Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Waziri alitoa maelekezo kwa barua ya tarehe 18.12.2018 kufanya marekebisho ya mpaka kati ya Wilaya ya Ubungo na Wilaya ya Kisarawe. Kazi ilianza tarehe 10.01.2019; walipitia GN Na. 41 ya tarehe 15.02.1974 na ramani yake Na. E1/341/254 iliyosajiliwa kwa Na. 43075 inayoonesha Hospitali ya Mloganzila.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa maelekezo umefanyika kikamilifu, aidha, mapendekezo na ushauri umetolewa ipasavyo. Taarifa hii imewasilishwa kwenye ofisi za Mheshimiwa Waziri kwa ajili ya kutoa GN mpya na mpaka sasa bado utekelezaji haujafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri ukifika kwenye majumuisho uweze kutuambia juu ya hitimisho ya suala hili ili wananchi wa maeneo haya waweze kupata huduma zinazostahili kwa mamlaka sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.