Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na kumpongeza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji na watendaji wake kwa kuwasilisha hotuba ya bajeti yao hapa Bungeni ili tuweze kuijadili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo ambayo nilikuwa napenda kupatiwa ufafanuzi na kutoa ushauri kwa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, viwanda vilivyobinafsishwa. Serikali iliamua kubinafsihsa viwanda vilivyokuwa vya Serikali na kubinafsishwa kwa wawekezaji lakini bado tunaona licha ya kuwa viwanda hivyo havifanyi kazi lakini vingine vimebadilishwa hata matumizi na vingine vimegeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa au mazao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mpango mkakati gani kwa sababu awamu hii Serikali ina mpango wa kufufua viwanda na ningependa kujua hatua gani watachukuliwa wawekezaji hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ningependa kujua katika ujenzi wa viwanda je, itazingatia katika maeneo yenye malighafi ili kupunguza gharama za kusafirisha malighafi kutoka zinakopatikana mpaka viwandani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wetu wa Iringa hasa katika Jimbo la Kilolo asilimia kubwa kuna kilimo cha nyanya, pilipili na vitunguu, lakini wakulima wamekuwa wakipata shida sana kupata masoko kwa kuwa Serikali inahimiza ujenzi wa viwanda na kuna eneo la EPZ je, mkakati wowote umewekwa na Serikali ili kupata mwekezaji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, maeneo yaliyoteuliwa na EPZ. Kwa kuwa Serikali ilitenga maeneo mengi sana kwa ajili ya uwekezaji katika viwanda lakini maeneo mengi bado wananchi hawajalipwa fidia likiwemo lililotengwa katika Mkoa wetu wa Iringa. Nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wananchi wanalipwa ili maeneo hayo yaweze kutumika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ubovu wa barabara zinazokwenda katika viwanda. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha barabara zote zinazokwenda katika viwanda zinajengwa kwa kiwango cha lami na barabara hizo zinahamishwa kutoka kuwa za Halmashauri na zinakuwa za TANROAD.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.