Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Waziri na Naibu wa Wizara hii kwa kazi nzuri na ubunifu mkubwa kwenye kutatua matatizo ya migogoro ya ardhi. Ninapongeza pia Katibu Mkuu pamoja na uongozi mzima wa Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Wilaya ya Moshi Vijijini, hususan Mji Mdogo wa Himo, kumekuwepo na migogoro mingi inayosababishwa na Maafisa Ardhi kufanya double allocation kwa nia ya kujipatia rushwa. Aidha, wafanyabiashara wachache wamejirundikia maeneo makubwa na mji ni kama vile umekuwa mali ya matajiri wachache. Tunaomba Wizara iingilie kati na kugawa maeneo yaliyohodhiwa bila kuendelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa kwenye Wizara ni ucheleweshaji wa vibali vya kujenga, pamoja na utoaji wa electronic titles jambo ambalo tuliahidiwa lingefanyika kwa haraka, inachukua muda mrefu na ingekuwa vizuri kuchapisha kwenye vyombo vya habari titles ambazo ziko tayari.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna umuhimu wa kutenga maeneo ya kilimo kwenye kila Halmashauri kwa wawekezaji wakubwa.