Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kusimamia na kutatua migogoro mingi ya ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza pia Waziri wa Ardhi, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara kwa kuandaa mpango mzuri wa mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi kwa mwaka 2021/2022.

Katika kuzingatia utekelezaji wa mipango hiyo napendekeza kama ifuatavyo; kwanza kusimamia na kuhakikisha kuwa sehemu kubwa ya ardhi ipimwe kwa kuwa kasi ya ukuaji wa miji ni kubwa.

Pili, kuhakikisha ankara za malipo ya kodi za ardhi zinatolewa kupitia simu za wateja n atatu, kuhakikisha hati za kumiliki ardhi zinatolewa kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, nne, Serikali kuendelea kutatua na kumaliza migogoro ya ardhi; tano, Serikali kuongeza wafanyakazi hasa katika kitengo cha mipango miji na Upimaji wa ardhi; sita, Serikali kuhakikisha vitendea kazi kama vifaa vya kupimia, magari na pikipiki vinanunuliwa na saba, Serikali ihakikishe Mabaraza ya Ardhi yanakuwepo katika kila Wilaya na kuhakikisha haki inatendeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nane, Serikali kupitia Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji kuhakikisha miundombinu ya barabara, umeme na maji inafikishwa katika maeneo yaliyopimwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naunga mkono hoja.