Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sikusimama Bungeni kutoa mchango wangu wa kawaida naomba nichagie kidogo kwa maandishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na kumpongeza Mheshimiwa Waziri Engineer Elias Kwandikwa, Katibu Mkuu na watendaji wote Wizarani pamoja na Mkuu wa Majeshi (CDF) pamoja majeshi yetu kwa kazi nzuri wanazofanya za ulinzi wa Taifa letu, lakini pamoja na majukumu mengine wanayoagizwa na Amiri Jeshi Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jeshi letu linafanya vizuri sana na linasifika hata nje ya mipaka yetu. Waheshimiwa Wabunge wenzangu wamechangia mengi mazuri kuhusu bajeti iliyoletwa kwetu na mimi naomba nichangie jambo moja tu ambalo naliona ni la muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kawaida wanajeshi wanatekeleza majukumu yao kwa amri na amri zote ni halali. Ni kwa ajili hiyo mataifa mengine mengi yanatumia majeshi yao kama nyumba ya kufanyia tafiti za kisayansi kwa sababu ya nidhamu ya kijeshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nchi yetu nayo ni sehemu ya dunia ya leo ya ki-TEHAMA, nashauri Serikali iangalie ni namna gani tunaweza kutumia majeshi yetu kama nyumba ya kufanyia tafiti za kisayansi (atomic, molecular, medical etc) na hata ujenzi wa viwanda vya kutengeneza magari ya kisasa na vifaa tiba na vya kijeshi pamoja na vifaa vya ujenzi wa miundombinu. Hili linaweza kufanyika kwa kutenga fedha na kuchukua vijana wetu wenye vipaji maalum watunzwe na kuhakikishiwa maisha mazuri na kutengenezewa maabara za kisasa kwa ajili ya tafiti ambazo tunazihitaji kitaifa kwa ajili ya maendeleo ya kisayansi.