Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kunipa nafasi hii nami nichangie Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi, lakini kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ambayo wanafanya pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, leo nataka kuchangia tu mambo mawili katika Wizara hii ya Uvuvi. Hapa nyuma kidogo tumekuwa na wimbi kubwa la upungufu au uhaba wa samaki viwandani, leo nataka niishauri Wizara jambo mojawapo ambalo linalosababisha kuwa na uhaba wa samaki katika viwanda vyetu.

Mheshimiwa Spika, ijulikane ya kwamba tuna samaki aina ya sangara hasa kwenye Ziwa letu la Victoria na samaki huyu kwa kilo moja anauzwa shilingi 9,000 mpaka shilingi 10,000 pale Mwaloni. Sasa chukulia samaki wa kilo tano kwa shilingi 9,000 atauzwa shilingi 45,000; lakini ijulikane ya kwamba bondo ndani ya ile samaki ndio lenye samani kubwa kuliko mnofu. Sasa wanapokuwa wanauza pamoja na bondo lake kwa shilingi 9,000 na akipeleka kiwandani atauza kilo moja kwa shilingi 12,000 ina maana kwa samaki mwenye kilo tano atamuuza shilingi 60,000; lakini bondo linauzwa zaidi ya shilingi 60,000 samaki mwenye kilo tano.

Mheshimiwa Spika, sasa mvuvi amekuja na option ambayo ni ya kawaida tu kwamba badala ya kumpeleka yule samaki kiwandani bora mnofu wake awauzie wananchi halafu yeye anufaike na lile bondo. Anajikuta kwa wananchi anaweza kumuuza yule samaki wa kilo tano mpaka shilingi 40,000 mpaka shilingi 50,000 na bondo pia akauza kwa shilingi 50,000.

Mheshimiwa Spika, hapo atajikuta ameingiza shilingi laki moja kwa samaki mwenye kilo tano, lakini atakapompeleka kiwandani atamuuza kwa bondo lake kwa shilingi 60,000 hata ningekuwa mimi nisingeweza kupeleka samaki yule kiwanda.

Sasa mimi niishauri Wizara, waruhusiwe wavuvi au wafanyabishara ambao wanapeleka samaki kiwandani basi kuwepo na thamani ya mnofu na thamani ya bondo liuzwe peke yake, hii itasababisha kunufaisha huyu mvuvi kwa sababu thamani ya samaki itaongezeka, na kama hazitafanya hivi maana yake wataendelea hao wavuvi kutaka samaki vipande vidogo vidogo, wanawauzia wananchi na viwanda nyetu vitaendele kuwa na uhaba kama ambavyo imeonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia ijulikane ya kwamba matumizi ya ndani yameongezeka ya watumia samaki kama kitoweo hata marafiki zangu hapa Wagogo wanataka samaki kutoka Ziwa Victoria kule Usukumani, sasa ni lazima tu viwanda vikose samaki. Kwa hiyo mimi niishauri Wizara kwamba pia lazima tujikite sana kwenye mabwawa ili tuendelee kupata samaki wengi na hawa samaki waweze kutumika katika matumizi yale ya kawaida ya ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia kupunguza ukiritimba hawa wawekezaji wanapokuja kwa ajili ya vizimba, ukija na kizimba utapewa masharti makubwa, tafute eneo kijijini, nenda katafute kibali, lete mtu wa TAFIRI aje apime, huu mlolongo unasababisha wawekezaji wanaondoka; nilitamani sana Wizara iliangalie hili ili mwisho wa siku tuwe na malighafi ya kutosha kwenye viwanda vyetu.

Mheshimiwa Spika, lakini suala lingine ambalo nilitaka kushauri ni tozo kwa wavuvi; kuna tozo nyingi hapa kwa wavuvi kuna tozo inayotozwa na TASAC ambao wanakuja kukagua ubora wa mtumbwi wanatoza shilingi 70,000.

Mheshimiwa Waziri umefika pale kwangu ulikuja wananchi walikulalamikia na ulisema utalishulikia hili lakini bado halijashughulikiwa bado wanatoza shilingi 70,000 kukagua ubora wa mtumbwi. Sasa hapa wananchi wangu wameniuliza swali ndogo sana kama leo mtumbwi ni mpya unakuja kukaguliwa nalipa shilingi 70,000 wakati ni mpya wala haujatumika, sasa wanakagua ubora upi wakati bado ni mpya.

Mheshimiwa Spika, hili swali ni very technque kidogo, mimi niishauri Wizara kwamba wananchi wetu hawajakataa kulipa, lakini wanaona shilingi 70,000 ni kiwango kikubwa sana ukilinganisha na kazi ambayo inakuja kufanyika. Kwa hiyo niiombe Wizara iweze kuliangalia hili.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna tozo kama leseni ya mtumbwi inayotozwa na halmashauri shilingi 30,000 lakini pia kuna leseni kwa mvuvi mmojammoja shilingi 20,000 hapa pia na penyewe nilitamani sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika naunga mkono hoja, lakini tuangalie bei ya samaki ukilinganisha na bondo. Ahsante sana. (Makofi)