Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi kwanza napenda Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na sisi wote kuwa hai kwa siku hii ya leo. (Makofi)

Napenda pia kumpaongeza Rais wetu mpenzi Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na timu yake yote. Pia napongeza Waziri wa Ulinzi kwa hotuba yake nzuri ambayo ametusomea leo asubuhi, kwa kweli imeshiba, inapendeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni mwenyeji wa Mkoa wa Lindi, kule kwetu Lindi na Mtwara tupo mpakani kabisa, mwaka jana kuanzia mwezi wa sita/wa saba mpaka kumi kidogo tuliishi kwa mashaka. Watu walikuwa hawawzi kufanya kazi zao, kazi kubwa ambayo inafanywa na wakazi wa Mkoa wa Lindi na Mtwara ni uvuvi na kilimo. Kipindi kile watu walikuwa wanashindwa kwenda mashambani kwao kwa sababu kuna watu waliingia ambao sio watu wazuri kutoka kwenye nchi za wenzetu japokuwa siwezi nikasema ni nchi gani, lakini inaonekana kuna watu waliingia wakawa wanafanya matendo ambayo hayafurahishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nashukuru sana nilipongeze Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania walichukua jitihada za haraka wakatuma vikosi vya Jeshi kwenye mipaka ile na ulinzi uliimarishwa, hatimaye hali ikarejea vizuri sana kwa kweli tunawapongeza sana tunasema ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Lindi na Mtwara kwa sasa wanaamani wanaendelea na kufanya kazi zao na tunaona bajeti iliyowekwa hapa tunaomba ipitishwe tu kwakweli tusishike shilingi ipitishwe vizuri kwa sababu wanaonesha wanania ya kulinda mipaka na walilinda mipaka ipasavyo, tunaomba bajeti yao iende vizuri ili kazi iendelee kusiwe na mkwamo wowote wa ulinzi na usalama wa mipaka yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo napenda kuliongelea ni suala la nyumba za wanajeshi, katika Wilaya ya Nachingwea kuna kikosi cha Jeshi kinaitwa Majimaji na Old Camp, nyumba zilizopo pale ukiziona kwa kweli zinakatisha tamaa na ukiambiwa wanaishi watu/wanajeshi kwa kweli inatisha. Ombi langu kwa Serikali kwa Wizara ya Ulinzi mfanye marekebisho ya zile nyumba ili watu wanaoishi mle wajisikie ni watu kama watu wengine wanaishi vizuri, zile nyumba zimechoka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi lingine nililonalo kwa Wizara ya Ulinzi ni ofisi zao, nimeshaingia kwenye ofisi zao mara nyingi hata pale Kikosi cha Mgulani ofisi zao kwa kweli haziko vizuri. Tunaomba Waziri wa Ulinzi ulichukuwe hilo ujaribu kuangalia kuboresha ofisi za jeshi kwa sababu zile ni ofisi kama zilivyo ofisi nyingine, tunaomba uboreshe ziwe vizuri ili na wao wafanye kazi vizuri, wajisikie wanapotimiza majukumu yao ya kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine napenda kuliongelea ni kuhusu barabara za mipakani. Wabunge wengi wameongelea hizo barabara, tunashukuru Serikali yetu kupitia Wizara ya Ujenzi wamejitahidi kutengeneza barabara hizo. Ila tunaomba tunatia msisistizo kwamba barabara zile ziendelee kuimarishwa ili ziwe vizuri hata kama kukitokea suala lolote kusiwe na tatizo jinsi ya kupita kwenye zile barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sina mengi ya kuongea kwenye Wizara hii ila ombi langu naomba tusishike shilingi tuwaache Wizara hii wapewe pesa zao vizuri ili waweze kufanya majukumu yao vizuri, kwa kweli wanajitahidi, wanafanya kazi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)