Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara kwa utekelezaji wa majukumu yao kwa kiwango. Mchango wangu utajikita katika sehemu zifuatazo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, sekta ya masoko. Wakulima wa mazao ya nafaka wanakabiliwa na changamoto kubwa ya masoko ya uhakika kwa mazao mfano soko la mpunga na mahindi kila mwaka yanakabiliwa na kutokuwa na soko la uhakika. Nashauri Serikali kupitia Wizara ichukue hatua katika kutafuta masoko ya mazao haya katika nchi jirani kama Sudan ya Kusini, Kenya, Zambia na nchi jirani ambazo zina uhaba wa mazao haya badala ya wafanyabiashara binafsi kusimamia na utafutaji wa masoko kwa mazao hayo makuu ya nafaka. Aidha, Serikali kwa kupitia vyombo vya habari watangaze taarifa za masoko kwa wakulima ili wawe na uwezo katika kujadili (debate) vyema bei inayolipa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kuhusu Bodi ya Leseni za Maghala. Naipongeza Wizara kwa mpango wake katika kuboresha na kuongeza wigo wa mkopo kwa wakulima vijijini ili kuongeza bidhaa za kilimo. Kwa kuwa Mkoa wa Morogoro ni ghala ya chakula la Taifa na moja ya Mikoa yenye viwanda vingi, naishauri Wizara ianzishe Ofisi ya Leseni ya Kodi za Maghala katika mkoa wa Morogoro ili kusogeza huduma zaidi na karibu ya wakulima ili kuongeza uwezo wao wa kuzalisha mazao kwa wingi/ufanisi kwa kuwezesha Mkoa wa Morogoro kutekeleza majukumu yake kiukamilifu kuwa ghala la chakula la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.