Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. HAMIS A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa leo ni mara yangu ya kwanza kuzungumza katika Bunge lako Tukufu, toka tumalize miaka mitano iliyopita ambayo pia nilipata heshima ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini, naomba nianze hotuba yangu kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai. Pili kwa kuwashukuru wanachama wenzangu wa Chama cha Mapinduzi wa Jimbo la Nzega Vijijini na wananchi wenzangu wote wa Jimbo la Nzega Vijijini kwa kunipa heshima ya kuwa Mbunge wao kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Mheshimiwa Spika, pili nikushukuru wewe mwenyewe kwa kunipa fursa ya kuzungumza katika hoja hii ya Waziri wa Kilimo siku hii ya leo. Jambo la kwanza ambalo napenda kulizungumzia linahusiana moja kwa moja na uelekeo wa kilimo cha umwagiliaji kwenye Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla wake limejaliwa kuwa na bahati ya kuwa na maji mengi ya baridi, siyo maji ya chumvi. Ukienda katika nchi ya Israel utakuta kule wanafanya treatment ya maji ya chumvi kuyafanya yawe ya baridi ili waweze kumwagilia, lakini sisi hatuna haya ya kufanya hivyo katika mito mirefu na maziwa makubwa duniani, 10 bora duniani, Tanzania imeajliwa kuwa nayo sita. Kwa hiyo, katika vyanzo vya maji baridi Tanzania tuna mtaji mkubwa ukilinganisha na nchi zote ambazo zinatuzunguka na hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nalisema hili kwa sababu naamini tunapoelekea tutashuhudia zaidi vita nyingi zikisababishwa na ukosefu wa maji baridi kuliko vita hizi za mafuta na gesi ambazo tumezishuhudia katika kipindi tulichopita, wanaziita water wars. Sasa ili tusiende huko, lakini pia tuweze kuitumia resource ya maji ambayo tumejaliwa by virtual of being Tanzanians na kuwa na hii land scape nzuri ni lazima kwanza tujipange kuhifadhi vyanzo vya maji hususani maji baridi.

Mheshimiwa Spika, la pili, ni lazima tupange kufanya matumizi endelevu na yenye faida kwa vizazi na vizazi vya nchi yetu. Sababu kubwa ni moja, leo hii tunawekeza kwenye kilimo, watu wetu tunawahamasisha walime ambao ni zaidi ya asilimia 70, lakini mwisho wa siku hatupati yield ya kutosha kwa ajili ya ku-sustained chakula cha ndani, lakini pia kwa ajili ya kuuza nje, wakati tuna vyanzo vya maji baridi vya kutosha kuliko nchi zote zinazotuzunguka hapa jirani.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo nataka niishauri Serikali kwamba katika Awamu hii ya Tano iliyopita na sasa tumeingia ya Sita, bahati nzuri Rais aliyeko sasa alikuwa sehemu ya Awamu ya Tano, imefanyika miradi kabambe mikubwa ya kihistoria ambayo inaweka legacy ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kiasi kikubwa sana. Napenda kuishauri Serikali iwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji kama legacy ya Serikali ya Awamu ya Sita, tutoke kwenye kilimo cha kutegemea mvua, kwa sababu kilimo cha kutegemea mvua kimesha-prove kwamba hakiwezi kutupeleka popote.

Mheshimiwa Spika, wakati sisi tunazaliwa na kukua pale Nzega, kiwango cha mvua kilikuwa kinazidi milimita za ujazo 2,000. Leo hii kiwango cha mvua kipo kati ya milimita za ujazo 600 mpaka 900. Ni kiwango ambacho hakiwezi kuivisha mazao ya mahindi mpaka kufikia mwisho na kuvuna. Kwa maana hiyo wananchi wetu ambao walizoea kulima kilimo cha kutegemea mvua wanalima mahindi leo hii wakiendelea na utaratibu huo wa kulima mahindi, hawawezi kuvuna. kwa hiyo, ni lazima sasa tubadilishe utaratibu, twende kwenye kilimo cha umwagiliaji na cha uhakika Zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nazungumzia huu unapaswa kuwa ni mradi kabambe ambao utaweka legacy ya Serikali ya Mheshimiwa Mama Suluhu Hassan ya Awamu ya Sita ni kwa sababu, vyanzo vya maji tulivyonavyo; Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa, Ziwa Victoria na mito yote ambayo inatengeneza haya maziwa na inayoingia baharini, kama tukitumia ipasavyo na tukitumia mabonde tuliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu tunaweza kuwa godown la chakula la Ukanda huu wa Afrika na hata kupeleka nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wazo langu ni kwamba, leo hii tunajadili sana, kila Mbunge akisimama anazungumza naomba maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, kuna baadhi ya vijiji havina maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Kwa nini tusiwe hapa Bungeni Wabunge tunajadili kuletewa maji kwa ajili ya umwagiliaji, kwamba tujenge mabomba makubwa ambayo mtu mrefu kama mimi naweza nikatembea ndani yake kutoka Ziwa Victoria, kutoka Ziwa Tanganyika, kutoka Ziwa Nyasa tuyatawanye mpaka huku Dodoma, Dodoma kuna ardhi nzuri, lakini hakuna maji, mvua ni chache. Kama tukileta maji kutoka Ziwa Victoria ama maji kutoka Ziwa Tanganyika maana yake yatapita mikoa yote ya huko Magharibi mpaka kufika hapa Dodoma na tutamwagilia na tutalima kwa uhakika, hata wale wafugaji wanaohamahama hawatakuwa na haja ya kuhama kwenda maeneo mengine ambayo yana vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wazo hili linaweza kuonekana ni wazo gumu kutekelezeka, lakini ni wazo ambalo linawezekana. Kama Israel leo hii wana-treat maji chumvi kuyapeleka kuwa maji baridi ili wafanye kilimo cha umwagiliaji kwenye nchi ambayo ni kame, kwa nini sisi tushindwe kutumia maji baridi ambayo tayari tunayo, arable land ambayo tunayo, tunakwama wapi?

Mheshimiwa Spika, mfano kule kwetu, kuna bonde maarufu sana linaitwa Bonde la Isagee, nimeona Wizara wanatujengea pale godown, kijijini kwangu Puge, ulipita pale na lile godown likijengwa pale maana yake liko kwenye catchment area ya walimaji wazuri wa nafaka ikiwemo mpunga na mahindi. Hata hivyo, kilimo kinachofanyika pale kwa kiasi kikubwa kinatoka kwenye hili bonde la Isegenhe kwa nini bonde kama lile lisipate maji ya uhakika kutoka kwenye mito na maziwa ya maji baridi ambayo yanatuzunguka hakuna sababu kwa niniā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. DKT. HAMIS A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.