Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ya Viwanda haiko kama Serikali haitakuwa na malengo makini kwa Watanzania. Kwanza, Serikali ijikite kwa kutoa vipaumbele ni viwanda vipi kwanza waanze navyo. Serikali ijali wawekezaji wa ndani wanapowekeza kwenye viwanda na iondoe sheria kandamizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuwe na miundombinu mizuri kama ya barabara bora zenye viwango, ambazo zitaruhusu bidhaa kusafirishwa kwa urahisi zaidi. Kuwe na uhakika wa umeme na siyo wa mafuta. Kwa upande wa biashara, wafanyabiashara wapunguziwe riba kwenye mabenki ili kwe na urahisi wa kufanya biashara na Watanzania wengi wawekeze kwenye biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wageni wakiwekeza kuwe na asilimia ya kuajiri Watanzania isiyopungua asilimia 90. Pia kuwe na masharti ya uwekezaji kuwa wanapowekeza, waboreshewe miundombinu katika eneo walilowekeza. Vilevile Serikali ifanye jitihada za makusudi za kupanua wigo na
fursa za kuanzisha masoko yenye masharti nafuu. Serikali ijifunze kutoka nchi nyingine vipi wamefanikiwa katika biashara na viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri tuweze kuendeleza viwanda vidogo vidogo kama SIDO na vinginevyo ili wananchi wapate ajira na kuwe na soko la karibu na uhakika ili kuuza bidhaa zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania wanahitaji Serikali iimarishe viwanda ambavyo kwa kuanzia vitaleta tija na kuendelea kama walivyoendelea nchi za jirani na za mbali na siyo kila siku hadithi. Wanatarajia kuona Tanzania ya viwanda vyenye neema mbalimbali na imeondokana na umasikini ulioenea. Pia Serikali itatue changamoto zilizopo katika sekta hii ili tufikie malengo tunayotarajia.