazalisha maziwa bilioni 2.7 kwa mwaka na target ni kufika bilioni nne, lakini uchakataji wa maziwa ambayo yanazalishwa ni two percent. Na mbaya zaidi kwa mfano mwaka 2018/2019 Serikali mmetoa vibali 417 vya kuingiza maziwa kutoka nje ambapo zilitumika zaidi ya bilioni 22 na kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi bilioni 22 na kitu zingetumika kuboresha viwanda vya Tanzania na kujenga viwanda vingine ili waweze kuchukua haya maziwa tungeweza kutoa fedha nyingi kwa hawa wafugaji na kutoa ajira nyingi hapa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mnada wa Magena kabla sijasahau; pale Magena tuna mnada wa kimkakati ambao ng’ombe wengi wamekwenda Kenya kutoka Mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara. Na tukifanya mnada ule wa Magena pale tutapunguza wizi wa mifugo kutoka pale Tarime.

Mheshimiwa Spika, wewe ni mwenyeji pale, unajua, ng’ombe wanatoka Rorya, Serengeti kuja pale wanakwenda Maabera, Kenya, lakini sasa hivi ukiuza ng’ombe kule unachukua hela za Kenya, inabidi ubadilishe upate hela za Tanzania. Lakini ukipeleka ng’ombe umetoka Simiyu au Mara kupeleka Kenya, ikifika jioni ng’ombe wa laki saba utauza laki tatu kwa sababu uko Kenya ili uweze kurudi Tanzania. Tunapoteza fedha nyingi sana za mapato. Tunaomba Serikali ifungue ule mnada wa Magena kwa maslahi mapana ya uchumi wa Wanatarime, Mara na Taifa kwa ujumla. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nitaandika mchango wa maandishi, muda ni mchache sana. Ahsante sana. (Makofi)