Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MPAKATE D. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hotuba ya Viwanda na Biashara kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani inatakiwa ifanyiwe marekebisho kutokana na upungufu, kwani ilishindwa kumfidia mkulima pindi mzigo wake ulivyopotea katika maghala makuu. Mzigo ukipotea ghala kuu sheria inamtaka mtunza ghala amfidie mweka mali, lakini sheria haimlazimishi kulipa, matokeo yake mweka mali anakuwa anadai mali zake bila mafanikio. Hivyo ninaomba sheria hii irekebishwe ili itoe msisitizo wa mtunza ghala kulipa mara moja pindi akipoteza mzigo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tozo nyingi sana zinazotolewa na Serikali pamoja na Halmashauri bila kumfahamisha tozo hizo wakati mfanyabiashara anapata leseni ya biashara. Ni vyema mfanyabishara apewe orodha ya tozo zote anazopaswa kulipa wakati anapewa leseni ya biashara. Kuna ule ushuru wa vipimo, kodi ya majengo, ushuru wa mazingira, tozo mbalimbali kama EWURA, Halmashauri na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kuna ukiritimba wa kupata vibali mbalimbali. Ni vyema mfanyabiashara akahudumia sehemu moja ili kuharakisha uwekezaji wa wafanyabiashara. Kwa mfano, vibali vya ujenzi, vibali vya mazingira, vibali vya Taasisi mbalimbali kama EWURA na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vingi vimebinafsishwa, lakini wafanyabiashara wamebadili matumizi ya viwanda hivyo bila kujali kuwa viwanda hivyo vilijengwa kwa madhumuni fulani ili kuwezesha mazao yetu kuongeza thamani. Ni vyema viwanda hivyo vifufuliwe kama ilivyokusudiwa ili kuongeza ajira kwa vijana wetu. Tuna malighafi nyingi sana tunazalisha, lakini tunauza ghafi badala ya kuongeza thamani ya mazao hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna ucheleweshaji wa huduma mbalimbali katika vitengo vilivyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara ikiwa ni pamoja na kufumbia macho sekta ndogo ya biashara ndogo ndogo (Wamachinga) ambao wanaendesha biashara bila utaratibu maalum ambao ungewezesha kundi ili kuwa na leseni za biashara na kuiongezea mapato Serikali kupitia leseni hizo.