Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia kwenye sekta hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, sekta hii ninaweza kuzungumzia kwa wavuvi wadogo wadogo. Kwenye Jimbo la Kawe ninapotoka wavuvi wadogo wadogo wapo kwenye kata ya Kunduchi na Kata ya Mbweni, lakini wanachangamoto, changamoto yao kubwa ni Sheria ya Uvuvi ambayo inawabana. Wavuvi hawa wanatakiwa wakiingia majini waingie mita 50, mita 50 kwenye kina ni unatoka Kunduchi una fika Unguja ndiyo unakuta hichi kina. Kwa hiyo, wanapata hii changamoto, lakini wana miundombinu hafifu, wanakuwa na bodi, zile boti engine yake ndiyo unashikia mkononi. Kwa hiyo, mawimbi yakimkuta katika ya bahari anazama na kupoteza maisha tuiangalie hii.

Mheshimiwa Spika, lakini pia ushirikishwaji katika utungaji wa sheria tunaomba wavuvi hawa wadogo wadogo washirikishwe kwa sababu kwenye taarifa zetu, wavuvi wadogo wadogo wanachangia asilimia 98 ya pato la sekta hii, kwa hiyo, tuwaangalie kwa uwangalifu mkubwa.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, changamoto zote wavuvi hawa wameweza kuvuna wastani wa tani 350 za samaki kwa mwaka hichi ni kiwango kidogo ukilinganisha na jinsi gani tulivyo na maeneo yetu, hiki ni kiwango kidogo na kwa sababu ni kiwango kidogo samaki hawatoshelezi kwa soko la ndani. Imelazimisha Serikali kuagiza samaki kutoka nje, samaki zinaagizwa tani 24 kutoka nje ambapo ni sawa na dola za Kimarekani milioni 25 uki-calculate kwa pesa ya Tanzania ni shilingi bilioni 690,000 kwa mwaka. Pesa hii ni nyingi na inakwenda nje kwa sababu sisi hatuna nyenzo za kutosha kusaidia wavuvi wetu wadogo wadogo.

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali yangu kwa sababu naona Waheshimiwa Mawaziri ni wasikivu na wanachukua kwa sababu tunapokwenda ni kuzuri, walikuwa wanalalamika nyavu zinachomwa lakini sasa hivi elimu naona inafika na nyavu hazichomwi na sasa hizi milimita 16 imeshaeleweka kwa wavuvi. Kwa hilo, nawapongeza.

Mheshimiwa Spika, lakini nishauri pia tujue idadi halisi ya wavuvi wetu hili tuweze kuwasaidia wavuvi, wanalalamika hawasaidiki kwa sababu hawakopesheki, hatujui hata idadi yao, hatuna jinsi ya kuwasaidia kuweza kupata nyenzo nzuri na thabiti za kuweza kuingia majini.

Niombe Mheshimiwa Waziri unapokuja ku-wind up uweke vitu muhimu na facilities ambazo zitasaidia hawa wavuvi waweze kuingia kwenye deep sea bila ya kupoteza maisha.

Mheshimiwa Spika, lakini niombe kwa sababu sekta hii ni muhimu sana, tunaweza kutanua wigo, tutanue wigo wa wawekezaji; wenzangu wamesema tutanue wigo kama tunaona tunafika hapa tunaweza kupiga hatua 100 mbele, tutanue wigo, tutafute wawekezaji waweze kuwekeza kwenye hii sekta, tuna utajirisho wa kutosha. Tukiweza kuweza vya kutosha sekta hii inaweza kuwa ya kwanza kwa kuingiza pato la Taifa. Inaweza kuwa ya kwanza kuajiri vijana wetu. Niki-refer kule nyuma kwenye Mpango wetu wa Pili wa maendelea tuli-target mpaka mwaka 2020 asilimia 4.6 ichangie pato la Taifa sekta hii kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, lakini hatukufika kwa sababu hatuna nyezo kwa hiyo hatuna nyenzo, mafunzo na hatuna vifaa muhimu, lakini mpaka 2019/2020 ni asilimia 24 tu ilitengwa katika sekta hii ya uvuvi. Kwa hiyo twende tukapitishe bajeti na itekelezwe ili tuweze kwenda kusaidia watu wetu sekta hii imeajiri vijana, vijana wengi wamekwenda hawana elimu, wapate elimu ya kutosha, lakini tutapata pato la Taifa, tutapata ajira za kutosha, tutapata mapato ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa sababu muda ni mchache, nashukuru sana. (Makofi)