Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi na mimi kuchangia Wizara hii muhimu. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenipa nguvu kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake kwa kazi nzuri wanayoifanya lakini pia nimpongeze kwa unyenyekevu ambao kwa kweli amekuwa akiuonesha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hii ni Wizara ambayo ni muhimu mimi naweza nikasema ndiyo moyo wa nchi, ni Wizara ambayo imetuletea heshima kubwa ndani na nje ya nchi kwa kweli Jeshi letu linasifika sana na ninawapongeza na niseme moyo huo wa kujitolea kuhakikisha Taifa linakuwa salama, uendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako mambo machache ambayo mimi nitashauri; kwa upande wangu mimi ninapakana na nchi ya Rwanda na Uganda, mipaka yetu iko salama, lakini nilikuwa ninaomba kuna Kata ya Kitwechenkula pale kuna mambo ambayo yanafanyika kwenye mpaka wetu kwa raia wetu siyo mambo mazuri. Niliombe Jeshi letu liangalie na ikiwezekana pale hatapawepo na kambi itapendeza kwa sababu wenzetu upande wa pili wao wana kambi na sisi tukiweka pale kambi nafikiri tutaheshimiana vizuri. Kwa hiyo niombe sana Serikali na Wizara hii iliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo mimi nilete pale kwenye Kata ya Kaisho kuna kambi isiyo rasmi, ile kambi iko katikati ya raia na unajua raia hawajazoea kuona majeshi kama hakuna ulazima wa ile kambi kuwepo pale iko barabarani kwanza hata kwa wanajeshi wetu inaweza wasiwe salama kwa sababu wako katikati ya wananchi hakuna uzio ni barabarani kwahiyo niombe sana Wizara iliangalie kama hakuna ulazima wa kambi ile kuwepo pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine Jeshi letu limefanyakazi kubwa sana na mkiona Taifa hili liko salama ni kwa sababu ya kazi nzuri inayofanywa na Jeshi letu sasa mimi nilikuwa ninaomba wakati mwingine wameeleza hapa ukiangalia nyumba za askari wetu kwa kweli unajiuliza hawa watu wanaosababisha Taifa liwe salama leo hii tuko hapa tumetulia kwasababu ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama mipaka yetu iko salama. Nchi nyingine hawawezi wakakutana namna hii hebu tuangalie namna gani tunaweza tukaboresha makazi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi nimekuja na hoja nyingine ikiwezekana hawa wanajeshi wanapostaafu wawe na bima ya maisha, kwa sababu tumeshawatumikisha wamechoka wanapostaafu hata hawana uwezo tena hawana nguvu kwa sababu nguvu kubwa wameiwekeza huku kupigana na kuhakikisha mataifa mengine yanakuwa salama. Kwa hiyo, tuhakikishe tunawapa bima ya maisha kama zawadi kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya. Kwa hiyo hilo ndilo ombi langu ambalo nimelileta kwenu na Waziri aliangalie pamoja na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ninaunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)