Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza Serikali kuweka mazingira mazuri ya kufanyia kazi kwa wanajeshi kama kujenga nyumba za kuishi pamoja na kununua vitendea kazi kama magari na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ihakikishe JKT inawezeshwa ili kuzalisha chakula cha kutosha kwa matumizi na biashara. Pia Serikali kuendelea kulisimamia Shirika la SUMA JKT kuendeleza viwanda na ujenzi wa majengo mbalimbali ya Serikali kuongeza mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kusimamia na kuondoa migogoro ya ardhi na mipaka baina ya Jeshi letu la wananchi pamoja na wananchi wanaoishi jirani na kambi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Waziri na Naibu Waziri na Makatibu Wakuu pamoja na Mkuu wa Majeshi kwa utendaji kazi wenye weledi kwa kuimarisha ulinzi nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.