Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza na mimi napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu kwa heshima na dhamana kubwa ambayo amenipatia ya kuwatumikia Watanzania katika nafasi ya Waziri wa Fedha na Mipango. Napenda kumuahidi na kupitia Bunge hili kuwaahidi Watanzania wote kwamba nitaitumikia nchi yangu kwa uwezo wangu wote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilisikiliza hotuba ya Mheshimiwa Rais, nimeisoma na naomba kwanza niseme mambo matano kwa faida ya Watanzania ambao hawajaisoma hii hotuba na wengine pengine hawakuisikiliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, kwamba Tanzania mpya itajengwa na sisi Watanzania wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kila Mtanzania ni lazima afanye kazi kwa bidii na kujituma (selflessness) na hili ndilo linatuwezesha kugeuza maisha ya dhiki kuwa kama Mbinguni, yaani change of hell into paradise, lakini ni lazima tujitume, tutoke jasho ili kukuza uchumi wa Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, rushwa, ufisadi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya mali na rasilimali zote za umma ni lazima tuvipige vita kwa nguvu zetu zote bila kuoneana haya. Kwa nafasi ambayo Mheshimiwa Rais amenitunukia, ni lazima mapato ya ndani ya kodi na yasiyo ya kodi, ni lazima yakusanywe kikamilifu kwa mujibu wa sheria. Hatutawachekea wakwepa kodi wala watumishi wa Mamlaka ya Ukusanyaji Mapato (TRA), wala Wizara na Idara za Serikali zinazokusanya maduhuli.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwetu sisi kama Wizara ya Fedha na Mipango, hawa ni nyoka, ni sawa na kucheza na cobra. Hatutakubali, tunawathamini sana wafanyabiashara wakubwa kwa wadogo, lakini watii Sheria za Kodi na sheria nyingine za nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la nne, ni lazima kuwa na hofu ya Mungu katika kuwatumikia wananchi. Ni lazima tuwe na uchungu na maisha duni ya Watanzania walio wengi vijijini na mijini. Hawa hawana uhakika wa chakula, wanakula mchunga ndiyo mboga yao bila fursa ya kuchagua; wanakunywa maji yasiyo salama, watoto wao wanakaa chini shuleni na kadhalika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la tano, amani na mshikamano katika nchi yetu, hii ni nguzo kuu ya maendeleo na ni lazima ilindwe kwa nguvu zote. Hivyo ni lazima kuzuia na kuzima ninachoita chaos of democracy kama tukio la jana na leo asubuhi hapa Bungeni. This is true costly to our country and we cannot afford it. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nisemee hoja mbili, tatu, nyingine nitazieleza kwa ufasaha zaidi wakati tunajadili Mpango kuanzia kesho. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ujenzi wa reli mpya ya kati kwa kiwango cha standard gauge, natambua Watanzania wana kiu kubwa sana ya kuwa na reli ya kisasa, lakini ni ukweli pia kwamba haitawezekana kujenga reli hiyo kwa Bajeti ya Serikali. Inakadiriwa ujenzi wa reli hiyo utagharimu kati ya dola za Kimarekani bilioni sita mpaka saba ambayo ni sawa na shilingi za Kitanzania trilioni 13.15 mpaka trilioni 15. Ni fedha nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Ununuzi wa Umma, niwataarifu kwamba Wizara iko katika hatua ya mwisho wa kuandaa marekebisho ya sheria hiyo na tutaileta for first reading nafasi ikipatikana ndani ya Mkutano huu wa Bunge. (Makofi)
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, nawaomba Watanzania wote wamuunge mkono kwa vitendo vya dhati Mheshimiwa Rais wetu na viongozi wasaidizi wake waandamizi kujenga Tanzania mpya. Tunaiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais kwa asilimia 200 na tunawaahidi Watanzania usimamizi mahiri kwa bajeti ya Serikali na maendeleo ya uchumi wa Taifa letu kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)